Umuhimu wa wosia


ni kweli kabisa wazazi wako hawakosei
 
Mimi si mwanasheria ila my mum alishampeleka baba mahakamani kwa hiyo najua sheria ya ndoa inasema nusu ya mali ni ya mke na nusu ni ya mume. Na watoto hawana chao once marriage inapo end, ni juu ya wazazi kama watapenda kuwapatia hao watoto chochote.

Sasa inakuwa vipi mume akifa afu akaandika mali zake zote kwa anaowapenda yeye na kuto mpa chochote wife au kumpa wife kiduuuchu. Je mahakama haiwezi kubatilisha will kama hiyo??? Taking into consideration kuwa mali ni yao wote kisheria?

 
Wezetu wa mbele huko (wazungu)ni kitu cha muhimu sana lkn huku kwetu wazee wakiambiwa wanaona km wanchuriwa kufa au watoto wana tamaa ya mali, ila kiukweli ni muhimu sana kuandika wosia.

Kama mi baba yangu ukimwambia atakukata jicho moja halafu maneno utakayoambiwa we mwenyewe utachoka, wazee wetu bwana wanaona ni kama uchuro na wasivyopenda kufa lol. Yaani huu ushauri bishanga ni mzuri ila nilivyokumbuka baba yangu ambavyo huwa anareact ukimwambia nimejikuta nacheka kwa kweli
 

Nyumba kubwa hii ishu imetokea kwa jirani yetu hapa wiki chache zilizopita, kisheria mume akifa mke anapewa nusu ya mali halafu watoto wanapewa ile nusu iliyobaki wagawane haijalishi huyo mke alizaa na huyo mume au la mradi wawe tu wamefunga ndoa halali.
 
Haifai hata kidogo kutegemea mali za urithi.

Kabisa husninyo mi huwa namwambia kabisa binti yangu ingawa ni mdogo, soma mama huu ndio urithi wako ninachojitahidi ni kubanana na baba yako upate elimu nzuri itakayokusaidia akikua ataelewa nilikua namaanisha nini na akichezea maisha vile vile ni yeye wa kujilaumu na si kuja kulilia urithi sijui wa baba au wa mama. We umeshaona kijana msomi anagombania urithi? huwa anajua kabisa hizi mali hata mimi nina uwezo wa kuwa na zangu ni hao wazurulaji na wavuta bange ndio wanaogombaniaga
 
hongera kwa kumkazania binti yetu asome manake unanipunguzia ile kazi,lol! ila usiombe aisee, kuna mijitu imesoma na ina wajukuu wasomi na bado inagombea mali za ndugu zao! ni issue ya utu tu aisee,tabia haina dawa. nilikutana na shosti mmoja mahakamani baba yao kafariki,baba mdogo anaishi uingereza na wanae wametapakaa dunia nzima. ameweka na wakili kabisa anagombea nyumba ya marehemu na anasema hamtambui mke wa kakake.hapo wamekuja mahakamani huyo mdada (30+), mamake na mdhamini wa ndoa wa wazazi. watu wana roho ndogo,acha kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…