Hypolite
JF-Expert Member
- Jul 6, 2017
- 235
- 484
Maduka ya rejareja yanayouza vitu vinavyonunulika kwa haraka(Fast moving consumable goodsi.e sukar, ngano, sembe&N.k hua ni mengi sana mitaani tunamoishi na yamekaribiana yahitaji akili & mbinu zakufanya biashara kaitka mazingira ya namna hii.
Mtu mmoja aliwahi nambia ni heri afanyie biashara sehemu yenye ushindani na soko lina pesa (liquidity) kuliko kufanyia biashara eneo leny ushindani mdogo ila lisilo na pesa (illiquid market)
Yafuatayo ni mambo kadhaa uwezayo kufanya ukajiweka kweny nafasi nzuri yakuhakikisha unashindana vilivyo vyema na kuwa na kua na mzunguko mzuri wa pesa.
Epuka kufanya kijiwe sehemu ya biashara yako kwa gharama yeyote ile, ushikaji na ushosti haupaswi kufumbiwa macho sehemu ya biashara na ukumbuke hili ukiwa muuzaji ni wa kike na mashosti hujaa kweny biashara yako kupiga stori basi tambua kabisa jinsia yakiume itakupita kama haioni kuna duka kwako nakwenda kununua fremu inayofuata vivyo hivyo kwa muuzaji wakiume unayeruhusu kijiwe kupiga stori na washikaji sehemu ya biashara, ondoa vivutio vinavyotengeneza mazingira yakijiwe kama benchi biashara yako haina muundo wa mteja kununua na kukaa kama mgahawa.
Usihodhi pesa ya biashara kama unahitaji kuikuza biashara yako, kumbuka kua upo kweny biashara ya kujumua na kuuza kwa rejareja (Trading business), hivo hakikisha mauzo yanabadilika kua bdhaa, jitahidi kununua bidhaa kila pesa inayoipatikana kulingana na mauzo(back to back reinvesting) na gharama kama vile za vyakula havikwepeki ukitumia kwa sku gharama ya 2000 kwa ajili ya chakula hakikisha hyo hyo sku utaingiza bidhaa yenye faida kubwa kuzidi 2000(+2000) kwa namna hyo utazimudu gharama zako binafsi huku unaikuza biashara yako kumbuka una mtaji mdogo na faida za duka la rejareja ni ndogo hivo ni rahisi mno kujikuta unakula mtaji badala ya faida.
Epuka kuuza hamna, najua mtaji ni mdogo ila yafaa kuhakikisha una vitu vinavyohitajika na soko, ikiwezekana usichukue katika mfumo wa carton chukua katika idadi ndogo kama supplier wako anakubali kufumua carton ili uweze pia kununua na bidhaa zingine usikusanye pesa mpaka ifike yakuhemea mzigo mkubwa hakikisha unanunua na kununua tena, ukomo ni pale duka la jumla limefungwa kwakua maduka ya jumla huwahi kufunga hivyo nunua bdhaa pesa ya mauzo ya kila sku mpaka sekunde ya mwishio kabla supplier hajafunga, usiende kulala na pesa ambayo ungeinunulia bidhaa hujijengi unajiharibu hakikisha unafuatilia mzunguko wako wa pesa kama unazidi kuongezeka(Money going out to buy goods&money comi ng in after selling)
Usikae mbali na biashara kiasi cha mteja kuita "dukaaaaaaaaaani" kumbuka hili ni duka la vitu vidogovidogo kama pipi, jojo, biscuits pia hivo sio rahisi mtu kukuinua ukiwa mbali huku anahitaji kununua jojo za 100 mteja ataona aibu kukusumbua kisa 100 ataenda
Mlango unaofuata muuzaji alipo anapotakiwa kuwa kama muuzaji, tayari mpaka hapo utakua umeshapoteza pato la 100
Epuka kukopesha mali kwa mteja, kumbuka muundo wa biashara yako ni kujumua nakuuza sio kujumua na kukopesha ufanyapo kukopesha ni kama kutengeneza tuta katka mfereji unaotiririsha maji, kumbuka ukopeshapo mteja ajapo kukulipa hakulipi na riba na kama ungezungusha hyo pesa kwenye mzunguko ingezaa hivo jitahidi kutokukopesha.
Kua shapu mikononi, wateja hupenda kuhudumiwa haraka na kuondoka hivo yafaa uwe haraka katika upimaji wa vitu kama sukari, ngano, sembe nakufungashia wateja kwa uharaka iwezekanavyo
Tumia simu kununua bidhaa & delivery (uwasilishwaji wa bidhaa mlangoni pako) kama supplier wako anafanya delivery kwa muda utumapo order yako basi hakuna haja yakuliacha duka au kulifunga kwa muda (temporary close) muda unaoutumia kwenda kununua huku nyuma unapoteza mapato wateja wajapo kama unauwezo wakupata kijana mwaminifu na mchapa kazi mzuri basi hakikisha yeye anakusogezea bdhaa nawe unakuepo dukani mara nyingi biashars ndogo za mitaani zinakosa kitu kiitwacho leverage other peoples resource, other peoples time badala yake hua ni my time, my resource.
