Una mipango gani kwa miaka 10-20 ijayo?

Una mipango gani kwa miaka 10-20 ijayo?

You can't choose your fate... Okay??
Hapa sasa ni mtazamo mwingine kabisa kwenye maisha. Mimi siamini kwenye vitu 3: miujiza, bahati na hatma.

Kila maamuzi ninayofanya yana-reflect maisha ninayoishi sasa. So, your point isn't valid in my opinion.
 
Ufanye nini? Zaidi ya kula na kulala sioni cha ajabu
 
Habari wana-JF. Kama tunavyojua mpango kazi kwenye maisha ndiyo dira itakayokuongoza katika maisha yako na kufikia malengo yako.

Kwangu nahisi safari ndiyo kwanza inaanza na maamuzi yangu ya leo yatakuwa na mchango mkubwa kwa maisha ya baadaye.

Nikiwa kwenye early 20s (23) tayari nipo kwenye first phase ya mpango kazi wangu. Mimi shule nilikuwa siipendi kabisa kwa miaka 11 yote niliyosoma elimu ya msingi mpaka sekondari ila mtazamo wangu ulibadilika baada ya kujiunga chuo nikiwa na 18 na kuanza kusoma kile ninachokipenda.

Toka nikiwa mdogo nilikuwa ni mtu ninayependa kutumia teknolojia ya computer ni kwasababu ilikuwepo nyumbani na mzee wangu alinifundisha nilipokuwa mdogo sana. Nilipenda kucheza games na kufanya simple tasks mbalimbali. Mimi ni mmoja wa Gen Z niliyetumia Windows XP miaka hiyo.

So baada ya kumaliza sekondari nilijua nataka kusomea nini basi moja kwa moja nikainza safari yangu kwenye field ya Information Technology, miaka yote niliifurahia mpaka nilipohitimu kwa ngazi ya Diploma.

Sasa ukiachana na hiyo historia (intro) fupi mpango kazi wangu umegawanyika katika phase 2.

1st phase: 10 years
2nd phase: 10 years

So huu ni mpango kazi wa miaka 20 ijayo. Kwenye first phase ndiyo msingi unapoanzia, kitakachofanyika hapa ndiyo kitaleta picha ya kitakachotokea baada ya miaka 20.

1. Natumaini nitakuwa hai kwa miaka 20 ijayo.

2. Nataka niweze kufanya vitu ninavyovifanya kwenye early 20s kwa uwezo uleule au kwa ufanisi zaidi ya sasa. Hapa ni afya kuwa bora zaidi.

3. Nataka kuamua namna maisha yangu ya baadaye yatakuwa, na siyo magonjwa kuamua muda wangu wa kuishi duniani. Hapa ni kwa kuwa makini zaidi na afya yangu ya akili mpaka mwili.

4. Nataka kuishi kwa miaka 20 ijayo.

1st phase:

1. Career Building. Hapa nataka kujenga career yangu kwenye Web Development & Graphic Design (Freelancer) ndiyo kitu ninachifanya kwa sasa ila ninapotaka kufika ni safari ndefu ambayo siwezi kufika kwa usiku mmoja ndiyo maana ujenzi wa career yangu upo kwenye first phase. Malengo ni kuwa bora kwenye hizo field: bora kweli.

2. Education. Kwenye first phase ya mpango kazi wangu nataka kujiendeleza kielimu mpaka level ya Bachelor Degree. Hii naitaka ikiwa ni mwanzo wa safari nyingine kwenye second phase ya mpango kazi wangu.

3. Health. Afya ndiyo kila kitu, afya ndiyo uzima. Bila afya imara huu mpango kazi si kitu. Hivyo jambo la muhimu zaidi ni kulinda na kuimarisha afya yangu ya akili na mwili kwa miaka 20 ijayo. Hapa ni kwa kupata mlo kamili, mazoezi, kuwa na bima ya afya, kuupa mwili na akili mapumziko panapohitajika, kuyapa vipaumbele mambo yatakayonijenga na kunipa furaha zaidi.

