Unataka Pendekezo lako la Mradi lifanikiwe? Zingatia yafuatayo

Unataka Pendekezo lako la Mradi lifanikiwe? Zingatia yafuatayo

Joined
Feb 5, 2022
Posts
38
Reaction score
60
teacher-in-classroom-students.jpg


Pendekezo la Mradi yaani "Grant/Business Proposal" ni andiko linaloonyesha hitaji (need), fursa (opportunity), au tatizo (problem) lenye kuhitaji kuchuliwa hatua. Mmiliki wa tatizo, fursa au hitaji anaweza kuwa Taasisi, Kampuni, Jamii au hata mtu mmoja mmoja. Kupitia Pendekezo la Mradi, muandaaji huweza kuainisha mpango (a detailed plan) unaohitajika ili kutatua tatizo (ikiwa kuna tatizo) , kufaidika na fursa (ikiwa suala ni fursa) au kukidhi hitaji (ikiwa suala ni hitaji). Mbali na mpango, muandaaji pia anapaswa kuainisha gharama za utekelezaji wa mradi, matokeo yanayotarajiwa kutokea baada ya utekelezaji wa Mradi, na makadirio ya muda wa utekelezaji wa Mradi.

Uandaaji wa Pendekezo la Mradi ni miongoni mwa njia za utafutaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi kwa Taasisi, Kampuni na hata kwa mtu mmoja mmoja. Pendekezo zuri la Mradi yaani "Successful Grant/Business Proposal" hujengwa katika misingi mikuu miwili, ambayo ni;
  • Kuijua hadhira yako ambayo ni; wafadhili au wadau wa mradi wako.
  • Kuandika kile ambacho hadhira yako inataka kujua na si kile unachojua wewe.
Ukiwa kama muandaaji wa Pendekezo la Mradi (Grant Writer) ni jukumu lako kuhakikisha unakuwa na ufahamu wa kutosha juu ya hadhira yako; hawa ndio watu ambao watasoma na kutoa maoni juu ya pendekezo lako la mradi. Wafadhili wamegawanyika katika sekta tofauti tofauti, kuna wafadhili ambao wamejikita na Miradi yenye misingi ya kisheria na haki kwa mfano Legal Service Facility (LSF), wengine wamejikita katika mazingira kwa mfano Tanzania Forest Fund (Mfuko wa Misitu Tanzania)

Hivyo basi pindi uandaapo Pendekezo lako la Mradi zingatia sekta ambayo mradi wako umejikita, na uandishi wako ujikite katika mtazamo (perspective) wa hao unaowaandikia pendekezo hilo. Kwa mfano; utafanya makosa endapo utatumia misamiati ya kisheria katika uandaaji wa pendekezo la mradi wa mazingira au ufanye kinyume chake.

Kujua hadhira yako inataka nini katika pendekezo lako la Mradi, Wito wa Uwasilishaji wa Mapendekezo ya Miradi yaani "Request for Proposals" ni nyaraka muhimu kwako itakayokujulisha juu ya nini mfadhili anataka kujua kutoka kwako. Nyaraka hii itaweza kukuonyesha maudhui ya mradi "thematic areas", aina ya miradi inayopendekezwa kwa kila "thematic area". Haiishii hapo nyaraka hii itaweza pia kukuonyesha bajeti ya programu (Ufafanuzi: Programu ni mjumuiko wa miradi mbalimbali yenye kushabihiana malengo) mbali na bajeti ya programu pia nyaraka hii itakuonyesha kiasi cha chini kabisa kuomba kwa ajili ya pendekezo lako (Award Floor) na kiasi cha juu kuomba (Award Ceiling) kwa pendekezo. Pia nyaraka hii itakuonyesha namna ya kuwasilisha pendekezolako, muda wa uwasilishaji wa pendekezo lako n.k

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
 
Umetembea mulemule safi sana. Hongera mtaalam nikiwa na kazi nitakutafuta.
 
