Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mimi nimeona 'makahaba wake za watu '
halafu mnasema wake za watu sumu
kumbe na makahaba wake za watu wapo?
Sasa hapo anataka tumshauri nini? Kuwa aendelee kuvumilia?
Angekuwa mdogo wangu Hutu ningemtandika makofi tu, yangemsaidia. Na alihang on wakati kuna hela, sasa kijogoo pori kimekuwa muflisi huh? Kweli akili za like, kha!
i
copy naona uko mbioni haswa hata mchaka chaka wakati mwingine unapumzika kuhema ukiwa unafanya hilo pumzika hapa japo kwa one line
si jambo la busara wasambaratike mwisho wa siku watoto wanaitaji kuwa na wazazi
asante sana nice day
Nikiliangalia hili tatizo kwa jicho la tatu ni hivi. Naanza na maswali
1. Kwa nini ameamua kushughulikia tatizo la mumewe sasa hivi? Why now? Kwa kuwa amefulia?
2. Je huyo jamaa alimuoa binti akiwa na pesa au alikuwa arosto/wa kawaida by then...?maana kama ulivyosema ndoa ina miaka mitano ni more likely dada pesa alizikuta.
3. Na kama alizikuta je mapenzi yalikuwepo au ndio wale wale wanaofuata mali kwa wanaume...? mwanaume alikuwa na pesa na mdada alikuwa mzuri kama ulivyosema hivyo kaka alipata kitu murua sababu ya pesa yake na wala si penzi.
4. Je nitakuwa wrong niki conclude kuwa huyu dada aliamua kuvumilia kwa kuwa alifata pesa toka kwa jamaa...? Sasa pesa imeisha anaanza kuona kuwa ni player wakati alikuwa hivyo toka nyuma na hakuchukua maamuzi yeyote magumu...na kama alimuoa akiwa player hapo hata suala la kuchukua maamuzi by then was irrelevant.
Why now that the guy is poor? Mwambie amvumilie kidogo pesa zikirudi ndio amuache kwani jamii haitamuelewa since kama ni tabia ya umalaya jamaa hakuanza leo wala ya jana...Why take action now?
Ndugu telitaibi huyo mwanamke aliolewa na huyo mwanaume kwa mapenzi ya dhati au kulikuwa ma msukumo fulani kama shinikizo la wazazi, mwanamke kubeba mimba n.k? Kuoa ni kitu kingine na kuwa na furaha ni kitu kingine; inawezekana kabisa huyo mwanamke siyo
chachu ya furaha kwa mwanaume hasa baada ya miangaiko ya kutwa nzima.
kwa hiyo telitaibi aendelee kukaa hapo kwenye ndoa na hayo manyanyaso yote halafu mume amletee ukimwi mwisho wa siku wafe wote?!wakishakufa nani atalea watoto?ni bora aangalie maisha yake na wanawe huyo mume atamuua jamani khaa!
hi, tusaidiane kuona namna ya kumsaidia mwanake mwenzetu na maisha haya ya familia yake, ana umri wa miaka 28 tu dada huyu ana watoto 2 ndoa yao ina miaka 5 mume ana umri wa miaka 33 tu, ni kijana msomi mzuri na aliyekuwa na maendeleo makubwa ya maisha kwa miaka 2 tu alimiliki magari 3 na nyumba kubwa 2 sasa hapo ndo balaa akajiona ndo dume la mtaa mke wa mtu asipite na kashida anapewa pesa na kulipa ngono mtaa mzima wauza bar twende makahaba wa mtaa twende sasa mambo yamekuwa kinyume magari 3 mpaka mguu hakuna kazi viwanja ni magenge ya wanawake wauza pombe awadanganye na vijipesa vya kodi
mke amekonda mawazo miaka yote analia apewe pesa afanye biashara kwa mumewe ni kama kumpandisha matapishi hampi chochote na mazalaliko yote ya mtaa mahitaji ya kawaida atajua mwenyewe mama ni mzuri mrembo mchapa kazi akaanza kupika popcon mara mandazi keki ajipatie matumizi kujiunga na vikundi vya mtaani ajipatie mikopo na vibati hadi leo ameshaweza kuchukua mkopo wa ml 3 na anakaribia kumaliza apate mkubwa zaidi ni mrembo anatongozwa jibu hatajiuza kwa pesa maisha kwani hayo ya wengine mpaka marafiki zake wameharibu maisha yao na asingependa amtende mwanamke mwingine anajua garama ya uchungu wake.
hadi sasa mume hashikiki kidogo kilichopo na barabarani wtoto hawaishi maisha ya kama dad ni mdogo na ni kijana tena msomi wale wa ilboru sec enzi hizo sikuku ya kuzaliwa wtoto yapita kama j4 vile sikuku wtt hawajui nguo wala zawadi hata muuza karanga za kubeba huvalisha wanae na wakajisikia kupendwa sana si hayo tu jamani pombe akirudi piga mke matusi ngoe nywele na hayo yote watoto wanaona na kulia wakisema mwache mama dad jamani anamvua nguo na kumfanyia ukatili akiita vijana wa kufagia nje waje kumuona mama matiti wazi usiku na mchana nikikumbuka haya nasisimuka na kumwambia MUNGU nini hatima ya mama huyu na watoto na haki ya ndoa hii hadi leo anamtimizia mume wajibu wake kama kawaida na mateso yote anacholia ni UGONJWA je? na mume ndo huyo akifa hatima ya watoto itakuwa vipi je atawezaje kuwasaidia watoto wasahau unyama na bado unaendelea watoto watakua watu gani na wanajifunza nini?nu huyu mume elimu yake ya mavyuo ndo hapo mwisho wa kutumia akili mimi nimeweza msaidia na hili tu amuombe tena sana na kutafuta watu ambao mume wake anawaheshimu tenaa wenye elimu na umri zaidi wamkalishe jamaa chini kama atasikia wewe unasenaje una mahali pa kumpeleka mama huyu asaidike hata kama ni kisheria na watoto hawa ndo chooooooooooooozi ziiiiiitooooooooo karibu na samahani usingizi koma na mengine hayakupata nafasi karibu sana nani anapinga ukatili nani anapambania haki za hawa wtoto ndo taifa la kesho saidia jamani nitafikisha na mambo yakiwa shwari nitarudi kuwashukuru si hadithi hadi leo wanalala na maisha haya na wataamkia tukichelewa kusaidia wapi kongosho, Mr Rocky,sweetlady,na wengine karibuni sana
Thanks dearest kwa kuitikia wito wangu; nilijua mawazo yako yatamsaidia kupata informed choices, who knows huenda naye uvumilivu (of course kwa msaada wa sala) waweza msaidia.yaani Kaunga ulivyoniita imebidi niache wadudu wangu nikukimbilie kwanza. haya ma sweet friend nimefika ngoja nimsome subiria nyanga tu.