Unakumbuka nini katika enzi za gazeti la Sani?

Unakumbuka nini katika enzi za gazeti la Sani?

Kutili plaza? Kutili kabati ya mbeho? Enzi hizo ukitaka kuoa mchagga? Tv ilikuwa ni chuo cha polisi na chuo cha ushirika tu. Umesahau YMCA. Balozi wa Tanzania nchini Kuwait alikuwa form four chopra sec (mwanza sec school).
Kweli mkuu. Nakumbuka 90 kombe la dunia nchini italia. Tulikuwa tukiangalia pale chuo cha ushirika, tv yao ilikuwa ni zile zisizo na rangi.(black n white) ccp pia tulikuwa tunaangalia. Wao walikuwa na coloured tv.
 
Kweli mkuu. Nakumbuka 90 kombe la dunia nchini italia. Tulikuwa tukiangalia pale chuo cha ushirika, tv yao ilikuwa ni zile zisizo na rangi.(black n white) ccp pia tulikuwa tunaangalia. Wao walikuwa na coloured tv.
Lakini ikifika usiku pale CCP unasikia "wanafunzi wa moshi sec muondoke sasa" . Hivi tulipokuwa miaka kabla ya 1980 tunanunua maziwa ya Arusha na mikate tunakuita Dukani kwa Muro bado yupo?
 
Kijarida cha wahenga enzi hizo

images.jpeg
 
Umenikumbusha mbali sana, miaka ya 80 kuelekea 90 ndipo nilianza kulifuatilia sana hili jarida lililokuwa linatoka kila mwezi na hadithi za kusisimua sana akina Chepe, Kipepe, Sokomoko, Ndumilkuwili, Lodilofa, Madenge, Kifimbo Cheza, Dokta Pimbi, nakumbuka pia kulikuwa na kurasa kadhaa za vichekesho ilikuwa inaitwa cheka unenepe.

Ikifuatiwa na hadithi za wimbi la Kitintale unakutana na akina Obi, Linda, Zumo, Bosi Mayuyu liyekuwa anaishi kisiwani aliyekuwa anafanya biashara za madawa ya kulevya na magenge yake ya unyang'anyi, Ole aliyekuwa mtesaji wa huyo mdosi na mabaunsa wenzake. Riwaya za akina Eddy Genzel Mauaji ya Hayawani, Kizaizai na nyinginezo zilizokuwemo kwenye hilo jarida.
 
Miaka ile, katuni hizi zilikuwa maarufu kiasi kwamba baadhi yetu tulipewa majina ya katuni zile kama majina ya utani.

R.i.P Mtunzi wa katuni hizi marehemu
Philip Ndunguru, aliyefariki mwaka 1986 akiwa na umri wa miaka 24. Katuni zake ziliendelea kuleta tabasamu miaka kadhaa iliyofuata. Kwa kumkumbuka mtunzi huyu, na kufurahia kazi zake.
 
Mzee Bawiji nae alikuwa anatunga hadithi nzuri, nakumbuka mwaka 87 tupo zahanati tumempeleka mgonjwa kutibiwa, kuna jamaa sijui alitoka kijiji gani alikuwa na gazeti la sani, dah tulitamani wagonjwa wasibiwe haraka ili tuendelee kuburudika na sani
 
Back
Top Bottom