Unakumbuka mwaka 1994 Wazanzibar walivyokasirika Rais wa Zanzibar kuondolewa kuwa Makamu wa Rais wa Muungano?

Tuombe Mungu yanayosemwa yatimie.
 
Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
 
Ni mwaka 1994. Mwaka 1985 kulikuwa na CCM tu.

Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
 
MdogoWenu said:
Nyerere akasema hilo lilikuwa ni tatizo kwa sababu Rais wa Zanzibar anachaguliwa na wazanzibar tu.
sijaona km ni Hoja za kitoto Rais Hussein Ally Hassana Mwinyi kachaguliwa na Wazanzibar tu, wakati Makamu Samia Suluh Hassan kachaguliwa na Wanzanzibar na Watanzania wote.
Kwa hiyo la kutokea iwe ugonjwa au kujiuzulu Makamu (Mama Samia Suluhu ndiye atahusika wakati mh Hussein Mwinyi atabaki Zanzibar na vikao vya Mwaziri atahudhuria chini ya Mama Suluhu Hassan)
km ulivyosema hapo juu kuwa Makamu akiwa Rais wa Zanzibar atafanya kazi zake zaidi hii mikanganyiko ilimkuta Mh John Malecela akiwa Makamu kwa Rais All Hassan Mwinyi alibanwa mpaka ikatoke G55, na ile ya Mrema kuwa Naibu waziri Mkuu ndio maana wakaona waitoe kwenye mfumo wa vyama vingi na bado ni kero
MY TAKE kwa sasa ni lazima Rais atoke Bara panga pangua
 
Kwaiyo mkuu unataka kusema kwamba uwezekano wa mama yetu kuwa raisi ni mdogo sana?
 
Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
1985-1990 wakati MWINYI ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, marehemu Sh. Idrisa Abdul Wakil alikuwa Rais wa Zanzibar na wakati huo huo ni makamo wa pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na huku Jaji Joseph Sinde Warioba alikuwa ni Waziri Mkuu na Makamo wa Kwanza wa Rais. Nadhani ni hivyo hivyo kwa 1990-1995 MWINYI Rais wa Jamhuri , Salmin Amour Juma Rais wa Zanzibar na Makamo wa Pili huku John Samwel Malechela Waziri Mkuu wa Jamhuri na Makamo wa Kwanza wa Rais ingawa Malechela hakumaliza kipindi chake kutokana na sokomoko la G55 lililopelekea nafasi yake kuchukuliwa na Cleopa David Msuya.
 
Wazanzibar wamezoea kudekezwa, hayo mabadiliko yalikuwa sahihi sababu rais wa wazanzibar huchaguliwa na wazanzibar sisi bara hatuwezi kuongozwa na mtu tusiyemchagua
 
Hivi ilikuwa 1994 au 1985? Kwa ninavyokumbuka Ali Hassan Mwinyi ndo alikuwa wa mwisho kuwa rais wa Zanzibar ambaye ni makamu wa rais wa jamhuri.

I stand to be corrected
Kwakua Mwinyi alikua Mzanzibar na rais wa muungano, waziri mkuu wa wakati huo ndio akawa makamu wa kwanza wa rais, na si mwingine ni mzee Joseph Sinde Warioba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…