Unapomkosea mwanamke, Usimwambie Unampenda, badala yake muombe Msamaha!

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Ikiwa Leo ni siku ya wanawake duniani ningependa nichangie mawili matatu.

Wanawake kama walivyo wanaume nao huwa Wana hisia za furaha na huzuni pia, kutofautiana katika ndoa ni Jambo la kawaida Sana kwasababu binadamu hatuja kamilika hivyo huwa tuna fanya makosa ima Kwa kujua au kutokujua au Kwa makusudi na wakati mwingine huwa hatukusudii Ila ndio udhaifu wetu kama wanadamu.

Sasa endapo imetokea tumewaudhi wenza wetu basi Busara inataka tuwaombe msamaha kwani huo ndio ubinadamu wetu, na Kwa kawaida binadamu yoyote angependa aombwe msamaha mara pale anapokosewa.

Sasa Kwa bahati mbaya Sana Sisi wanaume huwa tuna mtazamo mbaya kuhusu kuomba msamaha Kwa wenza wetu, tuna mtazamo kwamba kumwomba msamaha mwanamke ni kujishusha na kupunguza thamani yetu kitu ambacho si kweli, ukweli ni kwamba kuomba msamaha ni kuonyesha ukomavu na kuwajibika Kwa Yale makosa tuliofanya na hii itazidi kupandisha heshima yako mbele ya mwenza wako na kuonyesha kwamba unajali hisia zake na hivyo kumfanya akusamehe na akupende zaidi.

Hakuna Jambo linalo udhi kama umemkosea mwenza wako halafu badala ya Kumuomba msamaha badala yake unamwambia unampenda! Swali linakuja kichwani kama unanipenda kwanini umenikosea au kwanini umeniudhi?

Kwahiyo namna pekee ya kuweka mambo Sawa ni kuonyesha kwamba unajuta Kwa kile ulichofanya na unaomba radhi Kwa Hilo Kwa Nia Safi kabisa,na kufanya hivyo wala hakuta ondoa uanaume wako au kushusha thamani yako Bali utabakia kuwa mwanaume kamili na hadhi yako siku zote itabakia pale pale.

Kumbuka mapenzi ya kweli huwa haya angalii hadhi ya mtu Bali huangalia zaidi Utu WA mtu.

Katika siku hii ya wanawake duniani ningependa kutoa much love humu Jf Kwa Kalpana,Depal,To yeye, mademo iselle,baby zu Kwa kuwataja wachache.

Ni hayo Tu!
 
Usinuombe mwanamke msamaha especially Kama umechepuka. Wewe kataa halafu kataa tu, mwisho ataamini kwamba hujatoka nje. My friend, ukiomba msamaha inamaana umekubali kosa. Ni kosa kubwa Sana kukubali kosa ulilokosa mbele ya mwanamke.
Thank me later.
 
Usinuombe mwanamke msamaha especially Kama umechepuka. Wewe kataa halafu kataa tu, mwisho ataamini kwamba hujatoka nje. My friend, ukiomba msamaha inamaana umekubali kosa. Ni kosa kubwa Sana kukubali kosa ulilokosa mbele ya mwanamke.
Thank me later.
Ni kweli umeongea point muhimu Sana

Hapa nimezungumzia makosa mbali mbali ambayo kama wanadamu huwa inatokea tutakoseana Kwa namna moja au nyingine.

Lakini point yako inategemea na mazingira vile vile, je kama umekamatwa live katika eneo la tukio na ushahidi uko wazi hapo bilashaka kukiri ukweli na kuomba msamaha hakukwepeki.
 
"USIMUOMBE MWANAMKE MSAMAHA WALA KUOMBA SAMAHANI, TOA TU SABABU YA KWANINI UMEFANYA ULICHOFANYA, NIMEFAMYA HIVI KWA SABABU a, b, c"


Mwisho wa kunukuu maneno ya mzee wa kisukuma.
Hilo nalo linategemeana na mazingira na Aina ya makosa.

Kuna makosa mengine kuomba msamaha ndio solution na si vinginevyo
 
Hata anikute gesti nitakataa katakata. Siku ukikubali ujue hiyo Ni precedent, kila mkikosana anaanza na Hilo ulilotubu kwa mdomo wako.
 
Hawa watu wa Jamii ya JF ni watu wa wapi? Yani umkosee mwanamke halafu usiombe msamaha 🤣🤣 kweli watu wanaishi katika ndoto.

Scenario 1: Mwanamke akukute kwa macho yake unamsaliti. Kisha ukatae katu katu kuwa hujamsaliti

Baada ya hapo aku accuse unamsaliti then unakataa kata kata kuwa sijakusaliti. Kisha mwanamke anasahau ulimsaliti na kukupa mapenzi mengiiiii kwa sababu tu umekataa kukubali kuwa wewe ni msaliti🤣🤣🤣

Najiulza hao ni wanawake wa wapi? Wa JF?

Wahenga walisema 'akili si nywele'. Akasikika mwana JF mmoja 'mwalimu na vuzi Je?'
 
Scenario 2: Mwanamke anakufumania kuwa na ushahidi umemsaliti. Kisha ukubali kuwa uliteleza na ukamsaliti.

Baada ya hapo huyu mwanamke ambaye umekubali amekusaliti kwa kujihakikishia nae anataka kukukomoa. Anakukomoaje?
Yeye pia anaenda kukusaliti. Je kweli akikusaliti amekukomoa?

Mwanamke yeyote anayedhania kuwa anamkomoa mwanaume ile tu kwa sababu amemsaliti basi nawaza ni mwanamke wa dunia ipi? Bila shaka watakuwepo dunia ya JF ya wale waotao mchana. .


hapa niseme tu 'kwa kweli ' Ahh kama wakigoma wanavyosema 'kwa kweri kigoma ni jiji ila daresalamu ni Noma'
 
"USIMUOMBE MWANAMKE MSAMAHA WALA KUOMBA SAMAHANI, TOA TU SABABU YA KWANINI UMEFANYA ULICHOFANYA, NIMEFAMYA HIVI KWA SABABU a, b, c"


Mwisho wa kunukuu maneno ya mzee wa kisukuma.
Labda uishi na KAHABA.

Ila NGURUMBEMBE kama li KAJ.LA kamwe siwezi kuliomba msamaha wowote, maana kila nitakalomfanyia ni halali yake.
 
Tatizo ukijishusha kwa mwanamke kwa nia njema huwa anakuchukulia poa na ndio maana wanaume wengi huwa tuna amuwa kuishi nao kimafia.
 
Tatizo ukijishusha kwa mwanamke kwa nia njema huwa anakuchukulia poa na ndio maana wanaume wengi huwa tuna amuwa kuishi nao kimafia.
Hapo ndo mnapokosea
Unaweza ukawa umepata wife material,anaejielewa na kujua wajibu wake kwa mumewe ila sasa hii attitude yako ikampoteza!
Unapaswa umsome mwanamke ulie nae ni wa aina gani usiishi kwa kukariri!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…