Umuhimu wa Mfumo Dume (Ubaba)

Umuhimu wa Mfumo Dume (Ubaba)

Because men and women are wired differently.
Niambie basi hiyo tofauti maana ndo nina shauku nayo...

Nimesoma pg ya nyuma mwenzio Anhauser kasema anaenda kumtafuta aliyemzidi kipato...
 
Kuchakarika bana ndo mpango mzima kwa mwanamke na mwanamme...

Nani anataka mwenza mvivu asiyepigania maisha? Lakini hamjanishawishi kwa kusema pesa ndo msingi....yapo mengi ya msingi kwenye mahusiano.

Wewe upo tayari kuishi na mume milionea amabye hakuheshimu?

Mimi staki usawa hapo, ni mfumo dume ufanye kazi mwanzo mwisho.

Mimi nachakarika lakini na yeye achakarike tena zaidi yangu

Kipato chake kikiwa kikubwa zaidi yangu ninafurahi sana 😀
 
piga ua galagaza ..... Pesa ni muhimu...
Mwanamke anahitaji kuwa na uhakika wa kesho...kwamba atakula, watoto watasoma nk

huitaji kuwa tajiri..... Unahitaji kuwa na pesa ya kuyimiza mahitaji. Na hupendeza zaidi mwanaume akiwa na kipato kumzidi mwanamke........

Unafikiri bila pesa, njaa tumboni hapo hata mapenzi yananoga?
Mambo Badili? Nakuunga mkono,kichwa,miguu na niniliyuuuu.........
 
Baada ya makuzi mema yanayopingana na mfumo dume sasa ni wakati wa kuuangalia upande wa pili wa shilingi. Kwanza kabisa tafsiri ya neno patriarchy ambalo wanaharakati wa jinsia wanadai ni mfumo dume sio sahihi. Tafsiri yake halisi ni ubaba. Hii ni hali ya uongozi ama utawala uliojikita katika baba akisaidiwa ama kusaidiana na mama.

Wanaokubaliana na patriarchy inayotafsiriwa kama ubaba wanaamini kazi kubwa ya ubaba ni 'p' tatu yaani protecting (kulinda), providing (kutoa) na preside (kuongoza) japo wapo wanaodai p ya tatu ni profess (kuaminisha). Kama tulivyoona kwenye mjadala wa maamuzi, mapenzi hayawezi kwenda bila ubaba huu wa kuongoza, kulinda na kutoa.

Pamoja na kupinga ukatili wa mfumo dume ukweli ndio huo, ili mapenzi yafanikiwe lazima ubaba uongoze. Na tunapoongelea kutoa tunaongelea pesa - bila fedha penzi linakuwa mahututi na mwisho wake ni kufa tu. Pesa posa.

Its true lakn nadhani wababa wenyewe hawaelewi majukumu yao au hawajitambui wana nafasi gani.Matokeao yake wanatumia vibaya huu mfumo dume(ubaba)
 
Kumbuka mwanaume mnajisikia wakamilifu pale mnapoweza kutimiza mahitaji yote ya familia....... Kwa hiyo naweza kusema mnahitaji hilo on a different way..... Ndo maana mwanaume anapotaka mwanamke mwenye kipato si kwa ajili ya kutimiziwa hilo bali kama back up siku akishindwa mke amsitiri hadi atakaporecover, ila si mke achukue nafasi yake la hasha......


Na mwanaume hahitaji?
 
kuitwa baba kunaambatana na mambo flani ambayo lazima uyatimize vinginevyo hadhi au cheo cha kuwa baba kinashuka.
na mambo hayo yanahitajo pesa na hiyo pesa inategemea familia yako iko katika class level gani.
Baba lazima utoe mahitaji kwa famila yako. Hapa wanawake wanaweza sema mbona kuna wanawake wengi ndio wanahudumia familia zao?
Lakini inawezekana ni 1 au 3 kati ya 100 hivyo basi ni minor cirumstances.
Mimi magazeti na kutembelea mitandao mingi ya kijamii. Uwa naona watu wakitafuta wachumba.
Kati ya matangazo 10 ya wanawake wanao tafuta wachumba atleast 8 kama sio wote lazima kati ya sifa watakazo taja ya mwanaume wamtakaye watasema awe ana kazi tofauti na wanaume ambao wao usema tu sifa za kimwili na elimu ya secondary.
Je hii inamaanisha nini kwa wanawake kudemand mwanaume mwenye kazi?
Ina maanisha kwamba awe provider na inaonesha kwamba baba awe na uwezo wa kuendesha familia financially
 
Niambie basi hiyo tofauti maana ndo nina shauku nayo...

Nimesoma pg ya nyuma mwenzio Anhauser kasema anaenda kumtafuta aliyemzidi kipato...

