Unafanya nini ili usifilisike na usipotee kwenye ramani? Nafsi yangu inangia huzuni na hofu nikikutana na waliofilisika

Unafanya nini ili usifilisike na usipotee kwenye ramani? Nafsi yangu inangia huzuni na hofu nikikutana na waliofilisika

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Moja ya jambo linalotisha kwenye maisha ni kufilisika, ulikuwa na mali zako kidogo zinakusogeza na zinakupatia chochote, una watu wamekuzunguka unawapa kazi na unawapatia chochote japo kidogo, then inatokea hiyo hali inakata, humiliki Cha maana, mission za mjini zimekata, huonekani aisee unapauka, mahitaji ya msingi unayaona ni anasa, tabia za majungu zinakurudia, kutoka kutafuta muda saizi unawaza upotezaje muda, hali hii Huwa inatisha na kuchanganya sana.

Ninapokuwa mjini na ninapokutana na kaka zangu na watu tofauti wa hapa kwetu hasa wale walionekana miaka Ile wamebotoa au wapo njiani kutoboa halafu unakuta wamechoka, uzee huu hapa, ngozi zao hazishawishi, wamechagua kufanya kazi ndogo ndogo, mara bodaboda nk, wanakuomba pesa.

Niseme ukweli mimi binafsi nafsi yangu inangia na huzuni na hofu, huwa najiuliza wao walikosea wapi na mimi nina nini cha maana ambacho kinaweza kuwa ni ngao na uhakika.

Nikiwa kanisani nimejikuta sala yangu ni kuomba, "Mwenyezi MUNGU mwingi wa upendo, azibariki siku zangu, aniondolee siku za mateso, aniepushe na mikosi, laana na mabalaa," kwani Sioni what so special nilichonacho, je wewe unafanyaje ili usikae nje ya mstari wa maisha?
 
Ilo ombi lako la kuondolewa mateso nisiwe muongo dunia ni uwanja wa fujo tegemea lolote

Zaidi na zaidi ni neema tu

Zaidi na zaidi muishi Yesu kristo kwa roho na kweli

Sijui unaelewa kumuishi kristo?

Halafu chapa kazi ukiwa na amani mafanikio ni matokeo sio jibu.
 
Haka katopic kazuri, kama ulikuwa ndani ya akili yangu. Kwanza na mimi kama wewe, namtanguliza MUNGU mbele kwa maombi na sala. Japo umri wangu umekwenda, nakwenda na kasi ya vijana katika utafutaji. Huwa naziboresha biashara zangu ili ziendane na wakati. Kupotea kwenye GAME ni huzuni na ni aibu inayopelekea kupoteza maisha.
 
Kufilisika bwana kusikie tu Ila sio Jambo dogo linauma linaumiza sana.

Back in days uncle wangu alikuwa vizuri sana badaye akaja akafilisika sina namna naweza kueleza maisha magumu anayopitia Ila namuonea huruma kiasi kuna muda sipendi hata kukutana naye maana huwa naishia kwenda chooni kulia sana na badaye natoka na kuaga tu.
 
Kufilisika ni dhana kama ilivyo utajiri, kimsingi binadamu ana mahitaji makuu matatu, kula, kulala na ku-do

Hayo mengine yote ni mahitaji ya kutengenezwa (artificial needs) or imposed needs, kwa mfano huwezi kufa kwasababu unaishi bila simu au data, ila ukikosa simu au data utaona kama mambo hayako sawa.

Jifunze kukubali matokeo, rahisisha mahitaji yako, pambana upate kwanza mahitaji ya lazima mengine yatakuja kama ziada.

Ukishindwa kunielewa, wewe ni kiazi mbatata
 
Kuepuka tu starehe zisizokuwa za lazima eg; pombe, wanawake kutaka kumiliki gari za bei ghali etc na kuwekeza zaidi kwenye vitu kama nyumba, viwanja na mashamba.

Actually hakuna mwenye uwezo wa kusema anathibiti kipato chake kwa 100% kwamba aamke nacho kesho na keshokutwa but ukifuatilia wengi walioyumba na hawakuchoka sana ni wale waliowekeza kwenye nilivyovitaja hapo juu.

Pia wakati mwengine tamaa ya kutaka kufanya kila biashara huwa inaleta balaa la kufilisika so ukiweza stick na kile ulichokizoea lakini kiboreshe uzidi kudumu mchezoni.
 
Kufilisika ni jambo baya Sana Ila nidhamu na hekima huweza kumfanya MTU aendelee kukaa katika ramani.

Ikiwa utaanza kujizuia na starehe ambazo hazina umuhimu kama Pombe kupita kiasi, uzinzi, uvutaji Sana n.k hii inaweza kukubakisha juu.