Dah!!
Niko na ma idea kibao hafu naonaga processes ni ndeeefu.
 
teacher-in-classroom-students.jpg


Pendekezo la Mradi yaani "Grant/Business Proposal" ni andiko linaloonyesha hitaji (need), fursa (opportunity), au tatizo (problem) lenye kuhitaji kuchuliwa hatua. Mmiliki wa tatizo, fursa au hitaji anaweza kuwa Taasisi, Kampuni, Jamii au hata mtu mmoja mmoja. Kupitia Pendekezo la Mradi, muandaaji huweza kuainisha mpango (a detailed plan) unaohitajika ili kutatua tatizo (ikiwa kuna tatizo) , kufaidika na fursa (ikiwa suala ni fursa) au kukidhi hitaji (ikiwa suala ni hitaji). Mbali na mpango, muandaaji pia anapaswa kuainisha gharama za utekelezaji wa mradi, matokeo yanayotarajiwa kutokea baada ya utekelezaji wa Mradi, na makadirio ya muda wa utekelezaji wa Mradi.

Uandaaji wa Pendekezo la Mradi ni miongoni mwa njia za utafutaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi kwa Taasisi, Kampuni na hata kwa mtu mmoja mmoja. Pendekezo zuri la Mradi yaani "Successful Grant/Business Proposal" hujengwa katika misingi mikuu miwili, ambayo ni;
  • Kuijua hadhira yako ambayo ni; wafadhili au wadau wa mradi wako.
  • Kuandika kile ambacho hadhira yako inataka kujua na si kile unachojua wewe.
Ukiwa kama muandaaji wa Pendekezo la Mradi (Grant Writer) ni jukumu lako kuhakikisha unakuwa na ufahamu wa kutosha juu ya hadhira yako; hawa ndio watu ambao watasoma na kutoa maoni juu ya pendekezo lako la mradi. Wafadhili wamegawanyika katika sekta tofauti tofauti, kuna wafadhili ambao wamejikita na Miradi yenye misingi ya kisheria na haki kwa mfano Legal Service Facility (LSF), wengine wamejikita katika mazingira kwa mfano Tanzania Forest Fund (Mfuko wa Misitu Tanzania)

Hivyo basi pindi uandaapo Pendekezo lako la Mradi zingatia sekta ambayo mradi wako umejikita, na uandishi wako ujikite katika mtazamo (perspective) wa hao unaowaandikia pendekezo hilo. Kwa mfano; utafanya makosa endapo utatumia misamiati ya kisheria katika uandaaji wa pendekezo la mradi wa mazingira au ufanye kinyume chake.

Kujua hadhira yako inataka nini katika pendekezo lako la Mradi, Wito wa Uwasilishaji wa Mapendekezo ya Miradi yaani "Request for Proposals" ni nyaraka muhimu kwako itakayokujulisha juu ya nini mfadhili anataka kujua kutoka kwako. Nyaraka hii itaweza kukuonyesha maudhui ya mradi "thematic areas", aina ya miradi inayopendekezwa kwa kila "thematic area". Haiishii hapo nyaraka hii itaweza pia kukuonyesha bajeti ya programu (Ufafanuzi: Programu ni mjumuiko wa miradi mbalimbali yenye kushabihiana malengo) mbali na bajeti ya programu pia nyaraka hii itakuonyesha kiasi cha chini kabisa kuomba kwa ajili ya pendekezo lako (Award Floor) na kiasi cha juu kuomba (Award Ceiling) kwa pendekezo. Pia nyaraka hii itakuonyesha namna ya kuwasilisha pendekezolako, muda wa uwasilishaji wa pendekezo lako n.k

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Kuna organisations ambazo zinasaidia watu au others organisations and companies kupata funds like fundsforngo, gofundme etc etc. Wqnatoa service bure but unaweza pia kulipia kama unataka for premium membership ambayo wqnadai unapata msaada zaidi wa kupata funders. Je, ni kweli kuna unafuu kama ukilipia? Tupe uzoefu wako ktk mambo kama hayo please!
 
Kuna organisations ambazo zinasaidia watu au others organisations and companies kupata funds like fundsforngo, gofundme etc etc. Wqnatoa service bure but unaweza pia kulipia kama unataka for premium membership ambayo wqnadai unapata msaada zaidi wa kupata funders. Je, ni kweli kuna unafuu kama ukilipia? Tupe uzoefu wako ktk mambo kama hayo please!
Ndio. Kuna Taasisi ambazo husaidia watu kupata ruzuku.
Ila zingatia; Fundsforngos haijishughulishi na utoaji wa ruzuku kwa miradi, ila inatoa taarifa juu ya wapi ruzuku inapatikana na kwa taratibu zipi.
Huduma hii kwa fundsforngos hutolewa bure, isipokuwa kuna baadhi ya fursa hutolewa tu kwa wale waliojiunga kwa malipo yaani "premium members" Utofauti wa kuitumia fundsforngos bila kulipia na kuitumia ukiwa mwanachama ni kwamba fursa kama; taarifa juu ya KILA ruzuku, majarida mbalimbali na mafunzo ya mtandaoni juu ya fundraising hutopata ikiwa wewe si mwanachama.
Unataka kujua kama kuna nafuu, endapo utalipia. Kwa uzoefu wangu inategemea na uelewa wako na Taasisi yako juu ya "grant researching na fundraising skills". Ikiwa ufahamu wako na kwa Taasisi yako ni mdogo katika maeneo haya, kulipia kutakufaa kwa sababu; mbali na kukupa taarifa za KILA ruzuku pia utajifunza vitu vingi, tofauti na hivyo hakutokuwa na ulazima wa kujiunga.

