Umuhimu wa Kupaki gari lenye kutumia automatic transimission kwa usahihi

Toofast

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2015
Posts
522
Reaction score
942
Hii ni special kwa wasio kuwa na uelewa wa kupaki gari lenye automatic transmission kwa usahihi.

Hatua ni kama zifuatavyo:

1. Kikawaida gari likiwa kwenye drive au reverse ukiwa unajiandaa kupaki, cha kwanza kabisa ni kukanyaga breki ya mguu na kushift hadi kwenye neutral.
2. Kisha baada ya hapo utavuta breki ya mkono na kuachia breki ya mguu kwa sekunde kadhaa kwa ajili ya kuruhusu uzito wa gari ushikiriwe na breki ya mkono.
3. Kisha utakanyaga tena breki ya mguu na kushift hadi kwenye parking.
4. Kisha kuzima gari.

Umuhimu ni kwamba hizi hatua zinasaidia kulinda gearbox isiwe inabeba uzito wa gari kwa muda mrefu ukiwa umepaki. Kwa hiyo, uzito utakuwa unashikiliwa na breki ya mkono, na gearbox itadumu kwa muda mrefu.

Naongea hivi kwa sababu mimi nishawahi kupata matatizo yatokanayo na kutokufuata hatua za hapo juu. Mfano:

1. Gari lilikuwa likichengi gear kutoka parking kwenda drive na kuna sauti ya kitu kugonga ilikuwa inatoka. Lakini ATF ipo ya kutosha na safi, vile vile na mounting ni nzima.

2. Gari kuna wakati linachelewa kuchenji gia (delay shifting), lakini ATF ipo full tena ni safi na haina mileage kubwa.

Angalizo: Hizo hatua hapo juu haziwahusu wale wenye magari ambayo yana electronic parking brake, kwa sababu mimi sina uzoefu na gari hizo.

Hitimisho: Uzi tayari karibuni kuchangia, na najua wajuaji hawatakosekana.
 
Ipo hivi kwanza inashauriwa break ya mkono (handbrake) utumie pale tu inapobidi hasa kwenye miinuko lakini tafouti na hivyo kama unapaki sehemu tambalale weka kwenye P tu inatosha kwani handbrake kidogo kina shida kwenye kukirekebisha kinapoleta itata hivyo kinastahili kulindwa pia
 
breki ya mkono haitumiwi kwenye miinuko pekee mzee inatumika pia hata kama umepaki kwenge mteremko ,vilevile hata kwenye foleni na hii huwezi kujua umuhimu wake mpka itokee siku gari unayoendesha igongwe kwa nyuma
 
du,hii mpya kabisa..sijawahi kuisikia,labda ngoja wajuaji wengine waje wachangie..
 

Somo zuri sana mkuu...
 

Kwanza kabisa general name ni parking brake. Maana siyo zote zinakuwa operated na mikono. Gari kama Spacio, Premio, n.k. parking brake zake zinakuwa operated na mguu.

Pili, I wish ungejua parking mechanism ya gearbox ilivyo. Aiseeee haiko kimayai mayai. Ni tough.

Tatu, Parking mechanism has nothing to with matatizo ya gearbox ambayo uliyapata. Sijui kuchelewa kubadili gear au mshtuko.

Ni hivyo tu.
 
Nilikuwa nangoja comment kutoka kwa huyu jamaa[emoji16]

Thread closed!
 
breki ya mkono haitumiwi kwenye miinuko pekee mzee inatumika pia hata kama umepaki kwenge mteremko ,vilevile hata kwenye foleni na hii huwezi kujua umuhimu wake mpka itokee siku gari unayoendesha igongwe kwa nyuma
Mie nikisema kwenye miinuko wewe ukasema kwa kunipinga kua hata kwenye miteremko bado sijaona tofauti maana palipo na miinuko automatically kuna miteremko sijaelewa point yako ilikuwa nini ila nimecheka zaidi eti Hadi kwenye foleni unavuta handbrake duh
 
mzee nashukuru kwa mchango wako
ni kweli parking mechanism ni tough lkn unavopaki gari bila kufata hatua za hapo juu ,unakuwa unaiuwa gearbox taratibu hususani kama unapaki sehemu yenye kilima yaani ingekuwa ugonjwa ningeweza kusema hilo tatizo basi ni kansa,halitokei yaani ghafla Ila baada ya gari kuwa na mileage za kutosha ndo utaanza kuona effects zake
 
acha kukariri kwamba eti kila sehemu yenye mwinuko basi itakuwa mbele na mteremko samahani lkn kwani hujawahi kuona gari limepaki kwenye sehemu Ina muinuko halafu ndo mwisho wa barabara au parking area ,basi point yangu mi imebase sanasana kwenye sehemu Kama hizo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…