Una uhakika gani kuwa "sasa hivi" Haupo ndotoni?

Una uhakika gani kuwa "sasa hivi" Haupo ndotoni?

Nimewahi kuota kitu halafu nikiwa ndotoni huko huko nikasema natamani ingekuwa ndoto, baada ya mda nikashtuka kutoka usingizini nikagundua kumbe ilikuwa ndoto nikafurahi sana, maana halikuwa jambo zuri
 
Kuna jamaa aliota kaokota furushi la hela kuliinua kumbe kuna tundu chini akaamua kuliziba na kidole cha kati asubuhi kushtuka kakuta kajikaba kooni kajitia na dole kwny nonino.stori za zamani bana
 
Ndoto zinaumuhimu gani katika maisha ya mwanadamu?kisayansi tutasema chakula ni muhimu kutupa nguvu na kulinda mwili.haja ni kuondoa uchafu mwilini.jasho ni kupima mwili.nilitegemea kupumzisha akili lakini si kweli maana mara nyingine unaamka umechoka sana.
 
umenikumbusha movie moja inaitwa PASSENGERS watu walikufa kwenye ajari ya ndege lakini walikuwa wanaamin bado wapo hai kumbe wanaota...au hile series ya LOST mwishoni watakapogundua kumbe wamekufa...
 
Kwani kuna mtu kasema ana uhakika hayupo ndotoni
 
Kama ni maswali ya kiimani sina jibu ila kisayansi naweza tofautisha uhalisia na ndotoni kwa kuangalia SAA yani kwenye ndoto hata uwe sebleni na sikuzote huwa kuna saa, ndotoni hiyo saa hutoiona ubongo hauwezi kutengeneza tic-toc ya duniani.
 
Kama ni maswali ya kiimani sina jibu ila kisayansi naweza tofautisha uhalisia na ndotoni kwa kuangalia SAA yani kwenye ndoto hata uwe sebleni na sikuzote huwa kuna saa, ndotoni hiyo saa hutoiona ubongo hauwezi kutengeneza tic-toc ya duniani.
Mimi nilishaamka asubuhi ndotoni na nilipoangalia saa nikawahi shule bila kuoga kutokana na nilikuwa nimeshachelewa nusu saa nzima.
Ile natoka nyumbani speed kuwahi shule ndio nikakurupuka kitandani huku kukiwa bado hakujakucha vizuri.
 
Mimi nilishaamka asubuhi ndotoni na nilipoangalia saa nikawahi shule bila kuoga kutokana na nilikuwa nimeshachelewa nusu saa nzima.
Ile natoka nyumbani speed kuwahi shule ndio nikakurupuka kitandani huku kukiwa bado hakujakucha vizuri.
Ungeiangalia SAA mara ya pili ndo nilivyomaanisha kusema ubongo hauwezi kutengeneza tic-toc ya duniani. mfano angalia saa iseme 1723... icheki tena iandike 1023... hiyo ndoto sasa. Ila uhalisia cheki saa yako iseme 1725... rudia tena iseme 1725/6 hiyo reality.
 
Binadamu mara nyingi akikutana na jambo( kitu) la ajabu la kushangaza au kuhuzunisha sana kuna swali huwa anajiuliza hata mimi binafsi nimejikuta kama mara mbili hvi ikinitokea.

Swali: Hivi naota au?(akijiuliza yani nipo ndotoni au ndio real happen).
maswali naomba mnijibu:

1: Unawezaje kutofautisha kati ya ndoto na uhalisia?
zingatia: jambo unalofanya/linalotokea ndotoni halina tofauti na linalotokea katika hali halisi.
mfano: unaweza ota unapigwa na unalia na feelings zile zile utazipata ukiwa endapo utanapigwa live(sio ndotoni)

2: Una uhakika gani kuwa sasa hauoti ndoto hapo ulipo unaposoma hii thread?
maana hata ndotoni unaweza ukawa JF unasoma na kuandika thread.

3: Una uhakika gani kama jibu lako hilo ulilotoa ni sahihi na sio umetoa ndotoni sasa.
Ukitaka ufurahie maisha siku zote katika maisha yako, uwe unachukulia kila jambo ni ndoto ambayo unaweza kuiota utakavyo wewe. Stress zote za maisha zitakwisha na utakuwa huru.

Nakutakia undeleze hii ndoto yako njema unayoota unasoma thread yangu kumbe kiuhalisia hausomi.
UKIOTA UNATAKA KWENDA CHOONI USIKUBALI,KWANI HUO NI MTEGO!
 
Kuna jamaa aliota kaokota furushi la hela kuliinua kumbe kuna tundu chini akaamua kuliziba na kidole cha kati asubuhi kushtuka kakuta kajikaba kooni kajitia na dole kwny nonino.stori za zamani bana
hahahahahaaaa[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
lakini je ukiwa unaota huwa unajijua kuwa umelala? au hadi ndoto ikatize(iishe) ndio unakurupuka et kumbe ni ndoto
Kama utakua mfuatiliaji mzuri wa ndoto zako, unaweza ukaota halafu ukahisi kua upo usingizini, na inaweza kutoka kabla ya kuamka kutoka usingizini. Mimi imeashawahi nitokea baada ya kuona mambo yanayotokea kwenye ndoto hayapo duniani
 
Back
Top Bottom