Unakumbuka Simba ya Azim Dewj na Yanga ya Abass Gulamali?

Unakumbuka Simba ya Azim Dewj na Yanga ya Abass Gulamali?

Sodoku

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2016
Posts
1,271
Reaction score
2,903
Kiukweli miaka hiyo kulikuwa na ushindani mkubwa sana kati ya Matajiri hawa wawil na Simba na Yanga. Sijui ni nini kiliwatoa kwenye Ule Ushindani.

Mechi zao zilikuwa zikitabiria na watabiri akina Majura na mtabiri mwingine nmemsahau katika magazeti ya Mfanyakazi.

Nawakumbuka wachezaji kama akina abedi mziba,fred minziro,hussein marsha, george masatu, mtwa kihwelu,itutu kigi,nonda shaban,said mwamba kizota,fumo felician,danny mhoja,twaha hamidu,zamoyoni na method mogella,salum kabunda ninja, athuman china,idd paz n.k

Miaka hiyo wachezaji walikuwa wanajituma sana. Wanacheza kwa nguvu na akili. Mpira ulikuwa unasakatwa hasa.

Huku azim dewj na abbas gulamali wakitambiana ile mbaya.
 
Enzi zakina sanif lazaro 'tingisha' salum kabunda 'ninja'. Watangazaji wa mpira redio Tanzania walikuwa wanajua Sana kunogesha matangazo. Unasikia 'wao bila sisi moja'
 
Hizo enzi zitaisha.. huko mbele tutakua tunasimulia simba na yanga za sasa.. tutakua tunawataja kina KICHUYA, TAMBWE, AJIB, na wengine wote wanaotamba sasa.
 
Enzi zakina Yusuf Lazaro 'tingisha' salum kabunda 'ninja'. Watangazaji wa mpira redio Tanzania walikuwa wanajua Sana kunogesha matangazo. Unasikia 'wao bila sisi moja'
Sanifu lazaro "tingisha "game moja inapulizwa filimbi jukwaani rajabu rashidi "double r"anaushika mpira akidhani ni faulo inatengwa penalty anapiga almarhumu khamis gaga inagonga mwamba kisha yanga wanakimbiza na kufunga goli tuliokuwa uwanjani tunapata picha tofauti na wanao sikiliza yanga 3 simba 1.
 
Sanifu lazaro "tingisha "game moja inapulizwa filimbi jukwaani rajabu rashidi "double r"anaushika mpira akidhani ni faulo inatengwa penalty anapiga almarhumu khamis gaga inagonga mwamba kisha yanga wanakimbiza na kufunga goli tuliokuwa uwanjani tunapata picha tofauti na wanao sikiliza yanga 3 simba 1.
Yap.ni sanifu Lazaro nasiyo yusuf Lazaro. kaka
 
Kiukweli miaka hiyo kulikuwa na ushindani mkubwa sana kati ya Matajiri hawa wawil na Simba na Yanga. Sijui ni nini kiliwatoa kwenye Ule Ushindani.

Mechi zao zilikuwa zikitabiria na watabiri akina Majura na mtabiri mwingine nmemsahau katika magazeti ya Mfanyakazi.

Nawakumbuka wachezaji kama akina abedi mziba,fred minziro,hussein marsha, george masatu, mtwa kihwelu,itutu kigi,nonda shaban,said mwamba kizota,fumo felician,danny mhoja,twaha hamidu,zamoyoni na method mogella,salum kabunda ninja, athuman china,idd paz n.k

Miaka hiyo wachezaji walikuwa wanajituma sana. Wanacheza kwa nguvu na akili. Mpira ulikuwa unasakatwa hasa.

Huku azim dewj na abbas gulamali wakitambiana ile mbaya.
Mimi ni miongoni mwa walioshuhudia mpira ukichezwa kipindi hicho. Ni kweli mpira ulikuwa unapigwa, lakini hakuna tofauti sana na unavyopigwa sasa, ndio maana hata timu yetu ya taifa haikuweza kufanya lolote la maana. Tofauti tu ni kwamba wakati ule watu waliokuwa na vipaji vya asili walikuwa wengi ukilinganisha na sasa. Kinachosababisha tuone mpira ulikuwa mwingi kuliko sasa ni ile asili ya binadamu kupenda vya zamani kuliko vya sasa. Hata kina Gerd Muller, Paul Gaza, John Barnes, Abedi Pele, George Weah na wengine wa nyakati zilizopita wanasifiwa kuliko kina Robert Lewandowski, Yaya Toure.
 
