Unamnunulia mchepuko kitenge sare na mke wako, wanaume kuna mnalolitafuta

Unamnunulia mchepuko kitenge sare na mke wako, wanaume kuna mnalolitafuta

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Mke uliyemtolea mahari na kukabidhiwa na wazazi wake. Amekuzalia watoto, anafua na kupiga pasi nguo zako, anapika chakula watoto wako na wewe hamlali na njaa leo unampa mateso haya.

Leo amekwenda saloon kusuka yeboyebo ingawa hupendi ajichanganye ili asisikie ufuska wako. Amekutana na ule mchepuko wako wa bank uluimletea kitenge ulipoenda Ivory Coast. Kumbe ulinunua sare na mke wako.

Mchepuko anamjua mke wako na anamdharau kwakua ni mama wa nyumbani. Bank ajira yake aliipata kwakua branch manager ni mshirika wako wa biashara ulihakikisha anapita usaili.

Kuna kitu unakitafuta na utakipata hivi karibuni.
 
Zamani Mungu alikuwa anachelewa kujibu, ila Siku hizi kwa kuwa upuuzi ni mwingi wala hachelewi akichelewa sana ni mwaka mmoja tu.Siku zote malipo ni hapa hapa duniani, huwezi mdhalau Mke anaekuthamini na kukuheshimu ukabaki salama.
 
Sky Eclat,
Inasikitisha saana kama ni kweli. Ukiwa mother house ni kazi kweli na hasa kama ulishafanya kazi tena nafasi nzuri ila ikabidi ukae nyumbani kwa ajili ya hama hama.
 
Amekuzalia watoto

yule nurse aliyezaa watoto kwa uwezo wa roho mtakahela bila kukutana na Michael Jackson, akamkabidhi watoto, akasepa milele, ndio "amemzalia watoto" Michael Jackson

mke mliyekutana kwa hiari kunako samani tambarare hajakuzalia watoto, amezaa watoto!
 
kwa hiyo shida apa ni mchepuko kufanya kazi bank au kuvaa kitenge sare na mchepuko?
 
Sky Eclat, Wewe muombe Mungu akujibie kisasi kama umeshafahamu.

Malipo haizidi miezi tisa.
Kama hakupata mimba ikawagombanisha, atapata hata kipigo chochote kitakachowafarakanisha.

Ila wakati unaomba hayo nawe uwe msafi wa maneno na matendo kwa mumewe.
Maana isiwe kule ndiko anapopata pumziko la moyo baada ya kelele zako na masimango yako.
 
Nakuhakikishia sky eclat ukiwa na mimi ntakununulia vya tofauti kabisa na vya tanzania hii!!kazi kwako sasa!!!!
 
Back
Top Bottom