Ego ya kiume haikubali na ndio maana Anheuser akasema anaenda kutafuta ambae kipato chake (huyo mwanamke) kipo chini

Katika hali ya kawaida mwanamme hapendi mwanamke kumzidi kipato
 
Enzi za babu zako ardhi,ng'ombe,mbuzi etc ndo vilikuwa msingi wa mapenzi for a simple reason kwamba in those yesteryears those items were the currency of the day.No money no love bana asikudanganye mtu,binadamu haishi kwa longolongo bana anaishi kwa mkate (and of course pia kwa a good action in the sack!).

Bishanga asante sana umeongea jambo safi kweli. Enzi za mababu that was then and this is now.
 
Mimi staki usawa hapo, ni mfumo dume ufanye kazi mwanzo mwisho.

Mimi nachakarika lakini na yeye achakarike tena zaidi yangu

Kipato chake kikiwa kikubwa zaidi yangu ninafurahi sana 😀
Kwa nini lakini? Kwa nini unataka akuzidi?
Ili u,bebebshe majukumu ya familia yeye peke yake?
 
Kwa nini lakini? Kwa nini unataka akuzidi?
Ili u,bebebshe majukumu ya familia yeye peke yake?

Coz it will boost his ego and that is very important for our relationship
 
Niambie basi hiyo tofauti maana ndo nina shauku nayo...

Nimesoma pg ya nyuma mwenzio Anhauser kasema anaenda kumtafuta aliyemzidi kipato...

Jiulize kwa nini mwanaume akidundwa na mwanamke inakuwa fedheha zaidi kuliko akidundwa na mwanaume mwenzake?

Kuna kitu kinaitwa 'male ego'. Hiki kitu kipo na kama wewe sio mwanaume basi unaweza usielewe kabisa lakini sisi wanaume ndiyo tumeumbwa hivyo. We are conquerors, providers, protectors, etc.

Katika setting za kimahusiano na kifamilia kama tukiweza kutimiza yote hayo ambayo tunaona tunatakiwa kuyatimiza basi na roho zetu zinaridhika na tunakuwa na amani.

Sasa kama mkeo ndiyo anavuta mkwanja mkubwa zaidi maana yake ni kwamba hata mchango wake kwenye mahusiano yenu utakuwa mkubwa kumzidi mwanaume na hiyo hali si nzuri kabisa kwa mtazamo wa kiume.

Mbaya zaidi watu wa nje wakijua kuwa mwanamke ndiyo mwenye mkwanja basi maneno hayataisha. Kubali, kataa hii hali kwa mwanaume si nzuri kabisa. Hata upuuze vipi, mimi naamini itakusumbua tu.

Na mwanaume kama ego yake imejeruhiwa hiyo inaweza ikawa chanzo cha stress, depression, na mengine ambayo siwezi kuyaandika hapa!!
 
Hehehee why is it unfortunate? It should be fortunate, dont you think so?

Si unajua tena haki sawa na beijing. Siku hizi wanawake hatutaki kushindwa ati. Mwishowe ndio mwanzo wa cheating katika mahusiano.
 
Coz it will boost his ego and that is very important for our relationship

Hehehee haya bana nimekusoma na hapo juu...'men's ego'...

Kwa hiyo na sisi tukitafuta walotuzidi kipato/wenye pesa wasituite 'gold diggers'
 
Jiulize kwa nini mwanaume akidundwa na mwanamke inakuwa fedheha zaidi kuliko akidundwa na mwanaume mwenzake?

Kuna kitu kinaitwa 'male ego'. Hiki kitu kipo na kama wewe sio mwanaume basi unaweza usielewe kabisa lakini sisi wanaume ndiyo tumeumbwa hivyo. We are conquerors, providers, protectors, etc.

Katika setting za kimahusiano na kifamilia kama tukiweza kutimiza yote hayo ambayo tunaona tunatakiwa kuyatimiza basi na roho zetu zinaridhika na tunakuwa na amani.

Sasa kama mkeo ndiyo anavuta mkwanja mkubwa zaidi maana yake ni kwamba hata mchango wake kwenye mahusiano yenu utakuwa mkubwa kumzidi mwanaume na hiyo hali si nzuri kabisa kwa mtazamo wa kiume.

Mbaya zaidi watu wa nje wakijua kuwa mwanamke ndiyo mwenye mkwanja basi maneno hayataisha. Kubali, kataa hii hali kwa mwanaume si nzuri kabisa. Hata upuuze vipi, mimi naamini itakusumbua tu.

Na mwanaume kama ego yake imejeruhiwa hiyo inaweza ikawa chanzo cha stress, depression, na mengine ambayo siwezi kuyaandika hapa!!
Got you Ngabu....its crystal clear now!
 
Back
Top Bottom