Unaruhusuje Mitaala ya nchi za magharibi itumike nchini halafu unayakataa Maadili yao?

Unaruhusuje Mitaala ya nchi za magharibi itumike nchini halafu unayakataa Maadili yao?

Moja ya sababu za Russia kufanya operation yake dhidi ya Ukraine,ni kutokomeza utamaduni wa kimagharibi katika jamii ya warusi waliokuwa wanaishi Ukraine.Ukraine ilikuwa imisha anza kubadilisha mitaala ya shule iliyokiwa IPO katika lugha ya kirusi na kupandikiza mitaala ya kimagharibi.

Taifa lolote LA watu wanaojitambua hawawezi kuruhusu mitaala au ustaarabu wa mataifa mengine ndani ya Nchi yao.
 
Ile methali ya mtaka cha uvunguni sharti ainame tumeisahau?

Na kuna wakati mchonga alituonya kuwa wale wanaosema kule nje kuna hela nyingi, siku mkiletewa hela ya wauza bangi mtafanyaje?

Kimsingi, maadili ya magharibi yamemomonyoka sana na washaamua kuleta hilo zahma dunia nzima.

Historia inaonesha shule nyingi hapa Tanganyika na wakati wa Deusche Ostafrika zilimilikiwa na mashirika na dini hasa Anglican, Lutheran na Catholics. Moja ya msingi wa Imani ni kutii amri 10 za Mungu na kufuata biblia kama msaafu kimaadili hasa kwenye kuzuia uzinzi na uasherati.

Baada ya Uhuru kupatikana, JKN na waliofuatia walibaki wakiamini sheria za kuzuia uasherati na wenye mimba walifurushwa shule.
Misaada imetufanya 'tuiname' na sasa kama wenye mimba wanaruhisiwa kusoma na ruksa kurejea baada ya kujifungua, msingi wake, sheria ya kuzuia uasherati mashuleni sioni kama inasimama tena.

Ngamia huanza kuongoza kwato, baadae miguu, baadae kichwa, baadae mwili mzima na kajumba huwa kanajiangukia.

Tukifanya tathmini, sijui ngamia Yuko stage gani kwenye kutaka kuzama ndani ya nyumba yetu.

Profesa Mkenda 'anakomaa' ila wale wanaotoa budget support wizara ya Elimu kama wataona anazuia 'koneksheni' je atabaki kazini?

Kama alivyowahi kugoma kusaini kutoa vibali vya sukari kinyume na utaratibu, je, wazeiya wakimwaga pichi na kushinikiza mitaala ipitiwe upya ili masuala ya 'upinde wa mvua' kuwa sehemu ya mafunzo, na sio lazima kuona kuna he na she ila tukaaminishwa wanadamu ni zaidi ya he na she, je, prof ataweza kusimama kama Qatar kuzuia mafuriko ya mmomonyoko wa maadili bila support ya toka juu.

Wakati huzungumza na kufichua mengi yaliyositirika.

Mchana mwema!
Kongole kwako mkuu. Sasa hoja inakuja hivi; Kwa distance ambayo tumeshakwenda, kugeuza na kuanza kurudi tulikotoka ni mbali na ni gharama kubwa na halafu hatuko wamoja(hatuja simama pamoja) Kila mmoja anaimba wimbo wake.

Wapo wanaoamini na kuona kwamba kila kilichotoka magharibi ni kibaya(kitu ambacho ni dhana potofu kabisa) Wapo wanaoamini na kuona bora tuwe na mambo yetu wenyewe. Dhana hii ndo ya kipumbavu kabisa kwani Hatuko peke yetu hapa duniani au hapa sio "kisiwani" na hata hivyo hatuna chetu cha kipekee sana cha kuweza kujivunia.

Wapo wanaoamini na kuona kwamba tufanye kubalance mambo, tuchuje yale yaliyo mema(Yanayotufaa katika mazingira yetu) na tuibue mapya ya kikwetu zaidi kwa kutumia rasilmali zetu wenyewe. Hii ina mashiko zaidi lakini hoja inakuja, Je, wale "wawindaji" wanaotaka kujinufaisha binafsi tutawaweka fungu gani?- Uchu wa madaraka, Utajiri wa haraka -haraka, Umimi au wa-Kwetu huyu, Nidhamu mbovu n.k.

Lipo kundi la watu wa kiaina fulani ambalo ni hatari mno kwani hata lifanyike zuri kiasi gani wao hutoa Tasiri potofu na wapo negative saa zote na ni werevu mno kwa kupenyeza hoja fikirishi zisizo na ukweli wowote e.g. 1. Kuna ililetwa hapa, hoja ya watoto mashuleni kufundishwa kulawitiana - hivi kweli inawezekana? na huyo mwalimu atasimamaje hapo mbele ya darasa watoto say 45?. 2. Kwenye uzi huu wapo waliopindisha uzi na kupenyeza hoja ya Ushoga badala ya Mitaala ya Magharibi. Yan wao neno magharibi linamaanisha Ushoga.
Ni Tatizo na ni Fujo.

Viongozi na wenye dhamana ya kusimamia masuala yote ya Elimu watashindwa kutulia, kutafakari na hatimaye kupata njia mujarabu kwa Hatima ya Elimu italewayo hapa nchini.
 
Wazazi wa Tanzania wapo busy na CCM,hawana habari kuwa syllabus zinafundisha watoto wao ushoga huko mashuleni👇🐒🐒🐒
View attachment 2485772
Fainali juu ya upuuzi huo inachezwa AFRICA, na TANZANIA ndo main ground.

Dunia inaenda kujigawa pande mbili.

Wapinga Mungu na Waamini Mungu,

Ni Jesus followers Vs Anti Christ.

Freemasonry vs God believers.

Tusubiri.
 
Una uhakika hiki kimeanza kufundishwa mkuu?
Shule zipi hizo?
Kinafundishwa Marekani na Nchi nyingi Ulaya.

Na aliyewaaminisha wanawake kuwa Kuna SURUALI za kike alijua tutafika huko.

Kwa jinsi Serikali inavyotegemea mikopo ni ngumu kukataa Masharti hayo,

mabadiliko kiuongozi lazima yatokee kukabiliana na Hali hiyo.

Tuanze kujitegemea.
 
Kinafundishwa Marekani na Nchi nyingi Ulaya.

Na aliyewaaminisha wanawake kuwa Kuna SURUALI za kike alijua tutafika huko.

Kwa jinsi Serikali inavyotegemea mikopo ni ngumu kukataa Masharti hayo,

mabadiliko kiuongozi lazima yatokee kukabiliana na Hali hiyo.

Tuanze kujitegemea.
Tuanze kujitegemea kwa kiongozi yupi na mipango ipi?.
Tunapaswa kujitambua kabla ya yote
 
Back
Top Bottom