Mr the dragon
JF-Expert Member
- Apr 14, 2017
- 1,937
- 3,718
- Thread starter
-
- #41
Yap advance nilisomaga HGL mkuu.kwa hiyo haya mambo tulikuwa tunachezacheza nayo sana.Mia mkuuJamaa history ulipiga fresh coz unashusha nondo kama ilivyo na watu tunakuelewa big up.
Hoji kwanza ,amefika la ngapi?Mkuu labda umeelewa tofaut hii sarajevo assasination ni point maarufu ya causes of first world war.waliosoma history form four wanaijuavizuri
Ndo msingi wa title
Haya mauaji yaliwapa wababe sababu ya kutangaza vita ila watu walishajiandaa kitambo.Ferdnand alitumwa makusudi aende Bosnia na Mazayuni hayo hayo yakawa tuma wale vijana wamuue ili vita itokeeShukurani kwa kuuleta usomi huu wa historia katika lugha ya Kiswahili.
Kuna mjadala mkubwa kwa wanahistoria kujadili kama mauaji haya ndiyo yalisababisha vita vikuu vya kwanza, au yalikuwa ni catalyst tu iliyofanya chain reaction ianze mapema.
Kwa vyovyote, mauaji haya yalikuwa sehemu muhimu katika kuanza kwa Vita Vikuu vya kwanza vya dunua. Inawezekana kabisa.
Mauaji haya yasingetokea.
1. Vita vikuu vya kwanza visingetokea, au visingetokea kama vilivyotokea.
2. Mapinduzi ya Kibolsheviki Urusi yasingetokea, au yasingetokea kama yalivyotokea.
3. Kwa sababu Vita Vikuu vya Pili mwanzo wake uliendana sana na matokeo na mijataba ya Vita Vikuu vya Kwanza, basi kama Vita VikuuVya Kwanza visingetokea au visingetokea kama vilivyotokea, vya pili visingetokea au visingetokea kama vilivyotokea.
4. Kwa sababu wimbi la makoloni kudai Uhuru lilikuja baada ya matokeo ya Vita Vikuu vya Pili vya dunia (kisiasa na kiuchumi zaidi) i gewezekana kabisa kwamba bila ya Vita hizi kupiganwa, nchi nyingi za Aftika zingekuwa makoloni ya wazungu kwa miaka mingi zaidi ya ilivyokuwa. Wazungu waliona kuna matatizo ya gharama nyingi za kuendesha makoloni baada ya vita, na Waafrika wengi wakaamka kuona wazungu wanapigika baada ya vita, mambo haya mawili yalipangana vizuri jufanya wazungu wayaoe makoloni uhuru wa bendera huku wakijipanga kuyaendesha kwa mbali kutumia ukoloni mamboleo.
Kifupi, bila mauaji haya, dunia ingeweza kuwa tofauti sana leo.
Wafeli wao tu....hahahaaaSafi sana hii... Umewasaidia kidato cha sita
Achana naye hajasoma hisotory huyo,labda alikomaa na machemikoo tu.Hatuachie sisi wazee wa mafuvu tufurahie huondo.Asante sana mkuu umenikumbusha enzi hizo.Mkuu labda umeelewa tofaut hii sarajevo assasination ni point maarufu ya causes of first world war.waliosoma history form four wanaijuavizuri
Ndo msingi wa title
Hahahaaa huyo atakuwa mzee wa makemiko kweliiiAchana naye hajasoma hisotory huyo,labda alikomaa na machemikoo tu.Hatuachie sisi wazee wa mafuvu tufurahie huondo.Asante sana mkuu umenikumbusha enzi hizo.
Umeelezea vzur sana,ongera sanaHii pekee haikuwa sababu ya kuwepo kwa vita vya dunia ila ilikuwa kama kichocheo cha kuanza kwa vita.Kwa ufupi ipo hivi
Kipindi hicho nchi za ulaya zilikuwa katika migogoro mikubwa sana.Mfano Ufaransa alikuwa na mgogoro na Ujerumani kwa sababu Ujerumani aliishinda Ufaransa katika vita ya Franco-Prussian war mwaka 1870 na Ufaransa kunyang'anywa makoloni yake mhimu ya Alsace na Lorraine.