4. Family & relationships. Nataka kuwa karibu zaidi na familia yangu: hao ndiyo watu wangu niliokuwa nao toka siku ya kwanza naletwa Duniani na ndiyo watakaokuwa na mimi katika safari ya maisha yangu. Mahusiano ni jambo la muhimu, hii ni safari nyingine kuelekea kujenga familia bora. Lakini sitaki mahusiano yaharibu mpango kazi wangu kabisa, hivyo ni kazi nyingine ya kutafuta mtu sahihi wa kuwa naye.

5. Personal development. Hapa nataka kuwa bora zaidi kwenye Technology na ndiyo njia ya kuijenga career yangu. Nataka kuachana na addiction zote zinazozuia mpango kazi wangu kufanyika kwa 100%.

6. Finance. Hili jambo la muhimu, mwanzo na mwisho wa mpango kazi huu. Nataka kujenga career itakayonipa fursa za kufanya Duniani popote na kunipa kipato kinachoendena na thamani ya kazi nitakayoifanya. Nataka kuweza zaidi kwenye Cryptocurrency & Stocks: elimu hapa ni muhimu zaidi. Nataka kuwekeza kwenye kilimo na ufugaji wa kisasa, hii ndiyo back-up plan yangu japokuwa sitaki kuwa na back-up ni njia ya kwanza kujiona nimefeli kwenye mpango kazi wangu mkuu. Nataka kutafuta fursa nyingi zaidi za uwekezaji, sitaki kujipa limit, kujifunza zaidi ndiyo kufanikiwa zaidi.

7. Adventure. Malengo yangu kwa miaka 10 ijayo ni kusafiri zaidi, hasa nje ya nchi: kujifunza zaidi. Kupanda Mlima Kilimanjaro ni jambo lingine nataka kulufanya katika miaka 10, nilishatembelea Mbuga ya Wanyama ya Serengeti, hivyo kwa utalii Kilimanjaro ni my next target.

#: Kufurahia ujana ni jambo la muhimu zaidi kwasababu unakuja mara moja tu kwenye maisha. Kazi ni lazima ifanyike kwelikweli ila kufurahia maisha kila siku ni kushukuru kwa baraka hii tuliyonayo.

2nd Phase:

1. Education. Lengo kubwa kwenye second phase ya mpango kazi wangu itakuwa ni kujiendeleza kielimu kwa ngazi ya Masters. Hapa nataka kufuata nyayo za mzee wangu aliyehitimu masomo yake ya Masters nchini Netherlands. Nje ya nchi ndiyo lengo langu kuu kupata elimu huko, naamini fursa nyingi zaidi zitapatikana.

2. Family. Hapa sasa naamini ndiyo utakuwa wakati mzuri wa mimi kujenga familia bora baada ya msingi kutengenezwa kwenye first phase.

3. Work career. Hapa sasa ndiyo natarajia kazi kubwa zaidi itafanyika: kufanya kazi, uwekezaji kwa ajili ya kizazi changu.

4. Retirement. Baada ya miaka 20 ijayo natarajia kustaafu nikiwa na miaka 45-50. Ni muda ambao naamini ukifika napaswa kufurahia zaidi maisha na familia yangu bila kuwaza kufanya kazi tena. Lakini hili halitawezekana kama kazi bora na ya uhakika haitafanyika kwenye hii miaka 20 ya mpango kazi wangu.

5. Off-grid. Hapa naaminisha kuishi nje ya mji kabisa na familia yangu, mahali ambako nitafurahia maisha yangu baada ya kuikamilisha kazi kubwa iliyonileta Duniani. Kuwa na farm house ndiyo ndoto yangu kubwa. Kwa Tanzania tayari lipo eneo linalonivutia zaidi kuishi kwenye miaka 20 ijayo.

Yapo mengi ila hapa ni kwa kifupi tu. Ningependa kujua mipango yako kwa miaka 5, 10, 15 au 20 ijayo maana hapa tayari tunatofautiana umri, elimu, vipato.

