Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Maharage chandeKama umeanza kuhoji kuhusu hizi kampuni za watu upo kwenye njia sahihi, hongera sana🤝👍💪
kuna kanisa huwa napenda kwenda wakat wa kusifu kuna ke zinakatika hatar😆Mara nyingi najiuliza swali juu ya faida ya kusali ni ipi na kwanini watu wanatumia muda mwingi kusali na sio kutafuta mali.
Je, kusali ni lazima iwe katika nyumba za ibada au unaweza kusalia sehemu yoyote na kama unaweza kusalia sehemu yoyote kuna faida gani kukutana katika nyumba za ibada.
Je, unapaswa uombewe au ujiombee?
Msafara wa mamba kenge hawakosagi sawakuna kanisa huwa napenda kwenda wakat wa kusifu kuna ke zinakatika hatar😆
Naam hatukuletwa Ili tutafute mali ila pia hatukuletwa Ili tufanye ibadaMkuu, uliletwa duniani ili utafute mali?
Mbona ukiondoka duniani huondoki nazo?
😂🤣😅😆😁Msafara wa mamba kenge hawakosagi sawa
Yanarudishaje nyuma kwa mfanoMkuu unajua moja ya vitu vinanirudisha nyuma juu ya hizi imani za kidini ni matabaka kwann kuna matabaka sijui Muslim mara Christian kule Budas,Paganism nani yupo sahihi???
Kwan kanisa unaondoka nalo?Mkuu, uliletwa duniani ili utafute mali?
Mbona ukiondoka duniani huondoki nazo?
Huwezi ona umuhimu wake Hadi siku utakapoona umuhimu wa oxygenIfike mahali hizi nyumba za ibada zibomolewe tu.. Maana sijaona umuhimu wake.. ☹️☹️.
Kama kweli dini ina umuhimu, Leta huo umuhimu hapa,umuhimu utauona zitakapo bomolewa
• Kwa hiyo kabla ya hiyo biashara ya wazungu na waarabu haijaletwa na majahazi hapa Africa, Oxygen haikuwepo??Huwezi ona umuhimu wake Hadi siku utakapoona umuhimu wa oxygen
kiimani mkuu .Yanarudishaje nyuma kwa mfano
Umewahi kata oxygen• Kwa hiyo kabla ya hiyo biashara ya wazungu na waarabu haijaletwa na majahazi hapa Africa, Oxygen haikuwepo??
Oxygen ni kitu asilia mkuu, Kwa hiyo haiwezi kukata...Umewahi kata oxygen
Uko mzima hauitaji daktariOxygen ni kitu asilia mkuu, Kwa hiyo haiwezi kukata...
Oxygen na dini ni vitu viwili tofauti kabisa...
Hakuna maisha baada ya kifo. Huo ni uongo wa dini za kuletwa. Je waliowaua mababu zetu na kuwachukua utumwa hawakusoma hayo maandiko uliyoyaweka. Jiongeze Kwa kutumia fikira zako na siyo kufuata mkumbo wa story za kaleKuna maisha ya mwilini mkuu na kuna maisha ya rohoni, kila maisha yana maandalizi yake, wewe ukijikita kutafuta mali usiende kanisani kumtafuta Yesu utafanikiwa duniani lakini kwenye maisha yako baada ya kifo chako utaishia jehannum ya moto na hapo ndipo utakapokuwa milele hiyo ni kanuni!! Tunasali au kwenda kuabudu kanisani kwa sababu ni agizo la Mungu ( waebrania 10:25"
wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Ukifahamu kuwa baada ya kifo chako kuna maisha baada ya haya huwezi kuuliza hayo maswali yako mpendwa
Mara nyingi wanadamu tunaangalia sana vinavyoonekana, ndo unakuta unasoma sana muda wote kusoma, kuwa busy sana, kutafuta mali usiku na mchana, unasahau kuwa kuna maisha baada ya kifo chako,
2 korintho 4:18"
tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
Mtu ambaye anahoji kwanini watu wanasali au kwenda makanisani huyo mtu ni kipofu na ni mpumbavu maana hajui kitu pamoja na mali zake na usomi wake lakini hana kitu ni mtupu!
Zaburi 14:1"
Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema.
Ni vizuri kusoma sana, kutafuta mali, fedha nk lakini kumbuka ipo siku utasimama mbele za Mùngu kutoa hesabu ya mema au mabaya
Mhubiri 11:9"
Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.
Ni vizuri ukajifunza kwa hawa watu walikuwa na kila kitu Leo hawapo unapaswa kujiuliza Leo hii wapo wapi
1: magufuli
2:mengi
3: membe
4: mrema
5: kubaki
6: moi
7: mkapa
8: Queen Elizabeth
Nk
Luka 12:16
Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;
Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.
Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.
Akawaambia wanafunzi wake, Kwa sababu hiyo nawaambia, Msisumbukie maisha yenu, mtakula nini; wala miili yenu, mtavaa nini.
Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege! Na yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?
Basi, ikiwa hamwezi hata neno lililo dogo, kwa nini kujisumbua kwa ajili ya yale mengine?
Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,
kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.
Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.
hivyo mpendwa usione kuwa wanaosali ni wajinga hao wanajua wanachokifanya, ipo siku utayakumbuka maneno yangu lazima ujue kuwa kuna ziwa la moto na kuna ufalme wa Mungu uchaguzi wa sehemu utakapoenda ni wewe mwenyewe, unapaswa kujua kuwa pasipokumwamini YESU kristo hakuna kwenda mbinguni, usidanganywe na dini yako, Yesu ndiye njia pekee na uzima pasipo huyo Yesu utaishia motoni mpendwa
Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.
Ufunuo 21:8
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.
Matendo Ya Mitume 4:12
Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
Yohana 14:6
Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo.
Isaya 35:8
Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.
Mhubiri 12:14
katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.
Warumi 2:16
Siku njema
• Kumbe unazungumzia UZIMA??Uko mzima hauitaji daktari
Yakikukuta ndo utaelewa• Kumbe unazungumzia UZIMA??
• Kwa hiyo uzima na dini wapi na wapi?
• Mbona wengi wapo hospital kwa miaka kadhaa wakiomba kupata unafuu kupitia dini zao wanazo ziamini, pia masheikh na wachungaji wanaenda kuwaombea lakini hakuna kilicho badalika..!!! Au dini inachagua yupi awe mzima, na yupi awe mahututi, au yupi alale na njaa na yupi alale ameshiba????