Unaweza kuoa mke mwenye sura Personal na akakupasua kichwa tuu!

Unaweza kuoa mke mwenye sura Personal na akakupasua kichwa tuu!

Ubaya am uzuri wa kimuonekano kwa upande wako unaupima kwa vigezo gani?

Uzuri kigezo chake kikuu ni mvuto wa macho, kusikia na kunusa. Mtu mwenye mwonekano wa kuvutia huhusishwa na uzuri.

Wapo Watu na viumbe wanaovutia zaidi(Wazuri) kwa kuwatazama, kusikia sauti zao au harufu zao. Huo ndio uzuri.

Mengine ni faraja tuu
 
Inawezekana mkuu , ila kwa sasa mwanamke mzuri ni anae leta wazo la ugali unafikaje mezani mkuu , Figo zikishafeli ata uzuri wa sura huta uona mkuu.

Huo ni uzuri wa kimawazo Mkuu.
Mimi nazungumzia uzuri wa maumbile na mwonekano.

Ugonjwa ni matatizo na haiwezi kuwa excuse ya uzuri.

Ni sawa na useme Mwenye nguvu za kimaumbile na asiye na nguvu. Hizo ni sifa lazima tuwe na tabia ya kukubali ukweli na uhalisia
 
Uzuri kigezo chake kikuu ni mvuto wa macho, kusikia na kunusa. Mtu mwenye mwonekano wa kuvutia huhusishwa na uzuri.

Wapo Watu na viumbe wanaovutia zaidi(Wazuri) kwa kuwatazama, kusikia sauti zao au harufu zao. Huo ndio uzuri.

Mengine ni faraja tuu
Sawa.huo ni mtazamo wako na upande wako.una hakika unachokiita kibaya kinaweza kuwa kibaya kwa mwingine?
Acha hii mitazamo ya kitoto.kila mtu ameumbwa katika namna yake njema.huyu yuko hivi,huyu yuko vile.kila kitu ni chema hakuna ubaya.

Nyie ndo wale hata kichanga kikizaliwa mnakiita kibaya.

Kua na uachie huu upuuzi watoto
 
Huo ni uzuri wa kimawazo Mkuu.
Mimi nazungumzia uzuri wa maumbile na mwonekano.

Ugonjwa ni matatizo na haiwezi kuwa excuse ya uzuri.

Ni sawa na useme Mwenye nguvu za kimaumbile na asiye na nguvu. Hizo ni sifa lazima tuwe na tabia ya kukubali ukweli na uhalisia
Tatzo kila mtu ana jicho lake mkuu sidhani kama kuna uzuri wa General.
 
Sawa.huo ni mtazamo wako na upande wako.una hakika unachokiita kibaya kinaweza kuwa kibaya kwa mwingine?
Acha hii mitazamo ya kitoto.kila mtu ameumbwa katika namna yake njema.huyu yuko hivi,huyu yuko vile.kila kitu ni chema hakuna ubaya.

Nyie ndo wale hata kichanga kikizaliwa mnakiita kibaya.

Kua na uachie huu upuuzi watoto

Hatuzungumzii mtazamo tunazungumzia uhalisia.

Unachojaribu kukieleza hapo ndio upuuzi kwa sababu unaukataa ukweli.
Mungu kila kitu kikiwa chema kulingana na matumizi yake. Lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa katika hivyo vitu vyema kuna vizuri na vîbaya.

Ukishasema kuna kitu kizuri basi elewa umetamka kuwa kuna kitu kibaya. Ukishasema kuna Watu wazuri wa sura basi elewa kuwa umetamka kuna wabaya wa sura.

Ukishasema kuna Watu wenye tabia mbaya elewa automatically umesema kuna wenye tabia nzuri.

Lakini vyote ni vyema kwa sababu vina matumizi.

Ninyi ndio mnaotaka kuleta Unafiki kwa kuukataa Ukweli.

Uache utoto wa kujidanganya, na kuukimbia ukweli.