Ila kubwa kuliko yote Mungu na kutoa sehemu ya mali zako kwa wahitaji.

MAISHA ya anasa nimeona yana negative impact Sana na ndio njia ya uhakika ya kuukaribisha umasikini.

Mimi sio tajiri wala sio masikini Ila natamani Sana Mafanikio makubwa mbinu ambazo nazitumia ni

Kuwa na hekima -kuheshimu nilichonancho hata Kama ni kidogo

Kutoa hasa kwa wazazi na watoto.

Kukaa mbali na uzinzi ,pombe ,sigara ,bangi ,kubeti, night out.

Kujiwekea malengo kwa kuyaandika

FAIDA
Kupitia hizi mbinu nimejikuta hichi hichi kidogo nachopata kinatosha kunipatia kula , kulipa kodi ,kusaidia wazazi na kuweka Akiba huku jamaa zangu wakishindwa .

Mwisho nidhamu, uaminifu Mungu ndo ngao yangu.

Kufilisika kukosa hadi 100 ni jambo baya sana hasa ukiwa upo mzima wa Afya . hauna magonjwa .
 
Kufirisika bwana kusikie tu Ila sio Jambo dogo linauma linaumiza sana

Back in days uncle wangu alikuwa vizuri sana badaye akaja akafirisika Sina namna naweza kueleza maisha magumu anayopitia Ila namuonea huruma kiasi Kuna muda sipendi hata kukutana naye maana uwa naishia kwenda chooni kulia sana na badaye natoka nakuaga tu
Unamsaidiaje sasa, kutokana na maelezo yako inaelekea wewe sasa hivi mambo ni supa.
 
Kuwekeza pesa kwa mtu mtaalamu eidha mtaalamu huyo ni wewe au mwingine.

Nidhamu na kusimamia kile ambacho unadhani ukikifanya kitakutoa kwenye ramani basi usifanye.

Kutaka mafanikio ya haraka ni jambo baya sana,mtu kila biashara anayosikia inalipa anaingia mwishowe anaanguka..

Kudumu na biashara inayokupa faida ya asilimia kadhaa ni bora kiko kujaribu kila biashara.
 
Kuwekeza pesa kwa mtu mtaalamu eidha mtaalamu huyo ni wewe au mwingine.

Nidhamu na kusimamia kile ambacho unadhani ukikifanya kitakutoa kwenye ramani basi usifanye.

Kutaka mafanikio ya haraka ni jambo baya sana,mtu kila biashara anayosikia inalipa anaingia mwishowe anaanguka..

Kudumu na biashara inayokupa faida ya asilimia kadhaa ni bora kiko kujaribu kila biashara.
Shida ukidumu kwenye biashara moja, vipi kesho hio biashara ikaingiliwa na wababe zaidi yako?

Ndio mana watu wanajaribu kuwa na biashara japo 3 + mashamba ya matunda na miti na korosho + nyumba za kupangisha na UTT juu
 
Katopic kazuri, ukianguka tuliza akili utaamka.

Miaka fulani nilikuwa silali hotel ambayo ni chini ya elf 50 kwenda juu.

Baadae nikauguliwa na mama mzazi nikatumia hela zote na hakupona akafariki, Kuna siku nakumbuka maeneo ya Tandika nimeingia Guest chumba elf 15 mm nina elf 10, nilimuomba mhudumu akasema nakupa ila jitahid hata kukopa kesho umalozie elf 5. Niliingia room nililia kiume kitandani nikajisemea kwamba sasa nimejua kabla hujafa hujayaona ya Dunia.

Nikaendelea kujivuta vuta nikawa saww tena baada ya miaka kama miwili.

Ila pia utawala wa huyu Hangaya haubariki biashara zangu kwa sasa, profit margin inashake balaa
 
Katopic kazuri, ukianguka tuliza akili utaamka.

Miaka fulani nilikuwa silali hotel ambayo ni chini ya elf 50 kwenda juu.

Baadae nikauguliwa na mama mzazi nikatumia hela zote na hakupona akafariki, Kuna siku nakumbuka maeneo ya Tandika nimeingia Guest chumba elf 15 mm nina elf 10, nilimuomba mhudumu akasema nakupa ila jitahid hata kukopa kesho umalozie elf 5. Niliingia room nililia kiume kitandani nikajisemea kwamba sasa nimejua kabla hujafa hujayaona ya Dunia.

Nikaendelea kujivuta vuta nikawa saww tena baada ya miaka kama miwili.

Ila pia utawala wa huyu Hangaya haubariki biashara zangu kwa sasa, profit margin inashake balaa
Hilo la afya linaniogopesha sana,
Nawazaga siku nikate bima ya NHIF, na niwakatie wategemezi wangu,

Licha wanazinguaga ila ni wanaokoaga kimtindo
 
Back
Top Bottom