Amesema mzee mmoja maarufu kuwa kupigwa risasi na kupata ulemavu sio jambo zuri,lakini sio kigezo cha mtu kuingia ulingoni ili apate urais.
Matokeo yake kila unapokuwa unasimama majukwaani ni kuvunja sheria za nchi na kuambulia aibu.
Hivi kwa nchi kama Tanzania ambayo inajiendesha kwa misingi ya katiba na sheria mgombea urais unasimama jukwaani na kudai serikali ilikupiga risasi na rafiki yako Ansbert Ngurumo alinusurika kuuwawa na kukimbilia Finland. Huoni kama huu ni uchochezi?
Wewe ni mwanasheria Nguli unafahamu namna human rights violations zikifanyika hatua gani ziaweza kuchukukiwa. Kwa nini hizo hatua hujazifuata na kubaki kuongea maneno ya uchochezi?
Leo bila ya aibu unasema unazo habari za kusikia ambazo huna uhakika nazo, unasema maafisa wa polisi huko Songwe na Geita wamehamishwa vituo vya kazi, kisa tu waliwadhibiti wanachama na wafuasi wa CCM waliotaka kukufanyia vurugu. Mbona hizo habari hatujazisikia toka kwa msemaji wa jeshi la polisi? Hii ni aibu kwa mwanasheria nguli kutoa taarifa za kusikia tu.
Hii yote ya kuwa unaropoka mambo ambayo hayaendani na sera wala kampeni za Chadema ni sababu uligombea urais ukijua huwezi kushinda,bali ulitaka upatiwe nafasi kuonesha ghadhabu zako baada ya kuwa umeshambuliwa na watu wabaya. Lakini hii sio solution maana matamko yako yana lengo la kuhatarisha amani ya taifa letu.
Na wewe is ugombea uonyeshe hasira zako..
Poleni...mataga....