Nataka kuishi kwa miaka 20 ijayo.
Siri Huwa haiwekwi wazi plus mipango wewe subiria matokeo
 
_20230821_221920.JPG
 
Hongera mkuu,
Hata sisi tulikuwa na mipango na kuiandika sana kwenye MS Word, leo tunaishi tu liende 🤣
 
Hongera mkuu,
Hata sisi tulikuwa na mipango na kuiandika sana kwenye MS Word, leo tunaishi tu liende 🤣
😂😂😂

Si wamasemaga "maisha hayana formula". Kila kitu ni kujaribu, uzuri maisha yanakupa fursa kulingana na uwezo wako. Majani ya juu yakikushinda, kuliko kujifanya Twiga unarudi kula chini tu "kila Mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake".

Ila mpaka una-survive sasa hivi maana yake kuna mpango mwingine umetiki. Muhimu ni kukimbizana na fursa tu "kama kinyonga" unabadilika rangi kuendana na mazingira.
 
OMBA MUNGU USIFE UJIONEE MWENYEWE SCRIPT YAKO 😀
 
OMBA MUNGU USIFE UJIONEE MWENYEWE SCRIPT YAKO 😀
Hahah! Kama nilivyosema ni afya na kifo tu ndiyo vinaweza kukwamisha mpango kutimia. Hivyo ndiyo vitu ambavyo siyo guaranteed na sina uwezo wa kuamua viendaje kwenye maisha yangu.

Hapo juu kuna mdau nilimjibu mimi siamini kwenye vitu 3: miujiza, bahati na hatma. "Script" maana yake ni hatma nikiishi kutimiza yale niliyopangiwa. Mimi siamini hicho, ikitokea nimefeli itakuwa ni kwasababu yangu mwenyewe: labda sikujipanga vizuri au mpango kazi sikuufanyia kazi ipasavyo.

Maisha yangu yapo kwenye mikono yangu mwenyewe, mpaka nilipofika kuna vitu nimefeli kutokana na maamuzi niliyofanya miaka iliyopita.
 
Ndiyo maana nahitaji miaka 20 na inaweza kuchukua hata miaka 30 maana unachokipanga siyo kuwa kitanyooka tu.

Yes! Tanzania ni moja ya disadvantage kwenye mpango wangu. Career yangu naijenga zaidi kwenye freelance na kuna vitu kama serikali inafanya viwe vigumu.
Kwa mipango yako hii ulio ipanga,Hatua ya kwanza ni uondoke Tanzania.

Tanzania ni sehemu ngumu sana kufanikisha hayo uliyo yasema.
 
Hahah! Kama nilivyosema ni afya na kifo tu ndiyo vinaweza kukwamisha mpango kutimia. Hivyo ndiyo vitu ambavyo sina uwezo wa kupanga viendaje kwenye maisha yangu.

Hapo juu kuna mdau nilimjibu mimi siamini kwenye vitu 3: miujiza, bahati na hatma. "Script" maana yake ni hatma nikiishi kutimiza yale niliyopangiwa. Mimi siamini hicho, ikitokea nimefeli itakuwa ni kwasababu yangu mwenyewe: labda sikujipanga vizuri au mpango kazi sikuufanya ipasavyo.

Maisha yangu yapo kwenye mikono yangu mwenyewe, mpaka nilipofika kuna vitu nimefeli kutokana na maamuzi niliyofanya miaka iliyopita.
hongera kwa KUadmit hili,, ilikuaje ukasoma diploma baada ya degree?
umenikumbusha nilivyoacha kozi ya degree kwenda kusoma kozi ya mambo ya madini diploma kipindi hicho inaanzishwa chini ya MH MUHONGO SOSPETER.Yaani sijutii maamuzi yale baada ya kumaliza degree yangu ila ile kozi ningesota ila MUNGU MWEMA NA MIPANGO YAKE.
 
