Unatumia njia zipi kuboresha uhusiano wako?

Unatumia njia zipi kuboresha uhusiano wako?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kudumu kwa mahusiano kunategemeana na juhudi za pande zote mbili (mwanamke na mwanaume); na iwapo upande mmoja utalemaa, kuna uwezekano mkubwa kwa mahusiano kuvunjika. Baadhi ya juhudi wanazotumia:-
  • Wapo wanaotumia fedha
  • Wapo wanaokuwa wapole ili mahusiano yadumu
  • Wapo wanaojiongezea mapambo ili waendelee kutamanisha
  • Wapo wanaojiweka safi na kujipiga pamba ili kutamanisha
  • Wapo wanaotumia nguvu zao za ushauri ili kudumisha mahusiano
  • Wapo wanaotumia mitishamba/ndumba/limbwata n.k
  • Wapo wanaotumia elimu yao kama kishawishi kwenye mahusiano
  • Wapo wanaotumia njia za kuwa karibu karibu ili mwingine asiwahi nafasi
  • Wapo wanaotumia ufundi mwingi faragha ili kudumisha uhusiano n.k
Je wewe, unatumia njia zipi katika kuboresha au kudumisha mahusiano?
 
Vyote ulivyotaja vinategemeana

Na kila kimoja kina UMUHIMU wake kutegemea ,mtu,mazingira na mwenza husika

Kamwe
Huwez kitegemea kimoja wapo tu ukafanikiwa kudumisha mahusiano yako.
 
Nampa vizawadi, namsifia kulingana na alivyo, nampa tu hela kidogo na mwisho nampelea motoo Sanaa.....
 
Back
Top Bottom