Wazuri wapo na wabaya wapo. Ila wote ni muhimu kwa sababu kila mmoja anamatumizi yake.
 
Tatzo kila mtu ana jicho lake mkuu sidhani kama kuna uzuri wa General.

Unajaribu kusema hakuna uzuri wala ubaya.

Kitu kizuri ni kizuri tuu.
Na kitu kibaya ni kibaya. Hapa tunazungumzia mvuto.
Wewe unazungumzia kupenda.

Upendo ndio unaweza ukakufanya ukaona kitu kibaya ni kizuri. Na chuki inaweza kukufanya ukaona kitu kizuri ni kibaya.

Ila Akili itakufanya uone kitu kizuri ni kizuri na kibaya ni kibaya.
 
Kwema Wakuu!

Kuna ile kasumba ya wanaume waoga, wasiojiamini wanaosema kuwa, Kuoa Mwanamke mzuri ni sawa na kuwa na shamba la miwa karibu na shule ya Kayumba.

Acheni uoga vijana. Yaani uache kuoa Pisikali imenyooka kisa misemo ya waoga, wasiojiamini au Watu waliokataliwa na warembo. Labda sio mimi.

Ni bora useme wanawake wazuri sio type zako, wewe type zako ni zile za kina Achiduke Kingkong.

Kwa taarifa túu nikuambie unaweza kumchukua Mwanamke unayemuona mbaya au wakawaida na bado akakupasua kichwa mpaka ukakonda na kujiua. Kwani wangapi tunawaona huku mtaani.

Nawapa siri ndogo vijana, kuendeshwa na Mwanamke yeyote iwe ni mzuri au mbaya ni wewe mwenyewe ukitaka. Ni maamuzi yako tuu. Lakini ukiwa mwanaume kikamilifu hata Mwanamke angekuwa mzuri kama malaika hawezi kuendesha.

Huyo anayekuendesha akikushinda tuletee sisi tukufundishe namna ya kudili naye. Elewa pia kuwa huyo anayekuendesha akikutana na vyuma kama sisi anajilambalamba na kugeuzageuza macho kwa aibu na kujifaragua.

Kuwa Mwanaume, acha kudekadeka kama mtoto wa kike. Mwanamke ukimdekea anakubandua na kunyoosha kwa upuuzi wako.

Usiwe na shida sana na Mwanamke akijaribu kutikisa kibiriti kama kimejaa muonyeshe wewe haujaribiwi. Akitaka kuondoka mpe mkono wa kwa Kheri.

Onyesha kuwa wewe ni mwanaume bora na ambaye wanawake wenye nguvu wanakutafuta kwa udi na uvumba.
Sio kwa kumtambia au kumnyanyasa, nop! Bali kwa sifa kamili za mwanaume.

Yaani uache kuoa Mwanamke mzuri ambaye unavutiwa naye kisa unasikiliza maneno ya waoga. Ati ooh! Mwanamke mzuri anatongozwa sana. Sasa ulitaka uoe Mwanamke ambaye hatongozwi?

Mimi siwezi kuoa Mwanamke ambaye hajanyooka. Raha ya Mwanamke iwe mashine iliyosomwa mpaka dunia ikuone wewe kweli mwanaume.

Unaogopa Wanaume wenzako kuwa watakuchukulia Mke? Hivi huo woga wa kipuuzi mmeutolea wapi? Hujiamini bablai.

Ni sawa na mtu ati uache kujenga majumba mazuri au kuishi vizuri ati kisa unaogopa kulogwa. Hivi hizo akili huwaga mnazitolea wapi?

Mimi nakuagiza sasa, tafuta chuma kikali, mtoto mzuriii, akitembea Watu wanaacha shughuli zao. Kisha weka ndani. Kula vitu vizuri. Achana na kasumba za kijinga hapa.

Akiku-cheat unaachana naye, unatafuta chuma kingine kikali kilichonyooka. Yaani mpaka wakwanza akupigie simu akuamkie shikamoo. Hakikisha mnakuwa na watoto. Usiwe mjinga mjinga.

