Unadhani ni kwanini siku hizi ni nadra sana kunyimana mapenzi isipokuwa ndani ya ndoa tu ndio unaweza kunyimwa live unajiona?

Unadhani ni kwanini siku hizi ni nadra sana kunyimana mapenzi isipokuwa ndani ya ndoa tu ndio unaweza kunyimwa live unajiona?

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Nini hasa kimeingilia hapo katikati kwenye mapenzi, kwamba nje ya ndoa hakuna tena uchoyo wala kunyimana suala la mapenzi, unapewa tu kirahisi hata na mwenye ndoa, ila cha kushangaza ndani ya ndoa hata mwenye ndoa mwenyewe ananyimwa na anaweza kupewa kwa mbinde sana au kwa ratiba na masharti makali.

Lakin nje ya ndoa mtu anatoa au anapewa mapenzi bila hiyana na bila ugumu wala mbambamba yoyote na wengine kwenye mapenzi wanapeana hadi vitu vya ziada.

Nini sababu ya yote haya kutokea kwenye mapenzi ndugu zangu wadau, ukiachilia mbali pesa na magari🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Hata ndani ya ndoa unapewa labda tu mke wako hakupendi au Huwa anaipeleka Kwa mhuni Fulani inakandamiza vizuri zaidi Yako ndiyo maana Huwa anakunyima
Lakini malalamiko ni mengi mno wanandoa kunyimana gentleman,

Lakini hao hao nje ya ndoa wanatoa vizuri tu, na kinafiki mbele ya jamii wanajionyesha kupendana sana 🐒
 
Kukinaiana kunakosababishwa na kukosekana kwa upendo au kuchepuka
Lakini si mliahidiana kuvumiliana katika shida na raha, Lakini pia kua waaminifu? Kwanini mnachepuka tena?

mbona sherehe ya ndoa yenu ilikua ya gharama sana, kweli hamkua mnapendana kweli?🐒
 
Tatizo kabla ya ndoa watu twaficha zile inner behavior....
kwahiyo kumbe kuna udanyanyifu makubwa sana kabla ya ndoa right?

kumbe mnaficha ukweli ambao ndio baadae ndio unawapa mzigo mzito wa kubeba wanokutana nao wababa na wamama wa watu ndani ya ndoa zao? Maskini, dah!

Inasikitisha sana, inafedhehesha mno 🐒
 
Swali zuri sana, tena linahitaji hoja za msingi.

Unajua kuna vitu vinatokea tunavichukulia kirahisi sana au pengine ndio tunaona ni maendeleo ya technolojia nianze hivi:

Miaka ya nyuma jamii ilitunza maadili sana na jambo moja lililotiwa mkazo ni tendo la ndoa baada ya ndoa, na mabinti walikuwa makini na wakali sana juu ya hili, hiyo ilimlazimu mwanaume kuoa ili apate tendo la ndoa ambalo kwake ni hitaji muhimu sana, na hii ilifanya taasisi ya ndoa na familia kwa ujumla kupata heshima kubwa na kuwa jambo la muhimu katika maisha ya mwanadamu.

Siku hizi kuna vita kubwa sana juu ya hii taasisi ya ndoa pamoja na familia, ndio maana kuna makundi haramu yameibuka, Kataa ndoa, superwoman, haya makundi yako kimkakati kabisa kuhakikisha hii taasisi kuonekana haina maana, upatikanaji wa tendo lenyewe nje ya ndoa umerahisishwa mno, kiasi kwamba hakuna umuhimu wa kuoa ndio upate tendo la ndoa, Lakini pia ibilisi ameachilia roho ya uharibifu na mafarakano ndani ya hizo ndoa ili kusiwe na maelewano, lengo ikiwa ni kuisambaratisha hiyo ndoa na umuhimu wa ndoa yenyewe usionekane, ndio maana utashangaa binti amestrugle apate ndoa halafu anapata anaanza kumnyima mwenzake, mara anaanza mawasiliano na maex, mwisho wa siku ndoa inajifia kibudu.

Nini kifanyike?

1. Lazima turudi kwenye msingi wa kuelewa ndoa ni nini? na ni nini kusudio la kuwepo kwa ndoa ili tuwe na familia zilizo salama kwa vizazi vijavyo.

2. Lazima ijulikane kuwa ndoa ni mpango wa Mungu sio matakwa ya mwanadamu, na huo mpango unapigwa vita vikali lengo ni kuondoa upendo unaojengwa kupitia hizo ndoa, kama likiachwa kama lilivyo itafika kipindi binti kulala na baba yake, au kijana kumlala mama yake litaonekana jambo la kawaida.

3. Lazima hatua za madhubuti zichukuliwe, hasa kwa watumishi wa Mungu, ambao nao wamejikita katika kuhubiri pesa, mafanikio tu huku wakiacha mambo ya msingi, ukigeuka huku sadaka, ukigeuka huku sadaka. Yale mambo ya msingi yameachwa.

4. Jamii lazima ikubali kuwa kwenye hili tumeteleza, wametengenezwa wanawake ambao ni material oriented, jinsia ya mwanaume inapigwa vita maeneo yote, angalia hata maofisini utakuta idadi ya wanawake ni kubwa kuliko wanaume, halafu wanaume vijana hawana ajira, huyu mwanamke majukumu ya ndoa hawezi kuyabeba, tunaona mifano huku kwa maandiko mbali mbali mwanamke akipata nafasi ya cheo na kipato ndoa hakuna hapo, ila nje atagawa kipapa bila shida kwa kisingizio cha haniridhishi.
 
kwahiyo kumbe kuna udanyanyifu makubwa sana kabla ya ndoa right?

kumbe mnaficha ukweli ambao ndio baadae ndio unawapa mzigo mzito wa kubeba wanokutana nao wababa wa watu ndani ya ndoa zao? Maskini, dah!

Inasikitisha sana, inafedhehesha mno 🐒
Mbona umesema wababa tu..unamaanisha wanawake hawadanganywi...acha ubaguzi...
Ndiyo maana nimesema wenza tunaficha tabia...umebase kwa wababa😳
 
Mbona umesema wababa tu..unamaanisha wanawake hawadanganywi...acha ubaguzi...
Ndiyo maana nimesema wenza tunaficha tabia...umebase kwa wababa😳
hapana,
nazungumzia wachumba, michepuko na wanandoa wote kwa ujumla,

huenda ni typing error tu ambayo nadhani imerekebishwa 🐒
 
Ni kiherehere chako ukaoa malaya

KATAA NDOA
Mtu akitaka utelezi anapata anytime aoe nini sasa?
 
Back
Top Bottom