Miaka 10 au 20 ijayo Sina uhakika km ntakua bado naishi kwenye hii Duniani nadhani ntakua kwenye sayari nyingine huko naendelea na Maisha mengine, MUNGU akipanga na wewe unapanga unaweza hata kesho usifike hii ndio ikawa comment yako ya mwisho
 
Kwa mipango yako hii ulio ipanga,Hatua ya kwanza ni uondoke Tanzania.

Tanzania ni sehemu ngumu sana kufanikisha hayo uliyo yasema.
Kulingana na kazi zangu za freelance upo mpango kazi mwingine wa kuondoka Tanzania ila unahitaji pesa kuukamilisha.

Kwa sasa kuna nchi nyingi zinatoa Digital Nomad Visa ila kuna minimum requirements bado sijakidhi vigezo: kwenye kiasi cha pesa ninachopata kwa mwezi ndiyo tatizo.

Nahitaji kufikia €750 - €2,500 kwa mwezi kuwaza kuondoka Tanzania.

Tayari kuna nchi ndani ya Europe ipo kwenye mipango ila bado siuoni kama ni mpango halisia kwa sehemu niliyopo kwasasa katika maisha.
 
Habari wana-JF. Kama tunavyojua mpango kazi kwenye maisha ndiyo dira itakayokuongoza katika maisha yako na kufikia malengo yako.

Kwangu nahisi safari ndiyo kwanza inaanza na maamuzi yangu ya leo yatakuwa na mchango mkubwa kwa maisha ya baadaye.

Nikiwa kwenye early 20s (23) tayari nipo kwenye first phase ya mpango kazi wangu. Mimi shule nilikuwa siipendi kabisa kwa miaka 11 yote niliyosoma elimu ya msingi mpaka sekondari ila mtazamo wangu ulibadilika baada ya kujiunga chuo nikiwa na 18 na kuanza kusoma kile ninachokipenda.

Toka nikiwa mdogo nilikuwa ni mtu ninayependa kutumia teknolojia ya computer ni kwasababu ilikuwepo nyumbani na mzee wangu alinifundisha nilipokuwa mdogo sana. Nilipenda kucheza games na kufanya simple tasks mbalimbali. Mimi ni mmoja wa Gen Z niliyetumia Windows XP miaka hiyo.

So baada ya kumaliza sekondari nilijua nataka kusomea nini basi moja kwa moja nikainza safari yangu kwenye field ya Information Technology, miaka yote niliifurahia mpaka nilipohitimu kwa ngazi ya Diploma.

Sasa ukiachana na hiyo historia (intro) fupi mpango kazi wangu umegawanyika katika phase 2.

1st phase: 10 years
2nd phase: 10 years

So huu ni mpango kazi wa miaka 20 ijayo. Kwenye first phase ndiyo msingi unapoanzia, kitakachofanyika hapa ndiyo kitaleta picha ya kitakachotokea baada ya miaka 20.

1. Natumaini nitakuwa hai kwa miaka 20 ijayo.

2. Nataka niweze kufanya vitu ninavyovifanya kwenye early 20s kwa uwezo uleule au kwa ufanisi zaidi ya sasa. Hapa ni afya kuwa bora zaidi.

3. Nataka kuamua namna maisha yangu ya baadaye yatakuwa, na siyo magonjwa kuamua muda wangu wa kuishi duniani. Hapa ni kwa kuwa makini zaidi na afya yangu ya akili mpaka mwili.

4. Nataka kuishi kwa miaka 20 ijayo.

1st phase:

1. Career Building. Hapa nataka kujenga career yangu kwenye Web Development & Graphic Design (Freelancer) ndiyo kitu ninachifanya kwa sasa ila ninapotaka kufika ni safari ndefu ambayo siwezi kufika kwa usiku mmoja ndiyo maana ujenzi wa career yangu upo kwenye first phase. Malengo ni kuwa bora kwenye hizo field: bora kweli.

2. Education. Kwenye first phase ya mpango kazi wangu nataka kujiendeleza kielimu mpaka level ya Bachelor Degree. Hii naitaka ikiwa ni mwanzo wa safari nyingine kwenye second phase ya mpango kazi wangu.

