Nas Mapesa
JF-Expert Member
- Jul 31, 2014
- 5,286
- 5,421
We unastahili ban,unaleta story zako za kijingajinga ukfikiri humu ndai kuna mataahira,umetoka kuanzisha thread hukai na mwanamke now unatuletea huu upuuzi.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahahahah! Amesha sahau kama amedumu na bonge kwa miaka 10.We unastahili ban,unaleta story zako za kijingajinga ukfikiri humu ndai kuna mataahira,umetoka kuanzisha thread hukai na mwanamke now unatuletea huu upuuzi.
Kuna aina mbili ya matendo wanayofanya watu wakiwa na stressSasa stress si angekonda stress gani ananenepa
Aasante sana mheshimiwa umenisaidia sana naomba nijue nifanyeje sasaKuna aina mbili ya matendo wanayofanya watu wakiwa na stress
1. Kuna baadhi wanakula sana kwa maana wanapunguza msongo wa mawazo kwa kufanya kitu kinachofawariji bila kujizuia.
2. Kuna baadhi wanashindwa kula kwa sababu ya msongo wa mawazo.
Probably huyu mke wa mdau hapa ana msongo wa mawazo ambao umepelekea kushindwa tena kujizuia baada ya kujenga tabia ya kula kupita kiasi, na huu ukali unaokuja ukigusia mazoezi unaweza uka-justify kilichopo kwenye kichwa chake.
Aasante sana mheshimiwa umenisaidia sana naomba nijue nifanyeje sasa
Mkeo ana stress...
Nilifanikiwa kupata mwenza wa maisha (kuoa) mnamo mwaka 2006 kipindi ninaoa mimi nilikua na uzani wa kilo 50 na wife alikua na kilo 42 maisha yalisonga tukapata mtoto wakwanza. Wife alijifungua normal kabisa na tukalea mtoto wetu wa kwanza wife alikua na kilo 44 mpaka mwanetu anafikisha umri wa miaka mitatu mwaka 2009. Tukafanikiwa kupata mtoto wa pili ambae Mungu si athumani wife alijofungua salama pia na mpaka mwanetu anafikisha miaka mitatu wife alikua na kilo zile zile 44.
Hatujawahi kutumia njia yeyote ya uzazi wa mpango ila mnamo mwaka 2014 wife alianza kunenepa katika kipindi cha mwaka mmoja alitoka kilo 44 mpaka 76. Nilijitahidi kumshawishi japo kwa njia ambayo isinge mkwaza kua tuwe tunakimbia kimbia jioni wife akisikia swala la mazoezi anakua mkali nitanuniwa hata wiki tatu haongei yeye ni ku deal na watoto tu.
Ilipofika mwaka jana mwishoni wife alifikia kilo 95 kuna kipindi alikuwa anappata dalili za pressure tukaenda hospitali daktari alimshauri apunguze weight lakini alimgombeza daktari kama mtoto mdogo kua amuache yeye ni mtu mzima kama kumtibu ameshindwa aseme. Sikuwa na jinsi zaidi ya kua mpole na kupewa baadhi ya vidonge na kurudi nyumbani.
Mwezi uliopita wife amefika kilo 110 ambazo zinazidi kumuweka katika hatari yakupata magonjwa mengine ya hatari zaidi. Ameanza kukoroma kwa sauti kubwa sana usiku na akilala hataki umuamshe hata kama kuna kitu chochote kile amekua mkali sana na hata haki ya ndoa anasema anachoka sana skuizi ananipiga kalenda. Unene wa wife umekua ukinipa uoga na kumuonea mke wangu huruma sana hasa nikiona anapokua akilalamika miguu inamuuma.
Kuna siku nilijaribu kumwambia miguu inakuuma kwasababu ameongezeka uzito katika kipindi kifupi mno, hili lilizua ugomvi mpaka tukaenda kusuluhisha kwa wazazi baada ya miezi miwili ya kuvutiwa mdomo na kukosa amani ndani ya nyumba kwa kumshauri wife jambo la busara tu.
Kwa sasa nina kilo 54 wife anachezea 110 ninaomba ushauri nifanyeje wife anielewe na aweze japo kufanya mazoezi amekua kibonge sana na anapata matatizo ambayo yananiogopesha naweza kumpoteza mama watoto. Nilishawahi kujaribu kumshauri tujiunge kwa pamoja gym hilo ndilo lilizua maneno kuwa ninafuata wanawake huko gym namshangaa wife japo ni msomi ana masters yake ila haoni umuhimu wa afya yake.
Kitu kinachomfanya wife awe hivi ni kula kupita kiasi na kupenda sana vitu vya wanga kuna siku kulikua na birthday ya mwanetu alikula keki ya kilo tatu na ile sukari ya juu yote baada yakuwakatia watoto. Anaweza kutoka kazini akapita mahali akala hata kilo mbili za kitimoto, kuna siku nilimfuma anakula kitimoto bar kwa makadirio kilikua kama kilo 2 nikajaribu kudadisi nikagundua huwa ana desturi yakupita pale kila siku na ameweka oda kabisa na akifika nyumbani pia anafanya majukumu yake vizuri ikiwa ni pamoja na kuwapikia watoto na hula tena mara yapili na kulala akimaliza tu kula.
Ninaombeni ushauri ndugu zangu nifanyeje kunusuru afya ya mke wangu.
chai chungu hii, kama haoni hizi comments, ze big hebu kwanza jibu maswali, hii chai au gahawa, ukiwa muongo uwe na kumbukumbuze big usitufanye watoto wadogo na chai zako mara sikai na mke mara ana kilo 110,amekuwa nguruwe huyo