Acha kujidharau. Wewe pia unastahili kula vitu vizuri.

Maisha yako ni vile unavyojiona na kujifikiria. Ukijiona haustahili kula vizuri utaishia kuona vizuri vinawenyewe ambao ni sisi.

Kabla hujafa kula maisha Boya wewe. Tembea na Pisikali za aina yote. Tafuta wazungu, waarabu, wasomali, waafrika changanya mbele kwa mbele huko. Usiwe umezubaa zubaa.

Mapenzi yatakuumiza ukishaleta mambo ya kutaka kuamulia moyo wa mtu. Muache mtu afanye anachotaka. Pia mjulishe kuwa wewe nawe unafanya kile moyo wako utakavyokutuma.

Oooh! Taikon unapotosha Watu.
Sikupotoshi, nakuambia ukweli. Ukiishi unavyotaka kuna mambo hayawezi kukusumbua hasa mambo madogo. Ilimradi kuvunjika sheria za nchi.

Mtu anaogopa kuoa mke mzuri alafu akioa sura Personal anaogopa kuongozana na mkewe hata barabarani, sasa hiyo ni akili. Mtu anaogopa hata kumtambulisha mkewe kisa ujinga.

Kuoa sura Personal haimaanishi ati ndio hautaendeshwa na Mwanamke kama unaroho dhaifu. Yaani wewe sio mwanaume kamili.

Mwanaume kama umeoa, imejitahidi kuhudumia familia lakini haujapata hitaji la familia, kama Mwanamke anamdomo mdomo mwambie aondoke atafute hao anaowaona wanafaa, kisha wewe utatafuta Mwanamke mwingine mzuri zaidi yake.

Yaani Wake wa wenzako wakipita mate yakudondoke Wakati na wewe ulikuwa na nafasi ileile. Jitafakari.

Unaogopa ogopa nini? Ati unaogopa kuchapiwa, yaani kama mwehu. Au unaogopa kuachwa kwani wewe mwanamke. Ukiachwa au ukiacha si unaoa tena na tena na tena. Hakuna limit ya kuoa, nani anakupangia, huyo anayekupangia mwambie akuletee Mwanamke mzuri ambaye mtaendana, hawezi basi akae kwa kutulia.

Nitapiga mtu hapa!

Robert Heriel
Mtibeli
Taikon vipi? Mbona umechafukwa sana leo? Shemeji amekutenda? Pole, na asante kwa nondo.

Mwanaume ni kujiamini. Huwa ninashangaa wanaume wanapoomba samahani kwa wake zao. Eti baby samahani sitachepuka tena. Ilikuwa bahati mbaya. Basi mkewe anavimba kichwa na kufunga begi.

Mara unaenda kwa washenga kuomba msaada wa upatanisho. Hivi wewe ni mwanaume au bwege?

Pamoja Taikon

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Taikon vipi? Mbona umechafukwa sana leo? Shemeji amekutenda? Pole, na asante kwa nondo.

Mwanaume ni kujiamini. Huwa ninashangaa wanaume wanapoomba samahani kwa wake zao. Eti baby samahani sitachepuka tena. Ilikuwa bahati mbaya. Basi mkewe anavimba kichwa na kufunga begi.

Mara unaenda kwa washenga kuomba msaada wa upatanisho. Hivi wewe ni mwanaume au bwege?

Pamoja Taikon

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app

Mimi nashangaa jambo moja. Kuna Watu wanakiri kuwa kuna Watu wazuri alafu muda huohuo wanakataa hakuna Watu Wabaya.

Wanashindwa kuelewa kuwa mpaka useme uzuri ujue umeutofautisha na ubaya
 
Unajaribu kusema hakuna uzuri wala ubaya.

Kitu kizuri ni kizuri tuu.
Na kitu kibaya ni kibaya. Hapa tunazungumzia mvuto.
Wewe unazungumzia kupenda.