Kuhusu taarifa juu ya ruzuku, fahamu tu kwamba kuna Taasisi zingine nyingi zinazotoa taarifa bure, ila hutopata KILA taarifa ya ruzuku kwa mfano kuna advance-africa, BOND, commission.europe, voice.global, terravivagrants na nyinginezo. Lingine la kufahamu ni kwamba taarifa yoyote inayotolewa na fundsforngos ina chanzo chake ambacho ndie mfadhili husika, kwa hiyo kama una ufahamu juu ya grant researching, taarifa nyingi tu za ruzuku utaweza kuzipata kutoka kwenye vyanzo halisi .

Katika swali lako umetaja gofundme, malengo ya gofundme na fundsforngos ni tofauti. Gofundme ni taasisi ambayo inajishughulisha na ukusanyaji wa fedha kwa miradi mbalimbali inayowasilishwa na Taasisi mbalimbali. Ukusanyaji wa fedha hufanyika kupitia jamii ya mtandaoni (online community) kwa kitaalamu utafutaji wa ruzuku kupitia Taasisi kama gofundme hujulikana kama "crowdfunding"
Kuna Taasisi zingine nyingi zenye kuaminika ambazo hutoa huduma hii kwa mfano kuna Global Giving, KickStarter, Indiegogo n.k. Mara nyingi kwenye Taasisi hizi, unajiunga bure kwa kuwasilisha taarifa muhimu za Taasisi yako, kisha taarifa za Mradi. Unapofanikiwa ku-raise fedha kwa ajili ya mradi wako, wao huchukua asilimi kadhaa ya kiasi kilichopatikana, na wengine huenda mbele zaidi kwa ku-charge miamala (transaction fee)
Zingatia: Ili uweze kunufuika na fursa zilizoko kwenye hizi "crowdfunding platfroms" Taasisi yako au wewe mweyewe binafsi unapaswa uwe umewekeza kwenye mitandao ya kijamii (having presence on social media networks)

Natumai maelezo yangu yamekutosheleza.
Ahsante .

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
 
Ndio. Kuna Taasisi ambazo husaidia watu kupata ruzuku.
Ila zingatia; Fundsforngos haijishughulishi na utoaji wa ruzuku kwa miradi, ila inatoa taarifa juu ya wapi ruzuku inapatikana na kwa taratibu zipi.
Huduma hii kwa fundsforngos hutolewa bure, isipokuwa kuna baadhi ya fursa hutolewa tu kwa wale waliojiunga kwa malipo yaani "premium members" Utofauti wa kuitumia fundsforngos bila kulipia na kuitumia ukiwa mwanachama ni kwamba fursa kama; taarifa juu ya KILA ruzuku, majarida mbalimbali na mafunzo ya mtandaoni juu ya fundraising hutopata ikiwa wewe si mwanachama.
Unataka kujua kama kuna nafuu, endapo utalipia. Kwa uzoefu wangu inategemea na uelewa wako na Taasisi yako juu ya "grant researching na fundraising skills". Ikiwa ufahamu wako na kwa Taasisi yako ni mdogo katika maeneo haya, kulipia kutakufaa kwa sababu; mbali na kukupa taarifa za KILA ruzuku pia utajifunza vitu vingi, tofauti na hivyo hakutokuwa na ulazima wa kujiunga.

