Kingsmann
JF-Expert Member
- Oct 4, 2018
- 4,805
- 17,850
Manguli wa ndondi kutoka Urusi, Artur Beterbiev na Dmitry Bivol watakutana usiku wa leo (Saa 01:15, Jumapili) katika pambano lisilopingika (Undisputed) la Uzani Mwepesi (Light Heavyweight) mjini Riyadh, Saudi Arabia siku ya Jumapili.
Ikumbukwe kila mmoja hajawahi kupoteza pambano hata moja, huku Beterbiev akiwa ameshinda mapambano yake yote 20 kwa KO.
Ni pambano la kwanza lisilopingika (Undisputed) la ubingwa wa Uzani Mwepesi tangu 2002 na itakuwa mara ya kwanza mataji yote manne makubwa ya Ubingwa wa Dunia kushindaniwa katika zama hizi za mikanda minne (WBO, WBA, IBF na WBC).
Ikumbukwe kila mmoja hajawahi kupoteza pambano hata moja, huku Beterbiev akiwa ameshinda mapambano yake yote 20 kwa KO.
Ni pambano la kwanza lisilopingika (Undisputed) la ubingwa wa Uzani Mwepesi tangu 2002 na itakuwa mara ya kwanza mataji yote manne makubwa ya Ubingwa wa Dunia kushindaniwa katika zama hizi za mikanda minne (WBO, WBA, IBF na WBC).
Mikanda (Belts) Inayoshindaniwa.
Kwa mara ya kwanza katika zama za kisasa, mikanda yote minne ya Uzani Mwepesi itakuwa kwenye kushindaniwa - WBO, WBA, IBF na WBC.
Beterbiev ana umiliki wa mataji ya WBO, WBC na IBF, huku Bivol ataleta mkanda wake wa WBA kwenye mlinganyo huo.
Bingwa wa mara ya mwisho asiyepingika wa Uzani Mwepesi alikuwa Mmarekani Roy Jones Jr baada ya kumshinda mwenzake Reggie Johnson, lakini hiyo ilikuwa wakati wa zama za mikanda mitatu.
Beterbiev ana umiliki wa mataji ya WBO, WBC na IBF, huku Bivol ataleta mkanda wake wa WBA kwenye mlinganyo huo.
Bingwa wa mara ya mwisho asiyepingika wa Uzani Mwepesi alikuwa Mmarekani Roy Jones Jr baada ya kumshinda mwenzake Reggie Johnson, lakini hiyo ilikuwa wakati wa zama za mikanda mitatu.
Rekodi za Beterbiev na Bivol.
Beterbiev, mwenye umri wa miaka 39, ana umri wa miaka sita zaidi Bivol lakini amepigana mara tatu chache zaidi.
Pambano lao lilikuwa liwe tarehe 1 Juni lakini Beterbiev alilazimika kujiondoa baada ya kupata jeraha la goti katika mazoezi.
Wapiganaji wote wawili wanajivunia rekodi za kutoshindwa wakiwa na ushindi wa KO 32 kwa pamoja katika mashindano 43.
Beterbiev, ambaye alishiriki kama mchezaji wa Uzani Mzito kwenye Michezo ya Olimpiki ya 2012 huko London, ameshinda mapambano yake yote 20 kwa KO, hivyo kuwa bingwa pekee wa sasa wa ulimwengu kuwa na uwiano wa asilimia 100 wa KO.
Alianza kuwa bingwa wa dunia mwaka 2017 alipomshinda Enrico Kolling na kutwaa mkanda wa IBF wa Uzani Mwepesi.
Beterbiev alishinda mkanda wa WBC mnamo mwaka 2019 baada ya kumchabanga Oleksandr Gvozdyk na kuongeza mkanda wa WBO kwa kumchabanga Joe Smith Jr mnamo 2022.
Bivol alianza ndondi mnamo mwaka 2014, mwaka mmoja baada ya Beterbiev, lakini amekuwa akifanya mashindano zaidi kwa miaka 10 iliyopita.
Alishinda taji la muda la WBA katika pambano lake la saba pekee mwaka 2016 na akapandishwa daraja hadi kuwa bingwa mnamo Septemba 2017.
Bivol alipata ushindi wa pointi za kushangaza dhidi ya Saul 'Canelo' Alvarez mnamo mwaka 2022, na kuwa mtu wa pili kufikia mafanikio hayo baada ya Floyd Mayweather.
Ameshinda kwa KO mara 12 kwenye rekodi yake lakini mapambano tisa kati ya 10 ya mwisho ameshinda kwa KO.
Kura ya ushindi unampa nani?
A. Artur Beterbiev
B. Dmitry Bivol
Pambano lao lilikuwa liwe tarehe 1 Juni lakini Beterbiev alilazimika kujiondoa baada ya kupata jeraha la goti katika mazoezi.
Wapiganaji wote wawili wanajivunia rekodi za kutoshindwa wakiwa na ushindi wa KO 32 kwa pamoja katika mashindano 43.
Beterbiev, ambaye alishiriki kama mchezaji wa Uzani Mzito kwenye Michezo ya Olimpiki ya 2012 huko London, ameshinda mapambano yake yote 20 kwa KO, hivyo kuwa bingwa pekee wa sasa wa ulimwengu kuwa na uwiano wa asilimia 100 wa KO.
Alianza kuwa bingwa wa dunia mwaka 2017 alipomshinda Enrico Kolling na kutwaa mkanda wa IBF wa Uzani Mwepesi.
Beterbiev alishinda mkanda wa WBC mnamo mwaka 2019 baada ya kumchabanga Oleksandr Gvozdyk na kuongeza mkanda wa WBO kwa kumchabanga Joe Smith Jr mnamo 2022.
Bivol alianza ndondi mnamo mwaka 2014, mwaka mmoja baada ya Beterbiev, lakini amekuwa akifanya mashindano zaidi kwa miaka 10 iliyopita.
Alishinda taji la muda la WBA katika pambano lake la saba pekee mwaka 2016 na akapandishwa daraja hadi kuwa bingwa mnamo Septemba 2017.
Bivol alipata ushindi wa pointi za kushangaza dhidi ya Saul 'Canelo' Alvarez mnamo mwaka 2022, na kuwa mtu wa pili kufikia mafanikio hayo baada ya Floyd Mayweather.
Ameshinda kwa KO mara 12 kwenye rekodi yake lakini mapambano tisa kati ya 10 ya mwisho ameshinda kwa KO.
Kura ya ushindi unampa nani?
A. Artur Beterbiev
B. Dmitry Bivol