Upendo ndio unaweza ukakufanya ukaona kitu kibaya ni kizuri. Na chuki inaweza kukufanya ukaona kitu kizuri ni kibaya.

Akili itakufanya uone kitu kizuri ni kizuri na kibaya ni kibaya.
Ni kwel kabisa mkuu , naunga hoja yako 💯%
 
Ni kwel kabisa mkuu , naunga hoja yako 💯%

Ukiambiwa utaje ndege wazuri sio ajabu Watu wengi duniani wakamtaja Tausi na njiwa.
Lakini ni nadra sana kusikia mtu akikutajia bundi.

Haya tukirudi kwenye jamii moja. Kwa mfano kwenye Kuku.
Yapo majogoo mazuri ukiyatazama hivi unasema hili jogoo ni zuri sana.

Lakini ukija kwa binadamu Watu wanaogopa kusema ukweli kwa sababu fulanifulani, ikiwemo kutokuumiza hisia za wale wenye muonekano usiovutia(ambapo maana yake ni wabaya).

Ni kweli kila kitu ni chema kwa sababu kinamatumizi yake.

Mfano Watu wenye sura za kazi Wana role zao hasa role za mamlaka, jeshini, utawala, kutisha na kutiisha jambo.

Lakini huwezi kumleta mtu mwenye sura ya kazi ati awe mshehereshaji au shughuli za fasheni, huo ni uongo.
 
Ukiambiwa utaje ndege wazuri sio ajabu Watu wengi duniani wakamtaja Tausi na njiwa.
Lakini ni nadra sana kusikia mtu akikutajia bundi.

Haya tukirudi kwenye jamii moja. Kwa mfano kwenye Kuku.
Yapo majogoo mazuri ukiyatazama hivi unasema hili jogoo ni zuri sana.

Lakini ukija kwa binadamu Watu wanaogopa kusema ukweli kwa sababu fulanifulani, ikiwemo kutokuumiza hisia za wale wenye muonekano usiovutia(ambapo maana yake ni wabaya).

Ni kweli kila kitu ni chema kwa sababu kinamatumizi yake.

Mfano Watu wenye sura za kazi Wana role zao hasa role za mamlaka, jeshini, utawala, kutisha na kutiisha jambo.

Lakini huwezi kumleta mtu mwenye sura ya kazi ati awe mshehereshaji au shughuli za fasheni, huo ni uongo.
Hii ni kwel kabisa mkuu, kutokuumiza hisia za mwengne ata kama kuna ukweli ni hekima kubwa sana.
 
Hii ni kwel kabisa mkuu, kutokuumiza hisia za mwengne ata kama kuna ukweli ni hekima kubwa sana.

Na hakuna hiyo sababu.
Ila ni vizuri kila mtu kujitambua na kujikubali jinsi alivyo.
Unaweza usiwe mzuri kwenye mvuto wa kimapenzi na kingono lakini ukawa nzuri kwenye sekta zingine kama utafutaji wa mali na biashara.
 
Na hakuna hiyo sababu.
Ila ni vizuri kila mtu kujitambua na kujikubali jinsi alivyo.
Unaweza usiwe mzuri kwenye mvuto wa kimapenzi na kingono lakini ukawa nzuri kwenye sekta zingine kama utafutaji wa mali na biashara.
Sure mkuu.
 
Katika macho yangu haya ya nyama bado sijafanikiwa kuona mwanamke mbaya wa sura , ukiona nimesema wapo wabaya ni
kufuata mkumbo tu .

HAYA MAMBO YAPO KIMTINDO SANA UNAWEZA KUONA UNA MWANAMKE MZURI ILA MBELE YA MACHO YA MWINGNE NI WAKAWAIDA SANA.
Beauty falls in the eyes of the beholder
 
Mkuu huu Uzi ungenoga zaidi Kama ungeambatanisha na kapicha,ila bado hakujaharibika Jambo.
 
Hahahaaaaaa..Yaan tuna tabia za kufanana..Nakukubali sana kaka angu..Big u..
 
Back
Top Bottom