Kuhusu taarifa juu ya ruzuku, fahamu tu kwamba kuna Taasisi zingine nyingi zinazotoa taarifa bure, ila hutopata KILA taarifa ya ruzuku kwa mfano kuna advance-africa, BOND, commission.europe, voice.global, terravivagrants na nyinginezo. Lingine la kufahamu ni kwamba taarifa yoyote inayotolewa na fundsforngos ina chanzo chake ambacho ndie mfadhili husika, kwa hiyo kama una ufahamu juu ya grant researching, taarifa nyingi tu za ruzuku utaweza kuzipata kutoka kwenye vyanzo halisi .

Katika swali lako umetaja gofundme, malengo ya gofundme na fundsforngos ni tofauti. Gofundme ni taasisi ambayo inajishughulisha na ukusanyaji wa fedha kwa miradi mbalimbali inayowasilishwa na Taasisi mbalimbali. Ukusanyaji wa fedha hufanyika kupitia jamii ya mtandaoni (online community) kwa kitaalamu utafutaji wa ruzuku kupitia Taasisi kama gofundme hujulikana kama "crowdfunding"
Kuna Taasisi zingine nyingi zenye kuaminika ambazo hutoa huduma hii kwa mfano kuna Global Giving, KickStarter, Indiegogo n.k. Mara nyingi kwenye Taasisi hizi, unajiunga bure kwa kuwasilisha taarifa muhimu za Taasisi yako, kisha taarifa za Mradi. Unapofanikiwa ku-raise fedha kwa ajili ya mradi wako, wao huchukua asilimi kadhaa ya kiasi kilichopatikana, na wengine huenda mbele zaidi kwa ku-charge miamala (transaction fee)
Zingatia: Ili uweze kunufuika na fursa zilizoko kwenye hizi "crowdfunding platfroms" Taasisi yako au wewe mweyewe binafsi unapaswa uwe umewekeza kwenye mitandao ya kijamii (having presence on social media networks)

Natumai maelezo yangu yamekutosheleza.
Ahsante .

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
thanks a lot. Nimekupata vema mkuu.
 
Ndio. Kuna Taasisi ambazo husaidia watu kupata ruzuku.
Ila zingatia; Fundsforngos haijishughulishi na utoaji wa ruzuku kwa miradi, ila inatoa taarifa juu ya wapi ruzuku inapatikana na kwa taratibu zipi.
Huduma hii kwa fundsforngos hutolewa bure, isipokuwa kuna baadhi ya fursa hutolewa tu kwa wale waliojiunga kwa malipo yaani "premium members" Utofauti wa kuitumia fundsforngos bila kulipia na kuitumia ukiwa mwanachama ni kwamba fursa kama; taarifa juu ya KILA ruzuku, majarida mbalimbali na mafunzo ya mtandaoni juu ya fundraising hutopata ikiwa wewe si mwanachama.
Unataka kujua kama kuna nafuu, endapo utalipia. Kwa uzoefu wangu inategemea na uelewa wako na Taasisi yako juu ya "grant researching na fundraising skills". Ikiwa ufahamu wako na kwa Taasisi yako ni mdogo katika maeneo haya, kulipia kutakufaa kwa sababu; mbali na kukupa taarifa za KILA ruzuku pia utajifunza vitu vingi, tofauti na hivyo hakutokuwa na ulazima wa kujiunga.

Kuhusu taarifa juu ya ruzuku, fahamu tu kwamba kuna Taasisi zingine nyingi zinazotoa taarifa bure, ila hutopata KILA taarifa ya ruzuku kwa mfano kuna advance-africa, BOND, commission.europe, voice.global, terravivagrants na nyinginezo. Lingine la kufahamu ni kwamba taarifa yoyote inayotolewa na fundsforngos ina chanzo chake ambacho ndie mfadhili husika, kwa hiyo kama una ufahamu juu ya grant researching, taarifa nyingi tu za ruzuku utaweza kuzipata kutoka kwenye vyanzo halisi .

Katika swali lako umetaja gofundme, malengo ya gofundme na fundsforngos ni tofauti. Gofundme ni taasisi ambayo inajishughulisha na ukusanyaji wa fedha kwa miradi mbalimbali inayowasilishwa na Taasisi mbalimbali. Ukusanyaji wa fedha hufanyika kupitia jamii ya mtandaoni (online community) kwa kitaalamu utafutaji wa ruzuku kupitia Taasisi kama gofundme hujulikana kama "crowdfunding"
Kuna Taasisi zingine nyingi zenye kuaminika ambazo hutoa huduma hii kwa mfano kuna Global Giving, KickStarter, Indiegogo n.k. Mara nyingi kwenye Taasisi hizi, unajiunga bure kwa kuwasilisha taarifa muhimu za Taasisi yako, kisha taarifa za Mradi. Unapofanikiwa ku-raise fedha kwa ajili ya mradi wako, wao huchukua asilimi kadhaa ya kiasi kilichopatikana, na wengine huenda mbele zaidi kwa ku-charge miamala (transaction fee)
Zingatia: Ili uweze kunufuika na fursa zilizoko kwenye hizi "crowdfunding platfroms" Taasisi yako au wewe mweyewe binafsi unapaswa uwe umewekeza kwenye mitandao ya kijamii (having presence on social media networks)

