Unapozidishiwa chenji huwa unarudisha au ndio wimbo wa Albert Mangwear "kimya kimya" mwendo wa haraka mbele

Unapozidishiwa chenji huwa unarudisha au ndio wimbo wa Albert Mangwear "kimya kimya" mwendo wa haraka mbele

Ndio maisha Hayo mm sirudishagi Kuna siku nilienda kwa wakala kueka buk mbili nibetie maana bum lilikua limeisha akaweka buk 20 Sasa scenario hiyo unarudishaje hela ....take it ukifika muda wa kurudisha utarudisha tu
 
Katika mihangaiko ya hapa na pale unaweza kwenda dukani ama sokoni inapotokea muuzaji kakuzidishia 'chenji" unachukua hatua gani!??

Binafsi huwa narudisha
Wewe je? Wafanyabiashara wanapitia changamoto sana
Kuna mwamba alienda dukani kununua kitu akarudishiwa chenji. Sasa kwa vile jamaa alikuwa na stress kwa haraka haraka akajua mwenye duka kamzidishia chenji, hivyo akarudisha hela nusu kwa mwenye duka akimwambia kuwa amemzidishia. Mwenye duka nae hakukataa akapokea chap chap na kuzirudisha ndani ya droo la hela.

Mwamba ameenda kufika mbele ndo akili zinamrudia kuwa hela aliyokuwa nayo ni nusu. So ikabidi arudi kwa mwenye duka ili amrudishie zile hela alizodai kuwa kamzidishia. Cha ajabu alivyofika kule mwenye duka kagoma kumpa zile hela, eti chenji aliyomrudishia ilikuwa ni sawa. Jamaa kwa hasira kaondoka huku akimtukana muuza duka kuwa mzulumati. Sasa hapo nani anastahili lawama? Jamaa wema umemponza.
 
Hela nyingi nilizowahi kurudisha kwa mteja wangu zilikuwa 2.5m huyu alikuwa mke wa mwenye duka ndio alipewa maelekezo aniandalie 2.5 badala yake akaniwekea mezani 5m

Nikamwambia kwa kuziangalia tu hizi ni zaidi ya 2.5
Nikahakiki zangu nikamrudishia zake
Wa pili yeye alikuja kununua bidhaa akanizidishia laki 3, nilipomwambia hizi zimezidi alikaa chini kama dakika 3 hivi
Akaniambia sikutegemea mtu anaweza kurudisha laki 3 aliyozidishiwa
Nikamwambia najua wewe usingenirudishia
Cheko la huzuni likamtoka
 
Mwaka 2009 nilitumwa umeme Wa LUKU kipindi hiki umeme ulikuwa unanunuliwa Tanesco tu

Baada ya kupewa elfu tano nikatoa buku kwa ajili ya kununulia Peni na rula sikumuambia MTU .

So ile elfu nne nikaenda nayo kununua umeme

Kufika pale Tanesco yule jamaa aliniwekea umeme wa laki nne

Sasa umeme ulipomaliza muda mrefu bila kukatika watu hawakua wanajua .

Then mwenye nyumba akawa anachukua hela za umeme Kama kawaida huku umeme ukiendelea kuwepo


Kimbembe umeme ulipoisha Tanesco walianza kukata hela yao kila tukinunua .
 
Mwaka 2009 nilitumwa umeme Wa LUKU kipindi hiki umeme ulikuwa unanunuliwa Tanesco tu

Baada ya kupewa elfu tano nikatoa buku kwa ajili ya kununulia Peni na rula sikumuambia MTU .

So ile elfu nne nikaenda nayo kununua umeme

Kufika pale Tanesco yule jamaa aliniwekea umeme wa laki nne

Sasa umeme ulipomaliza muda mrefu bila kukatika watu hawakua wanajua .

Then mwenye nyumba akawa anachukua hela za umeme Kama kawaida huku umeme ukiendelea kuwepo


Kimbembe umeme ulipoisha Tanesco walianza kukata hela yao kila tukinunua .
😂Hio tunaita muosha kaoshwa
 
Asubuhi moja nimewahi CRDB bank ku deposit kama 2m plus. Nikajaza ile slip nikamaliza nikampa teller halafu nikatoa hela nikaziweka juu pale sijamuingizia kwenye kidirisha chake. Teller yuko busy anaingiza muamala. Kamaliza kanipa slip yangu, nikabaki namwangalia na yeye ananiangalia kama ananiuliza unasubiri nini hajui kama sijampa hela. Nikamwambia naomba nikuzawadie hizi hela, alishtuka sana akaziwahi chap akahesabu zimetimia akanishukuru huku akisema ameamka na stress sana hio siku,akasema ningeondoka angehangaika mwisho wa siku bila kujua short imetokea wapi.
 
Asubuhi moja nimewahi CRDB bank ku deposit kama 2m plus. Nikajaza ile slip nikamaliza nikampa teller halafu nikatoa hela nikaziweka juu pale sijamuingizia kwenye kidirisha chake. Teller yuko busy anaingiza muamala. Kamaliza kanipa slip yangu, nikabaki namwangalia na yeye ananiangalia kama ananiuliza unasubiri nini hajui kama sijampa hela. Nikamwambia naomba nikuzawadie hizi hela, alishtuka sana akaziwahi chap akahesabu zimetimia akanishukuru huku akisema ameamka na stress sana hio siku,akasema ningeondoka angehangaika mwisho wa siku bila kujua short imetokea wapi.
Ni mambo kama haya haya yanatokea madukani na kwa mawakala lakini chuma ulete ndo wanalaumiwa.
 
Kimbembe umeme ulipoisha Tanesco walianza kukata hela yao kila tukinunua .
Mwenye nyumba alitoa maelezo gani baada ya nyinyi kushangaa makato? Ila muuza LUKU mwezi huo alikula bonge ya hasara.
 
Back
Top Bottom