Lakini kibaya zaidi kulikuwa na miungano ya majeshi(millitary alliances) ya nchi mbali mbali.Kulikuwa na Tripple entente ya Uingreza,Ufaransa na Urusi.Vilevile Tripple alliance iliyohusisha Ujerumani,Italia na Austria-hungary.Hili lilikoleza moto zaidi.
Kumbuka Archiduke alitokea familia ya kifalme na alitegemewa kuwa mtawala wa Austria-hungary baada ya kifo cha Franz Joseph.Hivyo kifo chake kiliikasirisha Austria-hungary wakaanzisha vita dhidi ya Serbia wakidai serikali ilihusika kumuua.Kwa sababu Austria-hungary alikuwa katika umoja wa majeshi na Ujerumani ikabidi Ujerumani aje kumsaidia Austria-Hungary.Kitendo hicho kiliikasirisha Urusi ikaona Serbia inaonewa nayo ikaamua kuisaidia Serbia.Kama nilivyokuambia mwanzoni juu ya ugomvi uliokuwepo kati ya Ufaransa na Ujerumani.Hivyo Ufaransa akaona ndiyo fursa pekee ya kulipiza kisasi na kurudisha makoloni naye akaingilia vita akiwa upande wa Serbia na Urusi.Kumbuka Uingereza naye alikuwa kwenye muungano wa kijeshi na Ufaransa na Urusi hivyo nae hakukaa mbali akaamua kuwasaidia wa upande wake.hivyo ndivyo vita ilivyoanza na ndio tukio hili lilivyochochea.
Yaa,alutakiwa aonesha na Altimatum ya Austeo Hungary kwa Serbia.Mtoa post hii uliyoeleza sio point iliyosababisha vita, umetoa tu historia ya kifo cha mtu tu. Hujaeleza jinsi gani kuuawa kwake kumeleta vita.
Soma comment no 30Mtoa post hii uliyoeleza sio point iliyosababisha vita, umetoa tu historia ya kifo cha mtu tu. Hujaeleza jinsi gani kuuawa kwake kumeleta vita.
Lengo langu nilikuwa najaribu ku trace back background mpaka Archiduke Ferdinand anapigwa risasi.Maana wengi wanajua tu alipigwa risasi ila hawajui yaliyokua yanaendelea.Yaa,alutakiwa aonesha na Altimatum ya Austeo Hungary kwa Serbia.
Ni kiapo cha uzalendo alichotoka nacho kwao. Hata Wajapan, walikua na mbinu ya Kamikaze, unajiua katikati ya naadui huku ukiwadhuru wao kwa wingi. Ni kama wafanyavyo magaidi wanajilipua Iraki, Afghanistani na SyriaMmh . Sioni point hapo yaani wewe umuue adui halafu na wewe ujiue? Unafaidika nini sasa?
Kwa kukusaidia, mgogoro ambao ungepelekea vita ulikuepo na ulikua unafukuta tayari chini kwa chini kama mwandishi alivyoandika. Haya mauaji yaliharakisha tu mwanzo wa vita.Mwandishi asante kwa andiko lako japo hujasema ni kwa nini vita ya dunia ianze kwa sababu ya kifo cha huyo jamaa na mkewe. Washirika wa hiyo vita wanahusiana vipi na marehemu Franz?
Sababu kuu ni kwamba vita hivi vilibeba wanajeshi na rasilimali zingine kutoka almost mabara yote ambayo yalitawaliwa na Waingereza, Wajerumani, Wareno, Wafaransa nk. Makaburi ya wanajeshi walioshiriki vita hizi kwa Dar yapo pale Upanga, opposite na Redcross kama unatoka city centre kuelekea Selander.Mkuu kwanini ziitwe vita ya dunia wakati zimepiganwa na wazungu peke yao??? Huko america ya kusini hta haikurushwa risasi au ndio wazungu wanatuburuza
Usiombe ruhusa kiongozi, we tiririka tu ili tuchote elimu ya historia ya Ulaya hapa. Watu tunafika Serbia na Montenegro bila viza wala malipo. TiririkaMkuu Mr the dragon unaniruhusu kuchangia hii mada ???
Mkuu Mr the dragon unaniruhusu kuchangia hii mada ???
Karibu sana ML, mimi nimejazia kidogo hapo juu.