Kweli ulikuwa wakati mzuri. Illa kuhusu timu ya taifa wakati wao walifanya nini cha maana??? Mwaka pekee tangia uhuru ni mwaka 1980 kama sikosei tulishiriki mataifa huru ya afrika Nigeria tukafungwa mechi zote. Kuhusu timu ya Taifa na vilabu tuna rekodi mbili tatu nzuri kidogo lakini hazina mafanikio. Na hayajajirudia tena ila baada ya muda tena ka rekodi ina maana katika soka tuna tatizo tena sugu. Illa naungana nanyi vipaji tunavyo tatizo nini?
 
unakumbusha miaka ya akina hamis thobias gaga gagarino... ha ha ha.. watangazaji akina mbonde, mikidadi,charles hilary..walikuwa watangazaji wazuri sana miaka hiyo.

Sanifu lazaro "tingisha "game moja inapulizwa filimbi jukwaani rajabu rashidi "double r"anaushika mpira akidhani ni faulo inatengwa penalty anapiga almarhumu khamis gaga inagonga mwamba kisha yanga wanakimbiza na kufunga goli tuliokuwa uwanjani tunapata picha tofauti na wanao sikiliza yanga 3 simba 1.
 
unakumbusha miaka ya akina hamis thobias gaga gagarino... ha ha ha.. watangazaji akina mbonde, mikidadi,charles hilary..walikuwa watangazaji wazuri sana miaka hiyo.

Athuman Maulid, Zamoyoyoni Mogella, Bakari Tutu, Peter Tino, Amasha, Juma Mkambi, Minziro
 
Hapa chechei hawakuelewi kabisa unazungumzia nini. Simba walikuwa kipa idd pazi na mackienz ramadhan yanga wana Steven Nemes alikuwa anapenda kuvaa bukta


Athuman Maulid, Zamoyoyoni Mogella, Bakari Tutu, Peter Tino, Amasha, Juma Mkambi, Minziro
ich
 
kipindi hicho ilikua raha sana,na hicho ndio kipindi mtu akipigwa harudi home wiki nzima,siku hizi ujingaujinga tu mtu anafungwa anang'oa viti.
 
Enzi hizo kwenye matawi tunabet atakaeshinda atapikiwa na mtani wake siku 3 asubuhi,mchana,jioni raha sana
 
unakumbusha miaka ya akina hamis thobias gaga gagarino... ha ha ha.. watangazaji akina mbonde, mikidadi,charles hilary..walikuwa watangazaji wazuri sana miaka hiyo.
Yaah Charles hilary kuna game anatangaza taifa yanga na majimaji kisha morogoro simba na reli basi kulikuwa na kitu ile na huko morogoro halafu anaendelea kutangaza taifa anakwenda abeid mziba kwake yusuph bana aah inakuwa faulo pale Peter muhina anamchezea ndivyo sivyo Abubakary salum sureboy na huko morogoro simba na huko morogoro simba ana bao mbili hapo mashabiki wa msimbazi wakalipuka kwa furaha kisha akamalizia na reli ya morogoro wanaongoza kwa bao nne anakwenda octovean mrope kwake samli ayubu aah Abdul ntila anajichanganya na mpira unatoka nje.
 
Hapa chechei hawakuelewi kabisa unazungumzia nini. Simba walikuwa kipa idd pazi na mackienz ramadhan yanga wana Steven Nemes alikuwa anapenda kuvaa bukta



ich
Hiyo simba ya kina Morgan golini alikuwa moses mkandawile maulidi "big men "mbavu ya kushoto kulia alikuwa mussa "super "kiwellu na yanga hiyo golini alikuwa Joseph fungo kina bana edger fongo jeneral hapo kati sio mchezo.
 
unakumbusha miaka ya akina hamis thobias gaga gagarino... ha ha ha.. watangazaji akina mbonde, mikidadi,charles hilary..walikuwa watangazaji wazuri sana miaka hiyo.
Omary Jongo, Ahamedi Jongo, Charles Hilary, Dominic Chilambo acha kabisa wakati huo
 
Marehemu selestini sikinde mbunga, Deo Njohole, makumbi Juma, sanifu Lazaro Tingisha, zamoyoni Mogera, Abeid Mziba, Abubakari Salumu (sure boy)


Hawa kina Lunyamila walikuja baada ya kina Sanifu kuondoka
 
Back
Top Bottom