Unamzungumzia Diamond, humjui AY?

Unamzungumzia Diamond, humjui AY?

Nimeamua Kuandika Thread Hii Kutokana Na Magazeti Mengi Ya Udaku Kumsifia Diamond Kuwa Ndio Msanii Mwenye Mafanikio Hapa Tz Mfano Ktk Gazeti La Kiu La Tarehe 31dec 2012 Wanamwita Diamond Kuwa Ndo Msanii Expensive Hivi Diamond Ana Ue-xpensive Gani Kuliko AY

wasoma magazeti ya udaku naamini wao pia ni wadaku!!!

ikiwemo wewe mleta uzi!! uzi wako umekaa kidaku daku tu! toa reference za vitu unavyoviongelea. how comes unaleta uzi ambao uko robo?

umeuliza kitu cha msingi sana, hrbu jaribu kutofautisha kati ya economic growth na economic development.

hapo ndipo utajua kati ya diamond na Ay nani ni nani!
 
AY anapenda kujiendeleza nlikutana nae last time Learn IT chuo anaingia kipindi.

Diamond sina uhakika aliishia darasa la ngapi?
 
Successful Musicians from Tanzania, excluding gospel singers:

Targets: Both Richness and Popularity,

1. Lady Jay Dee
2. AY
3. Prof Jay
4. Juma Nature
5. Diamond
6. Mzee Yusuph
7. FA
8. Fid Q
9. Madee/Temba/Chege/Tunda (These guys fall in the same position)
10. Afande Sele

Factors:

1. Time since they started and all difficulties they faced/encountered.
2. Shows per year they attended, inside and outside of Tanzania.
3. Other properties they own, which obviously came from Music such as house/apartments, businesses, means of transports etc.

Source: Me
 
Nilianza kumfuatilia AY tangu alipokuwa CBM Crew; miaka kadhaa iliyopita very certain wakati Diamond akiwa bado Primary School! Hakuna shaka kwamba kwa kipindi chote hicho AY hajasahaulika lakini sikumbuki kipindi chochote over the entire time AY alipata kuwa Top....kwenye soka ya Tanzania, AY ni kama Kagera Sugar; imeendelea kusumbua kwa kipindi chote lakini haijapata kuwa Top! Katika hili la kuwa Top, AY hajawahi kufikia hata status ya Mr. Blue!! Diamond, kama kumbukumbu zangu zipo sahihi, tangu aingieze nyimbo "Nenda Kamwambie", bado hajawahi kushuka....ameendelea kuwa Top over the entire period of time; for almost Three Years Now!!

Tukirudi kwenye mafanikio, sijui tunataka kuzungumzia mafanikio ya nini....ikiwa ni ya kimuziki, angalau kwa kumlinganiasha na AY, Diamond mwacheni aitwe Diamond....the guy he's far better than AY. Hawa wote ni watu wa kujifagilia, AY huyu huyu alitutangazia kwamba kwamba ametengeneza Video kwa TZS 32 million! Lakini ukiangalia kwa makini ile video, mtu unaweza kujiuliza 32 million zilitumika tumika vipi; kwani ukiiangalia video yenyewe yenyewe, hakuna scenes zozote ambazo zinaonekana ni expensive scenes.....sana sana kuna scene za watu kula pombe!! Angalau Diamond, akisema alitumia USD 30,000 kwenye video yake, ukiiangalia video husika, inaleta sense!

Kubwa ambalo naona AY kamzidi Diamond kwa mbali ni ku-settle! AY ame-settle probably than any other Bongo Flavor Artist in TZ! Ni mtu ambae anaziona opportunities na kuzifanyia kazi. Kama mafanikio ya kimuziki ya Diamond angekuwa ndo aliyonayo AY, basi leo hii AY angekuwa kitu kingine kwa mafanikio ya kiuchumi!
 
Acheni Uchawi, ALMASI ipo kwenye CHATI. Dogo kwa sasa yuko juu, kwani mziki wake hua unapendwa na watu wengi tofauti na huyo AY. Mziki wake ni watu wa aina flani tu.
 
Back
Top Bottom