3. Health. Afya ndiyo kila kitu, afya ndiyo uzima. Bila afya imara huu mpango kazi si kitu. Hivyo jambo la muhimu zaidi ni kulinda na kuimarisha afya yangu ya akili na mwili kwa miaka 20 ijayo. Hapa ni kwa kupata mlo kamili, mazoezi, kuwa na bima ya afya, kuupa mwili na akili mapumziko panapohitajika, kuyapa vipaumbele mambo yatakayonijenga na kunipa furaha zaidi.

4. Family & relationships. Nataka kuwa karibu zaidi na familia yangu: hao ndiyo watu wangu niliokuwa nao toka siku ya kwanza naletwa Duniani na ndiyo watakaokuwa na mimi katika safari ya maisha yangu. Mahusiano ni jambo la muhimu, hii ni safari nyingine kuelekea kujenga familia bora. Lakini sitaki mahusiano yaharibu mpango kazi wangu kabisa, hivyo ni kazi nyingine ya kutafuta mtu sahihi wa kuwa naye.

5. Personal development. Hapa nataka kuwa bora zaidi kwenye Technology na ndiyo njia ya kuijenga career yangu. Nataka kuachana na addiction zote zinazozuia mpango kazi wangu kufanyika kwa 100%.

6. Finance. Hili jambo la muhimu, mwanzo na mwisho wa mpango kazi huu. Nataka kujenga career itakayonipa fursa za kufanya Duniani popote na kunipa kipato kinachoendena na thamani ya kazi nitakayoifanya. Nataka kuweza zaidi kwenye Cryptocurrency & Stocks: elimu hapa ni muhimu zaidi. Nataka kuwekeza kwenye kilimo na ufugaji wa kisasa, hii ndiyo back-up plan yangu japokuwa sitaki kuwa na back-up ni njia ya kwanza kujiona nimefeli kwenye mpango kazi wangu mkuu. Nataka kutafuta fursa nyingi zaidi za uwekezaji, sitaki kujipa limit, kujifunza zaidi ndiyo kufanikiwa zaidi.

7. Adventure. Malengo yangu kwa miaka 10 ijayo ni kusafiri zaidi, hasa nje ya nchi: kujifunza zaidi. Kupanda Mlima Kilimanjaro ni jambo lingine nataka kulufanya katika miaka 10, nilishatembelea Mbuga ya Wanyama ya Serengeti, hivyo kwa utalii Kilimanjaro ni my next target.

#: Kufurahia ujana ni jambo la muhimu zaidi kwasababu unakuja mara moja tu kwenye maisha. Kazi ni lazima ifanyike kwelikweli ila kufurahia maisha kila siku ni kushukuru kwa baraka hii tuliyonayo.

2nd Phase:

1. Education. Lengo kubwa kwenye second phase ya mpango kazi wangu itakuwa ni kujiendeleza kielimu kwa ngazi ya Masters. Hapa nataka kufuata nyayo za mzee wangu aliyehitimu masomo yake ya Masters nchini Netherlands. Nje ya nchi ndiyo lengo langu kuu kupata elimu huko, naamini fursa nyingi zaidi zitapatikana.

2. Family. Hapa sasa naamini ndiyo utakuwa wakati mzuri wa mimi kujenga familia bora baada ya msingi kutengenezwa kwenye first phase.

3. Work career. Hapa sasa ndiyo natarajia kazi kubwa zaidi itafanyika: kufanya kazi, uwekezaji kwa ajili ya kizazi changu.

4. Retirement. Baada ya miaka 20 ijayo natarajia kustaafu nikiwa na miaka 45-50. Ni muda ambao naamini ukifika napaswa kufurahia zaidi maisha na familia yangu bila kuwaza kufanya kazi tena. Lakini hili halitawezekana kama kazi bora na ya uhakika haitafanyika kwenye hii miaka 20 ya mpango kazi wangu.