Natumai maelezo yangu yamekutosheleza.
Ahsante .

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Asante kwa ufafanuzi mzur mkuu.
 
teacher-in-classroom-students.jpg


Pendekezo la Mradi yaani "Grant/Business Proposal" ni andiko linaloonyesha hitaji (need), fursa (opportunity), au tatizo (problem) lenye kuhitaji kuchuliwa hatua. Mmiliki wa tatizo, fursa au hitaji anaweza kuwa Taasisi, Kampuni, Jamii au hata mtu mmoja mmoja. Kupitia Pendekezo la Mradi, muandaaji huweza kuainisha mpango (a detailed plan) unaohitajika ili kutatua tatizo (ikiwa kuna tatizo) , kufaidika na fursa (ikiwa suala ni fursa) au kukidhi hitaji (ikiwa suala ni hitaji). Mbali na mpango, muandaaji pia anapaswa kuainisha gharama za utekelezaji wa mradi, matokeo yanayotarajiwa kutokea baada ya utekelezaji wa Mradi, na makadirio ya muda wa utekelezaji wa Mradi.

Uandaaji wa Pendekezo la Mradi ni miongoni mwa njia za utafutaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi kwa Taasisi, Kampuni na hata kwa mtu mmoja mmoja. Pendekezo zuri la Mradi yaani "Successful Grant/Business Proposal" hujengwa katika misingi mikuu miwili, ambayo ni;
  • Kuijua hadhira yako ambayo ni; wafadhili au wadau wa mradi wako.
  • Kuandika kile ambacho hadhira yako inataka kujua na si kile unachojua wewe.
Ukiwa kama muandaaji wa Pendekezo la Mradi (Grant Writer) ni jukumu lako kuhakikisha unakuwa na ufahamu wa kutosha juu ya hadhira yako; hawa ndio watu ambao watasoma na kutoa maoni juu ya pendekezo lako la mradi. Wafadhili wamegawanyika katika sekta tofauti tofauti, kuna wafadhili ambao wamejikita na Miradi yenye misingi ya kisheria na haki kwa mfano Legal Service Facility (LSF), wengine wamejikita katika mazingira kwa mfano Tanzania Forest Fund (Mfuko wa Misitu Tanzania)

Hivyo basi pindi uandaapo Pendekezo lako la Mradi zingatia sekta ambayo mradi wako umejikita, na uandishi wako ujikite katika mtazamo (perspective) wa hao unaowaandikia pendekezo hilo. Kwa mfano; utafanya makosa endapo utatumia misamiati ya kisheria katika uandaaji wa pendekezo la mradi wa mazingira au ufanye kinyume chake.

Kujua hadhira yako inataka nini katika pendekezo lako la Mradi, Wito wa Uwasilishaji wa Mapendekezo ya Miradi yaani "Request for Proposals" ni nyaraka muhimu kwako itakayokujulisha juu ya nini mfadhili anataka kujua kutoka kwako. Nyaraka hii itaweza kukuonyesha maudhui ya mradi "thematic areas", aina ya miradi inayopendekezwa kwa kila "thematic area". Haiishii hapo nyaraka hii itaweza pia kukuonyesha bajeti ya programu (Ufafanuzi: Programu ni mjumuiko wa miradi mbalimbali yenye kushabihiana malengo) mbali na bajeti ya programu pia nyaraka hii itakuonyesha kiasi cha chini kabisa kuomba kwa ajili ya pendekezo lako (Award Floor) na kiasi cha juu kuomba (Award Ceiling) kwa pendekezo. Pia nyaraka hii itakuonyesha namna ya kuwasilisha pendekezolako, muda wa uwasilishaji wa pendekezo lako n.k

