Unafanyaje kuishi maisha ya kigeto geto bila kupika?

Unafanyaje kuishi maisha ya kigeto geto bila kupika?

Jumanne Mwita

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2014
Posts
530
Reaction score
1,446
Kwa miaka 4 sasa na mwezi mmoja nimeishi bila kujipikia nikila kwa migahawa nfanya hivi kwa maisha haya ya kutojipikia kwa sababu mimi siyo mtu wa kukaa sehemu moja nikatulia hii ni sababu ya mazingira yangu ya utafutaji nakaa sehemu kwa muda mfupi baadae naenda eneo jingine nikiridishe kwenye mada leo bhana nimeona naumia kwa siku natumia chai 1,000 hadi 1500 inategemea nimepita wapi siku hiyo maana sina kasumba ya kula sehemu moja nikazoeleka.

Mfano: Chakula cha mchana natumia 2,000 hadi 2500 nikijilipua sana labda 3000 siku zingine.

Sasa leo nikaenda nilikozoea wanasema chakula nilichokuwa nakula 2,000 leo wamepandisha ni elf 2500 hivyo hivyo hadi chai mpaka vyakula vingine!

Imebidi niulize hivi nyie kwanini imekuwa ghafla sana na hizi bei za vyakula wanasema vitu vimepanda bei na wanasema hata bajeti imekuja na mabadiliko ya vitu kupanda hivyo tuzoee!

Nimeishiwa nguvu ya kuendelea kusema chochote imebidi nilipie tu nijipange kununua vitu na mimi nianze kujipikilisha, na kupika ndio mvivu wa kwanza katika sekta hii ya kijipikia hasa kuosha vyombo ni mtihani kwangu siyo kwamba najiona hapana, sijui wengine wasema wanaona "aibu" hapana kitu nachokuwa nazembea nipale nimekula nimeshiba nikimaliza vyombo vinaniangalia tena yaani kikifikia hatua hii ndio naona kupika kazi bwana.

Kwa wenzangu ambao mnaishi maisha ya kigeto geto bila kupika, mna ushauri gani juu ya hili? Je, kuna njia rahisi za kupika ambazo hazihitaji jitihada kubwa au muda mwingi? Na je, ni vipi mnavyopambana na gharama hizi za juu za chakula nazungumzia wewe kwa wale ambao hampiki huku mkiendelea kuishi bila kujipikia? Naomba uzoefu na mawazo yenu.

Karibuni kwa mjadala!
 
IMG-20240620-WA0922.jpg
 
Mishe zikikubana huna namna ila kama si mtu wa kudamka na kuchelewa kurudi Basi mgahawani Kula mchana tu.

Suala la vyombo osha unapotaka kupika na vinapokua vichafu hakikisha havina majimaji sababu huleta harufu ya uozo baada ya siku kadhaa bila kuoshwa.
 
Enzi zangu za ubachela nilikuwa najipikia mwenyewe, hao mama ntilie wanawekaga amira kwenye ugal
Na mwambie asidhani kupika mwenyewe ndio gharama zitapungua... Tena gharama inaweza kuwa juu zaidi..

Uzuri wa kupika mwenyewe ni ile kupata chakula chenye ladha nzuri na salama bila uchakachuzi... Ila gharama iko pale palee
 
Mkuu nakushauri tu jitahidi uwe unapika hata kama ni kujipikilisha baadae utazoe utakuwa mkali wa jiko,tabia ya kula kwenye migahawa siyo afya sana wengine usafi hawazingatii utakuja kuumwa yaliwahi kunikuta.
Nunua mahitaji kwa jumla huepusha pia gharama inaonekana hata usafi unaitaga wale wamama wa kitaa.
 
Na mwambie asidhani kupika mwenyewe ndio gharama zitapungua... Tena gharama inaweza kuwa juu zaidi..

Uzuri wa kupika mwenyewe ni ile kupata chakula chenye ladha nzuri na salama bila uchakachuzi... Ila gharama iko pale palee
gharama inategemeana na aina ya chakula unachokula, ugal hauna gharama issue ije kwenye mboga
 
Asante sana
Mishe zikikubana huna namna ila kama si mtu wa kudamka na kuchelewa kurudi Basi mgahawani Kula mchana tu.

Suala la vyombo osha unapotaka kupika na vinapokua vichafu hakikisha havina majimaji sababu huleta harufu ya uozo baada ya siku kadhaa bila kuoshwa.
Nimechukua hii
 
Na mwambie asidhani kupika mwenyewe ndio gharama zitapungua... Tena gharama inaweza kuwa juu zaidi..

Uzuri wa kupika mwenyewe ni ile kupata chakula chenye ladha nzuri na salama bila uchakachuzi... Ila gharama iko pale palee
Mboga haikamatiki kwa sasa uwe na kuanzia elf 4 hapo ndio unapata nyama au mboga yakueleweka maisha yamebadilika sana sasa hivi
 
Mkuu nakushauri tu jitahidi uwe unapika hata kama ni kujipikilisha baadae utazoe utakuwa mkali wa jiko,tabia ya kula kwenye migahawa siyo afya sana wengine usafi hawazingatii utakuja kuumwa yaliwahi kunikuta.
Nunua mahitaji kwa jumla huepusha pia gharama inaonekana hata usafi unaitaga wale wamama wa kitaa.
Shida ni gharama siyo rafiki ila kwa uoande wa usafi kuna hotel au migahawa wasafi
 
Nikipata wakati nipo nyumbani najipikia mwenyewe ila kama ninkazi basi huwa nakula sehem nzuri chakula kizuri basi, kupika mwenyewe inapendeza japo ghaarama zinazidi ila ni vuema
 
Nunua vitu digitali ambavyo vinaweza kukurahisishia kupika.

Mfano kuna ma-pressure cooker ya auto ambayo unaweza hadi kuya set muda gani yaanze kupika

Badala ya kuset kiwango cha moto kuivisha wali kwenye gesi ukiwa na pressure cooker maana yake hiyo kazi inafanyika automatiki.

Swala la kuosha vyombo zipo dish washer ambazo ni portable zinauzwa around 150K
 
Nunua vitu digitali ambavyo vinaweza kukurahisishia kupika.

Mfano kuna ma-pressure cooker ya auto ambayo unaweza hadi kuya set muda gani yaanze kupika

Badala ya kuset kiwango cha moto kuivisha wali kwenye gesi ukiwa na pressure cooker maana yake hiyo kazi inafanyika automatiki.

Swala la kuosha vyombo zipo dish washer ambazo ni portable zinauzwa around 150K
Kwa tunaojitafuta hivi vitu tunavisikia tu sema ikitokea nikapata pesa nitafanya hivyo 🤝🤝
 
Back
Top Bottom