Unamkumbuka Mussa Simba aka Black Moses: Huyu alikuwa bingwa wa Disco miaka hiyo

Unamkumbuka Mussa Simba aka Black Moses: Huyu alikuwa bingwa wa Disco miaka hiyo

Unga mbaya sana huyu dogo alifikia hatua mbaya sana ,ukiacha kitu vibaya usawa wake anapita nacho.

Mpaka akawa anafungiwa ndani .
 
  • Thanks
Reactions: T11


Pia kulikuwa na MARSHA YAHAYA HUSEIN....jamaa alikuwa wanachuana sana BREAK DANCE....walikuwa wakikutana ni balaa,,,waliteleza zile style za akina BUGA LUU na SHABA DUU ,,,zamani ndy watu walikuwa wanacheza DANCE,,, siku hizi MWANAMKE,,MWANAUME wote wanacheza style MOJA ,,,kutingisha MABEGA kama MTU Kashikwa na DEGEDEGE..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Enzi hizo alikuwepo Dada mmoja akiitwa Fatuma Zahoro au (DiscoDancer) R.I.P...huyu alijiua kwa kunywa vidonge vingi vya Cloroquine kisa kazuiwa kwenda kwenye Disco na wazazi wake..
Yote kwa yote Mussa Simba (R.I.P.) siku za mwisho za uhai wake alikuwa teja tena pwaku pwaku hatari..

Ndugu zake walikuwa wakimfungia ndani kwao Mwanza mitaa ya Rufiji..

Sina hakika kama alijiua lakini tatizo kubwa lilikuwa ni uteja..alikuwa amesha hathirika vibaya sana kwa madawa.
Huyo Fatuma siyo yule dada aliyekuwa mwanafunzi wa sekondari fulani mwaka 1985 au 1986 na akashinda shindano moja kubwa la kucheza break dance? Kama ndiyo yeye nakumbuka baba yake alikuwa ni baharia na baada ya kupata ushindi wa kucheza break dance na kusakamwa shuleni na mtaani kwao aliamua kujiua na kuacha simanzi kubwa. Miaka hiyo kwa Dar nilizoea kuwaona akina Black Moses na wengineo waliokwishatajwa. Pia nikienda zangu Mwanza nilikuwa nikiwaona wacheza break dance kama Bob Sado (si riziki?), Matongo (kama nimepatia jina), vijana fulani watoto wa mzee Jumbe (mmoja wa wazee maarufu pale Mwanza kwa miaka hiyo) akiishi mtaa wa aidha Rufiji au Uhuru. Enzi hizo ma Dj maarufu kwa Mwanza walikuwa ni Dj Yusuph na Bush Doctor ambao wote kwa sasa ni marehemu.
 
Anaitwa MUSSA SIMBA aka BLACK MOSES Huyu alikuwa bingwa wa Disco miaka hiyo... Enzi za muziki wa Disco Uko juu sana jamaa alikuwa maarufu sana kwa aina ya uchezaji mpaka disco linapotea kwenye ramani jamaa alikuwa Hana mpinzani

Jamaa baada ya kuwa maarufu kupitiliza aliamua kujiingiza kwenye madawa ya kulevya miaka hiyo na baada ya madawa kumtawala sana ulitokea ugomvi Kati yake na baba yake mzazi mzee SIMBA nyumbani kwao magomeni mapipa na MUSSA SIMBA aka BLACK MOSES aliamua kujiua

R. I. P KING BLACK MOSES View attachment 851604

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah, kujiua enzi hizo ilikuwa kama fashion...issue ndogo tu vijana walikuwa wanameza chloroquine
 
Anaitwa MUSSA SIMBA aka BLACK MOSES Huyu alikuwa bingwa wa Disco miaka hiyo... Enzi za muziki wa Disco Uko juu sana jamaa alikuwa maarufu sana kwa aina ya uchezaji mpaka disco linapotea kwenye ramani jamaa alikuwa Hana mpinzani

Jamaa baada ya kuwa maarufu kupitiliza aliamua kujiingiza kwenye madawa ya kulevya miaka hiyo na baada ya madawa kumtawala sana ulitokea ugomvi Kati yake na baba yake mzazi mzee SIMBA nyumbani kwao magomeni mapipa na MUSSA SIMBA aka BLACK MOSES aliamua kujiua

R. I. P KING BLACK MOSES View attachment 851604

Sent using Jamii Forums mobile app
Walikuwa na uwezo kujinyonga kama nyoka. Hata mazoezi yao hayakuwa ya kitoto. Leo huwapati wa jinsi hiyo.
 
Huyo jamaa alikuwa maarufu Sana enzi hizo tukiwa wadogo.
Alifahamika Tanzania kote kupitia show zake na kuandikwa kwenye magazeti na kutajwa Radio Tanzania back then.
 
Back
Top Bottom