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Sawa
 
Ndio. Kuna Taasisi ambazo husaidia watu kupata ruzuku.
Ila zingatia; Fundsforngos haijishughulishi na utoaji wa ruzuku kwa miradi, ila inatoa taarifa juu ya wapi ruzuku inapatikana na kwa taratibu zipi.
Huduma hii kwa fundsforngos hutolewa bure, isipokuwa kuna baadhi ya fursa hutolewa tu kwa wale waliojiunga kwa malipo yaani "premium members" Utofauti wa kuitumia fundsforngos bila kulipia na kuitumia ukiwa mwanachama ni kwamba fursa kama; taarifa juu ya KILA ruzuku, majarida mbalimbali na mafunzo ya mtandaoni juu ya fundraising hutopata ikiwa wewe si mwanachama.
Unataka kujua kama kuna nafuu, endapo utalipia. Kwa uzoefu wangu inategemea na uelewa wako na Taasisi yako juu ya "grant researching na fundraising skills". Ikiwa ufahamu wako na kwa Taasisi yako ni mdogo katika maeneo haya, kulipia kutakufaa kwa sababu; mbali na kukupa taarifa za KILA ruzuku pia utajifunza vitu vingi, tofauti na hivyo hakutokuwa na ulazima wa kujiunga.

Kuhusu taarifa juu ya ruzuku, fahamu tu kwamba kuna Taasisi zingine nyingi zinazotoa taarifa bure, ila hutopata KILA taarifa ya ruzuku kwa mfano kuna advance-africa, BOND, commission.europe, voice.global, terravivagrants na nyinginezo. Lingine la kufahamu ni kwamba taarifa yoyote inayotolewa na fundsforngos ina chanzo chake ambacho ndie mfadhili husika, kwa hiyo kama una ufahamu juu ya grant researching, taarifa nyingi tu za ruzuku utaweza kuzipata kutoka kwenye vyanzo halisi .

Katika swali lako umetaja gofundme, malengo ya gofundme na fundsforngos ni tofauti. Gofundme ni taasisi ambayo inajishughulisha na ukusanyaji wa fedha kwa miradi mbalimbali inayowasilishwa na Taasisi mbalimbali. Ukusanyaji wa fedha hufanyika kupitia jamii ya mtandaoni (online community) kwa kitaalamu utafutaji wa ruzuku kupitia Taasisi kama gofundme hujulikana kama "crowdfunding"
Kuna Taasisi zingine nyingi zenye kuaminika ambazo hutoa huduma hii kwa mfano kuna Global Giving, KickStarter, Indiegogo n.k. Mara nyingi kwenye Taasisi hizi, unajiunga bure kwa kuwasilisha taarifa muhimu za Taasisi yako, kisha taarifa za Mradi. Unapofanikiwa ku-raise fedha kwa ajili ya mradi wako, wao huchukua asilimi kadhaa ya kiasi kilichopatikana, na wengine huenda mbele zaidi kwa ku-charge miamala (transaction fee)
Zingatia: Ili uweze kunufuika na fursa zilizoko kwenye hizi "crowdfunding platfroms" Taasisi yako au wewe mweyewe binafsi unapaswa uwe umewekeza kwenye mitandao ya kijamii (having presence on social media networks)

Natumai maelezo yangu yamekutosheleza.
Ahsante .

OMAR MSONGA (BA. PPM &CD)
CONSULTANT
Project Management, Strategy, Fundraising & Training
Call: +255 719 518 367
Email: omarmsonga8@gmail.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA
Mzee baba umemwaga madini tupu
 
