Shukurani kwa kuuleta usomi huu wa historia katika lugha ya Kiswahili.
Kuna mjadala mkubwa kwa wanahistoria kujadili kama mauaji haya ndiyo yalisababisha vita vikuu vya kwanza, au yalikuwa ni catalyst tu iliyofanya chain reaction ianze mapema.
Kwa vyovyote, mauaji haya yalikuwa sehemu muhimu katika kuanza kwa Vita Vikuu vya kwanza vya dunua. Inawezekana kabisa.
Mauaji haya yasingetokea.
1. Vita vikuu vya kwanza visingetokea, au visingetokea kama vilivyotokea.
2. Mapinduzi ya Kibolsheviki Urusi yasingetokea, au yasingetokea kama yalivyotokea.
3. Kwa sababu Vita Vikuu vya Pili mwanzo wake uliendana sana na matokeo na mijataba ya Vita Vikuu vya Kwanza, basi kama Vita VikuuVya Kwanza visingetokea au visingetokea kama vilivyotokea, vya pili visingetokea au visingetokea kama vilivyotokea.
4. Kwa sababu wimbi la makoloni kudai Uhuru lilikuja baada ya matokeo ya Vita Vikuu vya Pili vya dunia (kisiasa na kiuchumi zaidi) i gewezekana kabisa kwamba bila ya Vita hizi kupiganwa, nchi nyingi za Aftika zingekuwa makoloni ya wazungu kwa miaka mingi zaidi ya ilivyokuwa. Wazungu waliona kuna matatizo ya gharama nyingi za kuendesha makoloni baada ya vita, na Waafrika wengi wakaamka kuona wazungu wanapigika baada ya vita, mambo haya mawili yalipangana vizuri jufanya wazungu wayaoe makoloni uhuru wa bendera huku wakijipanga kuyaendesha kwa mbali kutumia ukoloni mamboleo.
Kifupi, bila mauaji haya, dunia ingeweza kuwa tofauti sana leo.