Unalazimishwa na mkeo?

Unalazimishwa na mkeo?

hata wanawake wengine, my wife na joto la dar hili anaoga maji ya moto na kuoga asubuhi hakuna ugomvi ila jioni sasa daily lazima tugombane hataki kuoga, sometimes tukitoka kwenye sherehe na ma perfume anataka kulala hivyo hivyo, kwa hiyo mwenzenu nna kibarua cha kumwekea maji ya moto daily my wife wangu bafuni, nikichelewa tu akipanda kitandani tu kumuamsha ni kazi

maji moto na joto lote hilo??? ukitaka iwe rahisi kwake kuoga jioni make it fun, muoge nyote pamoja she will start looking forward!!
 
mijimwanaume mingine bwana haipendi kuoga kabsa...grrrrrrrrrrrrrr.kuna mmoja alikuwa anapenda gym jamani akitoka kule jasho utafikiri kanyeshewa! mmm bado mtu hataki kuoga yaani inatia kichefu chefu!
 
Niko na wadada/wamama walioolewa hapa ofisini. Wameanzisha thread ya mashambulizi hapa wanasema Wanaume wengi ni kero kwelikweli!.

Eti hawaendi kuoga mpaka waambiwe, au kulazimishwa au kubembelezwa mara mbili tatu au nne, na mkewe ndo atanyanyuka KWENDA BAFUNI.

Eti wasipofanya hivyo mibaba mingi tu inapanda kitandani na kuanza kukuroma bila kuoga!


sio wote jamani, kuna wanaume wasafi aisee, yaani mie wangu ananipa challenge kubwa hawezi kulala bila kuoga hata kama amerudi nyumbani saa nane usiku...halafu anajispray kamanukato na kuchana nywele ati he's got to be smart in his dreams... sio wote and i love him sooo much for that!

sasa kasheshe uoge mapema kama saa moja jioni halafu bado upo jikoni unahangaika na vitunguuu yaani bafuni bado utarudi!!!! duh!!! saa ingine inaudhi lakini ndivo hivyo...waridi na miiba yake!!
 
What i can say nimejifunza mengi sana kwenye huu mjadala mzito. Thanks alot wachangiaji hasa kwa wale walioko kwenye ndoa waliotoa personal experience pia wale waliotoa shared experience. Imekuwa mada ya mafundisho na mabadiliko sana. Big Up JF
 
What i can say nimejifunza mengi sana kwenye huu mjadala mzito. Thanks alot wachangiaji hasa kwa wale walioko kwenye ndoa waliotoa personal experience pia wale waliotoa shared experience. Imekuwa mada ya mafundisho na mabadiliko sana. Big Up JF

Thanks alot SIPO.

Even myself imenipa changamoto za kutosha, na nmejifunza vitu vipya lukuki.

Ongea na watu upate viatu!
 
Mimi hii mada hata siitaki maana nikianza kuongea sitamaliza. Kuoga, uchafu asilia, bado hajatupa tupa nguo zake hovyo yaani kweli ni kazi hebu endeleeni kwanza
 
...ama kupenda ni upofu, si ajabu tabia hizo zilikuwepo tangu enzi za mapenzi motomoto... iweje sasa imekuwa kero?
BTW, kisu kinakata kote kote...uchafu ni tabia ya mtu, haijalishi ni mwanamke au mwanaume, 'asili ni kovu la kudumu!'
..Mbu hilo nalo neno. Kama mwanamke alikubali kuolewa na bwana ambaye kuoga lazima akumbushwe that means aliyajua haya tangu enzi za uchumba/urafiki wao alitakiwa kumrekebisha tangu huko otherwise angemwaga tu. Sasa leo mko kwenye ndoa ndio unagundua kuwa jamaa kuoga shurti kwa filimbi??? Majungu tu hayo!!!
 
Mimi hii mada hata siitaki maana nikianza kuongea sitamaliza. Kuoga, uchafu asilia, bado hajatupa tupa nguo zake hovyo yaani kweli ni kazi hebu endeleeni kwanza
Mamii naona una uchungu sana, usijali wapo watu wa aina hii, yani inaudhi we acha tu! unawezaje kulala bila kuoga lakini? kwanza mimi hata nkisema nijaribu itatokea hata usiku wa manane nakurupuka kuoga, maana hata usingizi siwezi pata ntaishia tu kugeuka kitandani, hata baada ya kudo lazima nioge ndo niwe confortable kulala peacefully.
 
Mamii naona una uchungu sana, usijali wapo watu wa aina hii, yani inaudhi we acha tu! unawezaje kulala bila kuoga lakini? kwanza mimi hata nkisema nijaribu itatokea hata usiku wa manane nakurupuka kuoga, maana hata usingizi siwezi pata ntaishia tu kugeuka kitandani, hata baada ya kudo lazima nioge ndo niwe confortable kulala peacefully.

Kuna Mchungaji alipata kutufundisha kuwa mtu asijaribu kwenda kuoga baada ya ku'do...ni kosa la jinai!

Tulipomuuliza kwanini akasema kuwa "Nani aliyesema yale makitu ni uchafu...?...Nani aliyepata kudhurika nayo?...Ungekuwa uchafu usingekuwa na baraka ya uumbaji", Tukaachwa hoi!

Akasema mkimaliza kunanihino na kama mmeshachoka, basi mnakumbatiana na kulala zenu fofofo, hadi aidha asubuhi, au mida ya majogoo, mtakaposalimiana tena..lol!
 
Back
Top Bottom