Truths
JF-Expert Member
- Mar 26, 2017
- 1,494
- 1,504
Mgombea Urais wa Kenya anaeungwa mkono na ngome ya NASA, Raila Odinga amepinga matokeo yanayoendelea kutangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi ya nchi hiyo (IEBC).
Odinga ameeleza kuwa kutokana na kutokuwepo fomu hizo ni vigumu kubaini matokeo yanayotangazwa na IEBC yanatoka wapi.
“Mfumo umeachwa na sasa ni mitambo ndio inayopiga kura. IEBC wamesema kwamba hakuna chama chochote kilichopinga matokeo. Lakini vyama vitapingaje matokeo bila kujua asili yake? Ni fomu namba 34A pekee inazoonesha chanzo cha matokeo,” amesema Odinga.
“Kwa hivyo, tunakataa matokeo yote yaliyotangazwa kwa sasa na kuitaka tume ya IEBC itoe fomu 34A za kila kituo kabla ya matokeo zaidi kutangazwa,” aliongeza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Odinga ameeleza kuwa kutokana na kutokuwepo fomu hizo ni vigumu kubaini matokeo yanayotangazwa na IEBC yanatoka wapi.
“Mfumo umeachwa na sasa ni mitambo ndio inayopiga kura. IEBC wamesema kwamba hakuna chama chochote kilichopinga matokeo. Lakini vyama vitapingaje matokeo bila kujua asili yake? Ni fomu namba 34A pekee inazoonesha chanzo cha matokeo,” amesema Odinga.
“Kwa hivyo, tunakataa matokeo yote yaliyotangazwa kwa sasa na kuitaka tume ya IEBC itoe fomu 34A za kila kituo kabla ya matokeo zaidi kutangazwa,” aliongeza.
Sent using Jamii Forums mobile app