Lets engage waweza ongezea point kadhaa mkuu tupate kujifunza sote.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mtu mmoja aliwahi nambia ni heri afanyie biashara sehemu yenye ushindani na soko lina pesa (liquidity) kuliko kufanyia biashara eneo leny ushindani mdogo ila lisilo na pesa (illiquid market)
Yafuatayo ni mambo kadhaa uwezayo kufanya ukajiweka kweny nafasi nzuri yakuhakikisha unashindana vilivyo vyema na kuwa na kua na mzunguko mzuri wa pesa.
Epuka kufanya kijiwe sehemu ya biashara yako kwa gharama yeyote ile, ushikaji na ushosti haupaswi kufumbiwa macho sehemu ya biashara na ukumbuke hili ukiwa muuzaji ni wa kike na mashosti hujaa kweny biashara yako kupiga stori basi tambua kabisa jinsia yakiume itakupita kama haioni kuna duka kwako nakwenda kununua fremu inayofuata vivyo hivyo kwa muuzaji wakiume unayeruhusu kijiwe kupiga stori na washikaji sehemu ya biashara, ondoa vivutio vinavyotengeneza mazingira yakijiwe kama benchi biashara yako haina muundo wa mteja kununua na kukaa kama mgahawa.
Usihodhi pesa ya biashara kama unahitaji kuikuza biashara yako, kumbuka kua upo kweny biashara ya kujumua na kuuza kwa rejareja (Trading business), hivo hakikisha mauzo yanabadilika kua bdhaa, jitahidi kununua bidhaa kila pesa inayoipatikana kulingana na mauzo(back to back reinvesting) na gharama kama vile za vyakula havikwepeki ukitumia kwa sku gharama ya 2000 kwa ajili ya chakula hakikisha hyo hyo sku utaingiza bidhaa yenye faida kubwa kuzidi 2000(+2000) kwa namna hyo utazimudu gharama zako binafsi huku unaikuza biashara yako kumbuka una mtaji mdogo na faida za duka la rejareja ni ndogo hivo ni rahisi mno kujikuta unakula mtaji badala ya faida.
Epuka kuuza hamna, najua mtaji ni mdogo ila yafaa kuhakikisha una vitu vinavyohitajika na soko, ikiwezekana usichukue katika mfumo wa carton chukua katika idadi ndogo kama supplier wako anakubali kufumua carton ili uweze pia kununua na bidhaa zingine usikusanye pesa mpaka ifike yakuhemea mzigo mkubwa hakikisha unanunua na kununua tena, ukomo ni pale duka la jumla limefungwa kwakua maduka ya jumla huwahi kufunga hivyo nunua bdhaa pesa ya mauzo ya kila sku mpaka sekunde ya mwishio kabla supplier hajafunga, usiende kulala na pesa ambayo ungeinunulia bidhaa hujijengi unajiharibu hakikisha unafuatilia mzunguko wako wa pesa kama unazidi kuongezeka(Money going out to buy goods&money comi ng in after selling)
Usikae mbali na biashara kiasi cha mteja kuita "dukaaaaaaaaaani" kumbuka hili ni duka la vitu vidogovidogo kama pipi, jojo, biscuits pia hivo sio rahisi mtu kukuinua ukiwa mbali huku anahitaji kununua jojo za 100 mteja ataona aibu kukusumbua kisa 100 ataenda
Mlango unaofuata muuzaji alipo anapotakiwa kuwa kama muuzaji, tayari mpaka hapo utakua umeshapoteza pato la 100
Epuka kukopesha mali kwa mteja, kumbuka muundo wa biashara yako ni kujumua nakuuza sio kujumua na kukopesha ufanyapo kukopesha ni kama kutengeneza tuta katka mfereji unaotiririsha maji, kumbuka ukopeshapo mteja ajapo kukulipa hakulipi na riba na kama ungezungusha hyo pesa kwenye mzunguko ingezaa hivo jitahidi kutokukopesha.
Kua shapu mikononi, wateja hupenda kuhudumiwa haraka na kuondoka hivo yafaa uwe haraka katika upimaji wa vitu kama sukari, ngano, sembe nakufungashia wateja kwa uharaka iwezekanavyo
Tumia simu kununua bidhaa & delivery (uwasilishwaji wa bidhaa mlangoni pako) kama supplier wako anafanya delivery kwa muda utumapo order yako basi hakuna haja yakuliacha duka au kulifunga kwa muda (temporary close) muda unaoutumia kwenda kununua huku nyuma unapoteza mapato wateja wajapo kama unauwezo wakupata kijana mwaminifu na mchapa kazi mzuri basi hakikisha yeye anakusogezea bdhaa nawe unakuepo dukani mara nyingi biashars ndogo za mitaani zinakosa kitu kiitwacho leverage other peoples resource, other peoples time badala yake hua ni my time, my resource.
Lets engage waweza ongezea point kadhaa mkuu tupate kujifunza sote.
Sent using Jamii Forums mobile app
=======
PIA, SOMA MADA HII:
Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu - JamiiForums
PIA, SOMA MADA HII:
Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu - JamiiForums