5. Off-grid. Hapa naaminisha kuishi nje ya mji kabisa na familia yangu, mahali ambako nitafurahia maisha yangu baada ya kuikamilisha kazi kubwa iliyonileta Duniani. Kuwa na farm house ndiyo ndoto yangu kubwa. Kwa Tanzania tayari lipo eneo linalonivutia zaidi kuishi kwenye miaka 20 ijayo.

Yapo mengi ila hapa ni kwa kifupi tu. Ningependa kujua mipango yako kwa miaka 5, 10, 15 au 20 ijayo maana hapa tayari tunatofautiana umri, elimu, vipato.

Nataka kuishi kwa miaka 20 ijayo.
Kila lakheli mkuu....

1. Career Building. Hapa nataka kujenga career yangu kwenye Web Development & Graphic Design (Freelancer) ndiyo kitu ninachifanya kwa sasa ila ninapotaka kufika ni safari ndefu ambayo siwezi kufika kwa usiku mmoja ndiyo maana ujenzi wa career yangu upo kwenye first phase. Malengo ni kuwa bora kwenye hizo field: bora kweli.


Mdogo angu Dunia imebadilica sana nakupa huu ushuuda wa mdogo wetu cousin last born...

Mwaka 2021 alimaliza bachelor degree upande wa computer science na jua computer science ni wide sanaaaa...

Dogo akahudhuria Kila interview kuanzia Takukuru, utumishi, Tra hakupata akajiunga na bro angu ana kampuni ya mambo ya finance na accounting software......

Bro alikua anampa kazi za coding sanaaa mda mwingi yupo pekeake jifungia sana ndani mpaka nikagundua izo kazi za software developer Zina damage Brain 🧠🧠 🤣🤣🤣🤣😂😂😂

All in all naona kama umechagua njia yako hongera timiza hitaji la moyo wako stay safe and blessed
 
Habari wana-JF. Kama tunavyojua mpango kazi kwenye maisha ndiyo dira itakayokuongoza katika maisha yako na kufikia malengo yako.

Kwangu nahisi safari ndiyo kwanza inaanza na maamuzi yangu ya leo yatakuwa na mchango mkubwa kwa maisha ya baadaye.

Nikiwa kwenye early 20s (23) tayari nipo kwenye first phase ya mpango kazi wangu. Mimi shule nilikuwa siipendi kabisa kwa miaka 11 yote niliyosoma elimu ya msingi mpaka sekondari ila mtazamo wangu ulibadilika baada ya kujiunga chuo nikiwa na 18 na kuanza kusoma kile ninachokipenda.

Toka nikiwa mdogo nilikuwa ni mtu ninayependa kutumia teknolojia ya computer ni kwasababu ilikuwepo nyumbani na mzee wangu alinifundisha nilipokuwa mdogo sana. Nilipenda kucheza games na kufanya simple tasks mbalimbali. Mimi ni mmoja wa Gen Z niliyetumia Windows XP miaka hiyo.

So baada ya kumaliza sekondari nilijua nataka kusomea nini basi moja kwa moja nikainza safari yangu kwenye field ya Information Technology, miaka yote niliifurahia mpaka nilipohitimu kwa ngazi ya Diploma.

Sasa ukiachana na hiyo historia (intro) fupi mpango kazi wangu umegawanyika katika phase 2.

1st phase: 10 years
2nd phase: 10 years

So huu ni mpango kazi wa miaka 20 ijayo. Kwenye first phase ndiyo msingi unapoanzia, kitakachofanyika hapa ndiyo kitaleta picha ya kitakachotokea baada ya miaka 20.

1. Natumaini nitakuwa hai kwa miaka 20 ijayo.

2. Nataka niweze kufanya vitu ninavyovifanya kwenye early 20s kwa uwezo uleule au kwa ufanisi zaidi ya sasa. Hapa ni afya kuwa bora zaidi.

3. Nataka kuamua namna maisha yangu ya baadaye yatakuwa, na siyo magonjwa kuamua muda wangu wa kuishi duniani. Hapa ni kwa kuwa makini zaidi na afya yangu ya akili mpaka mwili.

