Unataka Kupima kama huyo Mpenzi wako ni Wife Material? Mpeleke kwa Mama Ntilie, akisumbua mhudumu mara 3 kwa sababu zinazovumilika PIGA CHINI!

Chukua huyo wife material anayesema hawezi Kula chakula cha mwanamke mwenzie!!!!
Achana na akina Mimi nikiwa mwenyewe,hata mwezi unakata Sijaingia jikoni halafu fresh tu🤗🤗🤗🤗🤗🤗
 
Lakini chipsi anakula na hajari kama mishkaki imelala; kweli adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe
Kwenye chips sijawah msikia,tena kuna sehem ni maarufu sana kuna wapika chips wengi sana lakin ile sehem chips zao sio nzur kabisa mara ziungue mayai wanaweka kidogo hata viazi,customer care hawana

Yaan mimi ndo niliianza kumsanua kuwa hapa hapana tuwe tunaenda kwingine ila yeye alikuwa haoni wala kusikia
 
Nilikutana na mmoja mjinga sana aircondition ipo mpaka mwisho ila bado anaita wahudumu waje warekebishe maana haifanyi kazi vizuri, mara chakula kina chumvi kibao anaita tena mhudumu kumsema, usiku mara usinikojolee ndani tutagombana, asubuhi tulivyoondoka nikapiga chini ujinga staki
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu ila unaongea fact..🤣🤣🤣🤣🤣 Kuna demu nilimtoa out sehemu tukale kitimotooo aiseee hapanaa pale ndo nikajua huyu ni bomuuu haswaaaa yani hamna mke paleee analalamika mpaka vitu vidogo sana ambavyo unaweza hata usinotice just imagine alihesabu vipande vya ndizi zile nusu nusu wanakata kwenye kitimoto pia akaangalia moja size ilikuwa ndogo sana nilimkataza apotezeee tutalipa tu weew alimuita mhudumu akamchambaa na akasema hatulipiii ndizi zile ndogo🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣mamaeee nilijisikia aibuu sanaaa yule manzi nilipotoka pale na namba nikafutaaa khaaa uvumilivu hama kabisa.
 
Acha mbinu za mwaka 1947! Bro tumeishatoka huko, ni sawa na kusema oa mwanamke anayejua kufua, kulima,kupika! Mambo ya hovyo kabisa, kuna mashine za, kufua, kukausha, kulima, kupanda! Tupo 2025!
 
Acha mbinu za mwaka 1947! Bro tumeishatoka huko, ni sawa na kusema oa mwanamke anayejua kufua, kulima,kupika! Mambo ya hovyo kabisa, kuna mashine za, kufua, kukausha, kulima, kupanda! Tupo 2025!
Mpka sasa kuna Wanawake wa familia za Kawaida hawajui kupika hivi hii usababishwa na nini ?😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…