Unakumbuka mwaka 1994 Wazanzibar walivyokasirika Rais wa Zanzibar kuondolewa kuwa Makamu wa Rais wa Muungano?

Unakumbuka mwaka 1994 Wazanzibar walivyokasirika Rais wa Zanzibar kuondolewa kuwa Makamu wa Rais wa Muungano?

Kama nimemuelewa vizuri mwandishi wa uzi hu (kama ni kweli huo ndio msimamo wa Nyerere ) ni hivi; yule rais wa Zanzibar, Watanganyika hatukushiriki kumchagua (though still is too theoretical cause rais wa Zanzibar anachaguliwa na Dodoma) kachaguliwa na Wapemba na Waunguja, huyu makamo wa rais wa muungano anachaguliwa pamoja na rais aliyeko madarakani; Ingawa tuombe Mungu apishilie mbali mawazo ya wachangiaji wengi, Mungu atuepushe kabisa.
Tuombe Mungu yanayosemwa yatimie.
 
Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
 
Ni mwaka 1994. Mwaka 1985 kulikuwa na CCM tu.

Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
 
MdogoWenu said:
Nyerere akasema hilo lilikuwa ni tatizo kwa sababu Rais wa Zanzibar anachaguliwa na wazanzibar tu.

MrFroasty

Hoja za kitoto hizo, makamu wa Rais anapigiwa kura na nchi nzima kushika nafasi ya umakamo. Tena na gharama zingekuwa nafuu, kwa vile kusingekuwa na makamo wa Rais, badala yake nafasi hii ingekuwa nearly empty kwa vile Rais wa tz akiwa hai makamu anashughulika kazi zake za Urais Zanzibar.
sijaona km ni Hoja za kitoto Rais Hussein Ally Hassana Mwinyi kachaguliwa na Wazanzibar tu, wakati Makamu Samia Suluh Hassan kachaguliwa na Wanzanzibar na Watanzania wote.
Kwa hiyo la kutokea iwe ugonjwa au kujiuzulu Makamu (Mama Samia Suluhu ndiye atahusika wakati mh Hussein Mwinyi atabaki Zanzibar na vikao vya Mwaziri atahudhuria chini ya Mama Suluhu Hassan)
km ulivyosema hapo juu kuwa Makamu akiwa Rais wa Zanzibar atafanya kazi zake zaidi hii mikanganyiko ilimkuta Mh John Malecela akiwa Makamu kwa Rais All Hassan Mwinyi alibanwa mpaka ikatoke G55, na ile ya Mrema kuwa Naibu waziri Mkuu ndio maana wakaona waitoe kwenye mfumo wa vyama vingi na bado ni kero
MY TAKE kwa sasa ni lazima Rais atoke Bara panga pangua
 
Nyerere na Bomani waliku right kabisa. Katiba ya tanzania haijawahi kuwa wazi kuhusu kupokeana madaraka wakati Rais akifa; kwa mfano wakati Karume alipofariki, Makamu wa wa pili wa Rais wakati huo alikuwa Kawawa, lakini yeye hakuwa promoted kuwa makamu wa kwanza wa Rais, badala yake aliletwa Jumbe ambaye alikuwa waziri wa nchi kwenye ofisi ya Makamu wa kwanza Rais wakati huo.

Halafu Nyerere alipostaafu, Mwinyi hakuwa automatic choice bali kulikuwa kampeini kubwa sana ya "huyu ni mwenzetu" iliyofanywa na Nyerere ili kumkubali Mwinyi kama mrithi wa Nyerere, kulikuwa na uwezekano mkubwa sana wa watu wengine kuiwania nafasi hiyo.

Bado kulikuwa na woga wa "Treason Act 1351" kuhusu kuongelea uwezekano wa rais kufia madarakani.
Kwaiyo mkuu unataka kusema kwamba uwezekano wa mama yetu kuwa raisi ni mdogo sana?
 
Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
1985-1990 wakati MWINYI ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, marehemu Sh. Idrisa Abdul Wakil alikuwa Rais wa Zanzibar na wakati huo huo ni makamo wa pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huku Jaji Joseph Sinde Warioba alikuwa ni Waziri Mkuu na Makamo wa Kwanza wa Rais. Nadhani ni hivyo hivyo kwa 1990-1995 MWINYI Rais wa Jamhuri , Salmin Amour Juma Rais wa Zanzibar na Makamo wa Pili huku John Samwel Malechela Waziri Mkuu wa Jamhuri na Makamo wa Kwanza wa Rais ingawa Malechela hakumaliza kipindi chake kutokana na sokomoko la G55 lililopelekea nafasi yake kuchukuliwa na Cleopa David Msuya.
 
Wazanzibar wamezoea kudekezwa, hayo mabadiliko yalikuwa sahihi sababu rais wa wazanzibar huchaguliwa na wazanzibar sisi bara hatuwezi kuongozwa na mtu tusiyemchagua
 
Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
Kwakua Mwinyi alikua Mzanzibar na rais wa muungano, waziri mkuu wa wakati huo ndio akawa makamu wa kwanza wa rais, na si mwingine ni mzee Joseph Sinde Warioba
 
Back
Top Bottom