Je unawezaje kupata fund za mradi?
Ndio, unaweza kupata "fund" kwa ajili ya kutekeleza mradi wako.
Kabla ya kuendelea kujibu swali lako, ningependa kukufahamisha kwanza aina za ruzuku ambazo unaweza kuomba, nazo ni;
  • Capital Grant: hii ni ruzuku inayoombwa na Taasisi kwa ajili ya ukarabati au ujenzi wa mioundombinu ya Taasisi kama vile jego la ofisi n.k
  • General Operating Grant: Hii ni ruzuku inayoombwa na Taasisi kwa ajili ya kuendesha shughuli za kila siku za Taasisi kama vile; ulipaji wa mishahara/posho, umeme, maji n.k
  • Technical Assistance Grant: Ruzuku hii inahusiana na kuwajengea uwezo watendaji wa Taasisi, au utoaji wa masaada wa kitaalamu katika utekelezaji wa Mradi.
  • Endowment: Hii ni aina ya ruzuku inayowekezwa ili itoe faida baadae, ambapo; hiyo faida itapaswa kutumika kwa ajili ya programu za Taasisi husika.
  • Challenge: Hii ni aina ya ruzuku inayopatikana kwa sharti kwamba muombaji anapaswa kwanza kuwa na kiasi fulani cha ruzuku kutoka kwenye vyanzo vingine.
  • Matching: Hii ni aina ya ruzuku inayotolewa kwa ajili ya kujaziliza ruzuku itakayotolewa na wafadhili wengine.
  • Demonstration: Hii ni aina ya ruzuku inayotolewa kwa ajili ya mradi ambao; endapo utafanikiwa kwenye utekelezaji, basi utakuwa mfano wa kuigwa.
  • Start Ups: Hii ni aina ya ruzuku inayotolewa kwa ajili ya kufadhili mradi mpya au Taasisi mpya.
Upatikanaji wa ruzuku unategemea na mazingira unayoombea;
1. Ikiwa unaomba as an individual; Mara nyingi "Start Ups Grant" kwa jina jingine "seed grants" hufadhili miradi ya mtu mmoja mmoja. Na miradi inayopata ufadhili sana ni ile inayokuja na suluhisho juu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii, pia iwe miradi ambayo itakuwa kwa haraka (The built projects or companies are to grow fast)

2. Ikiwa unaomba as an organization; aina nyingi za ruzuku kama nilivyoainisha hapo juu zinaelekezwa kwa Taasisi, ni jukumu lako kuzingatia masharti, vigezo na utaratibu unaotolewa na mfadhili husika kuomba fedha.

Ahsante.
 
Ndio, unaweza kupata "fund" kwa ajili ya kutekeleza mradi wako.
Kabla ya kuendelea kujibu swali lako, ningependa kukufahamisha kwanza aina za ruzuku ambazo unaweza kuomba, ambazo ni;
  • Capital Grant: hii ni ruzuku inayoombwa na Taasisi kwa ajili ya ukarabati au ujenzi wa mioundombinu ya Taasisi kama vile jego la ofisi n.k
  • General Operating Grant: Hii ni ruzuku inayoombwa na Taasisi kwa ajili ya kuendesha shughuli za kila siku za Taasisi kama vile; ulipaji wa mishahara/posho, umeme, maji n.k
  • Technical Assistance Grant: Ruzuku hii inahusiana na kuwajengea uwezo watendaji wa Taasisi, au utoaji wa masaada wa kitaalamu katika utekelezaji wa Mradi.
  • Endowment: Hii ni aina ya ruzuku inayowekezwa ili itoe faida baadae, ambapo; hiyo faida itapaswa kutumika kwa ajili ya programu za Taasisi husika.
  • Challenge: Hii ni aina ya ruzuku inayopatikana kwa sharti kwamba muombaji anapaswa kwanza kuwa na kiasi fulani cha ruzuku kutoka kwenye vyanzo vingine.
  • Matching: Hii ni aina ya ruzuku inayotolewa kwa ajili ya kujaziliza ruzuku itakayotolewa na wafadhili wengine.
  • Demonstration: Hii ni aina ya ruzuku inayotolewa kwa ajili ya mradi ambao; endapo utafanikiwa kwenye utekelezaji, basi utakuwa mfano wa kuigwa.
  • Start Ups: Hii ni aina ya ruzuku inayotolewa kwa ajili ya kufadhili mradi mpya au Taasisi mpya.
Upatikanaji wa ruzuku unategemea na mazingira unayoombea;
1. Ikiwa unaomba as an individual; Mara nyingi "Start Ups Grant" kwa jina jingine "seed grants" hufadhili miradi ya mtu mmoja mmoja. Na miradi inayopata ufadhili sana ni ile inayokuja na suluhisho juu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii, pia iwe miradi ambayo itakuwa kwa haraka (The built projects or companies are to grow fast)

2. Ikiwa unaomba as an organization; aina nyingi za ruzuku kama nilivyoainisha hapo juu zinaelekezwa kwa Taasisi, ni jukumu lako kuzingatia masharti, vigezo na utaratibu unaotolewa na mfadhili husika kuomba fedha.

Ahsante.
Okay nmeelewa Na je watu ambao wana idea lakini hawana ujuzi wa how to get izo grant inakuaje meaning unampataje mfadhili especially wa big projects
 
Back
Top Bottom