Unapataje ujasiri wa kumuacha mke mwenye mtoto mdogo unayempenda?

Unapataje ujasiri wa kumuacha mke mwenye mtoto mdogo unayempenda?

WhoWeBe

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2022
Posts
2,299
Reaction score
4,282
Mke mmeshashindwana kwa kila namna; kiuchumi hamuendi, kisocial hamuendi, kinidhamu n.k hamuendi, yaani ni tabu tupu na umeshafanya maamuzi kichwani ya kumrudisha kwao mara baada ya mavuno maana si kwa kutoelewana huku. Yaani katika wiki maelewano yanaweza kuwa ya siku mbili tu, siku zingine zote hata kusalimiana ni shida.

Katikati ya uelekeo wa kutekeleza maamuzi hayo, kuna kikwazo kikubwa; mtoto, binti mmoja mchangmfu anayeelekea kutimiza miaka mitatu hivi karibuni. Mtoto anakupenda nawe unampenda mno, kila muda wa kurudi kazini unapofika katoto kanasimama barazani kukulaki, yamekuwa mazoea ya kupendeza mno yanayokutia simanzi hata yakikosekana siku mbili tu. Vikelele vya kitoto ndani hadi anapolala nayo ni burudani nyingine.

Ukifikiria kuikosa burudani hii, pozi inagoma kuwekeka. Katika upendo huu wa kina, linakuja suala la kufikiria (imagination) ni namna gani binti huyu ataishi huko aendako kwa baba mlezi (lazima atapatikana tu).

Mbinu gani wadau ya kutumia kuneutralize hisia hasi hii?

Karibuni!
 
Na hapo ndipo kiburi cha huyo unayetaka kumuacha kilipo..anajua unampenda sana mwanae.ki ufupi baba hawezi kumpenda mtoto zaidi ya mamaye,bali baba anamjali mtoto kuliko mamaye.so wewe angalia ni wapi furaha yako ilipo.
 
Na hapo ndipo kiburi cha huyo unayetaka kumuacha kilipo..anajua unampenda sana mwanae.ki ufupi baba hawezi kumpenda mtoto zaidi ya mamaye,bali baba anamjali mtoto kuliko mamaye.so wewe angalia ni wapi furaha yako ilipo.
 
Mimi huchagua kuishi, nao tu!!! maana mtoto atateseka sana, mwanaume unapaswa kusimamia familia yako ibaki salama,

Mama yake ata kama hamuendi lakin tafuta namna ya kumvumilia kwa ajili ya mtoto

Tetea damu yako kwa gharama yyte, dunia harsh sana kumuacha akue mbali na Wewe mkuu
 
Wanaume wa Afrika ndio maana mnakufa kwa msongo wa mawazo kwa kutojitambua.Kuweni free kama wazungu,unashindwaje kupima faida na hasara.

Cha msingi hakikisha unamjali mtoto hata baada ya kumuacha mama yake,utakufa na msongo na utamuacha hapo huyo mtoto.
 
mimi huchagua kuishi, nao tu!!! maana mtoto atateseka sana, mwanaume unapaswa kusimamia familia yako ibaki salama,

mama yake ata kama hamuendi lakin tafuta namna ya kumvumilia kwa ajili ya mtoto

tetea damu yako kwa gharama yyte, dunia harsh sana kumuacha akue mbali na Wewe mkuu
Yani uvumilie kuishi na MTU kwa ajili ya mtoto hizo akili au matope?
Kwani mkipeana distance mtoto hatahudumiwa?
 
Ndio Maisha hayo ndugu yangu,ila hata hvyo usilalamike sana maana ulivyoshauriwa usikimbilie hayo mambo mpaka ukue,hukuskia,ulishauriwa pia utumie ndomu ukaziba maskio,Sasa ni mwendo wa kutulia dawa iingie.
 
Back
Top Bottom