4. Nataka kuishi kwa miaka 20 ijayo.

1st phase:

1. Career Building. Hapa nataka kujenga career yangu kwenye Web Development & Graphic Design (Freelancer) ndiyo kitu ninachifanya kwa sasa ila ninapotaka kufika ni safari ndefu ambayo siwezi kufika kwa usiku mmoja ndiyo maana ujenzi wa career yangu upo kwenye first phase. Malengo ni kuwa bora kwenye hizo field: bora kweli.

2. Education. Kwenye first phase ya mpango kazi wangu nataka kujiendeleza kielimu mpaka level ya Bachelor Degree. Hii naitaka ikiwa ni mwanzo wa safari nyingine kwenye second phase ya mpango kazi wangu.

3. Health. Afya ndiyo kila kitu, afya ndiyo uzima. Bila afya imara huu mpango kazi si kitu. Hivyo jambo la muhimu zaidi ni kulinda na kuimarisha afya yangu ya akili na mwili kwa miaka 20 ijayo. Hapa ni kwa kupata mlo kamili, mazoezi, kuwa na bima ya afya, kuupa mwili na akili mapumziko panapohitajika, kuyapa vipaumbele mambo yatakayonijenga na kunipa furaha zaidi.

4. Family & relationships. Nataka kuwa karibu zaidi na familia yangu: hao ndiyo watu wangu niliokuwa nao toka siku ya kwanza naletwa Duniani na ndiyo watakaokuwa na mimi katika safari ya maisha yangu. Mahusiano ni jambo la muhimu, hii ni safari nyingine kuelekea kujenga familia bora. Lakini sitaki mahusiano yaharibu mpango kazi wangu kabisa, hivyo ni kazi nyingine ya kutafuta mtu sahihi wa kuwa naye.

5. Personal development. Hapa nataka kuwa bora zaidi kwenye Technology na ndiyo njia ya kuijenga career yangu. Nataka kuachana na addiction zote zinazozuia mpango kazi wangu kufanyika kwa 100%.

6. Finance. Hili jambo la muhimu, mwanzo na mwisho wa mpango kazi huu. Nataka kujenga career itakayonipa fursa za kufanya Duniani popote na kunipa kipato kinachoendena na thamani ya kazi nitakayoifanya. Nataka kuweza zaidi kwenye Cryptocurrency & Stocks: elimu hapa ni muhimu zaidi. Nataka kuwekeza kwenye kilimo na ufugaji wa kisasa, hii ndiyo back-up plan yangu japokuwa sitaki kuwa na back-up ni njia ya kwanza kujiona nimefeli kwenye mpango kazi wangu mkuu. Nataka kutafuta fursa nyingi zaidi za uwekezaji, sitaki kujipa limit, kujifunza zaidi ndiyo kufanikiwa zaidi.

7. Adventure. Malengo yangu kwa miaka 10 ijayo ni kusafiri zaidi, hasa nje ya nchi: kujifunza zaidi. Kupanda Mlima Kilimanjaro ni jambo lingine nataka kulufanya katika miaka 10, nilishatembelea Mbuga ya Wanyama ya Serengeti, hivyo kwa utalii Kilimanjaro ni my next target.

#: Kufurahia ujana ni jambo la muhimu zaidi kwasababu unakuja mara moja tu kwenye maisha. Kazi ni lazima ifanyike kwelikweli ila kufurahia maisha kila siku ni kushukuru kwa baraka hii tuliyonayo.

2nd Phase:

1. Education. Lengo kubwa kwenye second phase ya mpango kazi wangu itakuwa ni kujiendeleza kielimu kwa ngazi ya Masters. Hapa nataka kufuata nyayo za mzee wangu aliyehitimu masomo yake ya Masters nchini Netherlands. Nje ya nchi ndiyo lengo langu kuu kupata elimu huko, naamini fursa nyingi zaidi zitapatikana.

