Umuhimu wa kuwalipa wasanii pesa inayowawezesha kuishi bila kujichanganya na jamii

Umuhimu wa kuwalipa wasanii pesa inayowawezesha kuishi bila kujichanganya na jamii

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Msanii ni kioo cha jamii na jamii ina watu wenye uwelewa tofauti na hupokea ujumbe katika mapokea tofauti. Mfano tamdhilia ina kipengele cha mama wa kambo mtesi wa watoto. Nia ya sanaa ni kuweka wazi matendo yanayoendelea katika jamii lakini kuna watakao pokea na kumchukia yule msanii hasa kama wale watoto wanaoteswa wameshakua icon ya taifa.

Sasa msanii anaamua kupanda basi kituo cha Mbezi anakwenda Mbeya amepata udhuru. Anaweza kutokea mhuni mmoja amchape makofi akimwambia weww mtesi wa watoto. Ni muhimu sana kwa wasanii kuwezeshwa kutumia usafiri binafsi na wakikutana na mashabiki iwe katika haki ya usalama wakiwa kama mastaa.

Nchi za Magharibi wasanii wengine hasa chipukizi wanalalamika kuwa malipo ni madogo. Huko ambako magwiji wa sanaa wanatengeneza pesa ya kueleweka. Nchi za Afrika wasanii wetu wanafanya kazi kulinda majina tu na kuoata nafasi ya kuonyesha sura kwenye screen.

Kuna dada mmoja kule Nigeria amechomoa battery baada ya kusema hela wanayoitegemea kuishi ni hela wanazohongwa na ma sponsor ambao wengi wao ni viongozi wandaamizi serikalini. Huyu dada alienda mbali na kusema sponsor wako akiwa mzito basi utaonekana kwenye tamthilia na filamu zinazobamba.
 
Unachojaribu kutetea mtoa mada

Ndo kimefanya wasanii wengi kuishi maisha feki yasiyoendana na kipato chao halisia.

Inapotokea kayumba kidg kisanaa,
Ndo unakua mwanzo wake wa kufilisika HARAKA Sana maana matumizi yake yatabaki pale pale, humu kipato kimeshuka.

Mf:
Nguo ya elfu 50 maduka ya kawaida,
Kwasababu Ni msanii atatakiwa ainunue kwa laki 5 maduka classic kwa Kuhofia jamii itamchukuliaje.

Wakati nguo Ni ile ile imetoka kwa mzalishaji mmoja.
 
Back
Top Bottom