2. Family. Hapa sasa naamini ndiyo utakuwa wakati mzuri wa mimi kujenga familia bora baada ya msingi kutengenezwa kwenye first phase.

3. Work career. Hapa sasa ndiyo natarajia kazi kubwa zaidi itafanyika: kufanya kazi, uwekezaji kwa ajili ya kizazi changu.

4. Retirement. Baada ya miaka 20 ijayo natarajia kustaafu nikiwa na miaka 45-50. Ni muda ambao naamini ukifika napaswa kufurahia zaidi maisha na familia yangu bila kuwaza kufanya kazi tena. Lakini hili halitawezekana kama kazi bora na ya uhakika haitafanyika kwenye hii miaka 20 ya mpango kazi wangu.

5. Off-grid. Hapa naaminisha kuishi nje ya mji kabisa na familia yangu, mahali ambako nitafurahia maisha yangu baada ya kuikamilisha kazi kubwa iliyonileta Duniani. Kuwa na farm house ndiyo ndoto yangu kubwa. Kwa Tanzania tayari lipo eneo linalonivutia zaidi kuishi kwenye miaka 20 ijayo.

Yapo mengi ila hapa ni kwa kifupi tu. Ningependa kujua mipango yako kwa miaka 5, 10, 15 au 20 ijayo maana hapa tayari tunatofautiana umri, elimu, vipato.

Nataka kuishi kwa miaka 20 ijayo.
Hongera sana mdogo wangu kwa good plan hii plan yako watanzania wengi wakishastaafu ndo wanataka kuwa na financial freedom wakati umri ushaenda.

Mie pia mipango yangu inafanana na yako kasoro we are in diffent professional my main target to retire young but rich then to travel the world.

Hamna kinachoshindika kama Mwenyezi Mungu atakupatia uhai mrefu na Afya nzuri, watanzania wengi huwa wanaamini baada ya kuona matokeo hivyo usikatishwe tamaa na maneno yao...
 
hongera kwa KUadmit hili,, ilikuaje ukasoma diploma baada ya degree?
umenikumbusha nilivyoacha kozi ya degree kwenda kusoma kozi ya mambo ya madini diploma kipindi hicho inaanzishwa chini ya MH MUHONGO SOSPETER.Yaani sijutii maamuzi yale baada ya kumaliza degree yangu ila ile kozi ningesota ila MUNGU MWEMA NA MIPANGO YAKE.
Baada ya kumaliza Secondary Education sikuendelea na Advance kwasababu sikupata ufaulu mzuri kwenye masomo ya Sayansi na option iliyobaki ilikuwa kwenda kusoma Arts. Huko sikuwa na passion na kitu chochote.

Nikafanya uamuzi wa kujiunga na chuo kusoma kile ninachofanya sasa kwa furaha zaidi. Ni uamuzi bora niliofanya kwenye maisha yangu.
 
Miaka 10 au 20 ijayo Sina uhakika km ntakua bado naishi kwenye hii Duniani nadhani ntakua kwenye sayari nyingine huko naendelea na Maisha mengine, MUNGU akipanga na wewe unapanga unaweza hata kesho usifike hii ndio ikawa comment yako ya mwisho
Ni kweli kabisa wote tunaishi kwa matumaini kuwa sekunde 1 ijayo tutakuwa hai na wapo wengi tunavyoandika hapa hawatafika sekunde 1 ijayo.

Kifo ni sehemu ya maisha, haimaanishi tusiwe na mipango kwasababu miaka kadhaa mbele hatutakuwepo.
 
Una plan nzuri, una malengo ya mbali ila kikubwa maisha yana namna yake sio pdf

Nikiwaa na 23 tayar nlikuwa na hyo degree ya IT, graphics nlifanya sana, web nlitengeneza na nlifanyia watu project zile za final year ila maslahi yake ni madogo kikubwa nachoweza kukushauri jaribu kufocus na mtaaa unahitaji nn switch malengo yako vzr lkn jitahidi uwe na multiple streams of income
 
Back
Top Bottom