Ungekuwa na Mamlaka Serikalini, ungefanya nini kuikuza Tanzania kiuchumi bila kumuongezea mzigo mwananchi?

Ungekuwa na Mamlaka Serikalini, ungefanya nini kuikuza Tanzania kiuchumi bila kumuongezea mzigo mwananchi?

Kwanza ningehakikisha raslimali zote za nchi mfano madini, gesi, mbuga za wanyama, mito, maziwa, ardhi yenye rutuba, nk. Zinakuwa na manufaa kwa nchi, badala ya mabeberu!

Nitahakikisha matajiri waubwa kama akina Ahmed Shabiby wanaotaka kila mwananchi kukatwa 2000 kila mwezi kwenye simu kwa ajili ya kufanyia ujinga gani sijui! Wanalipa kodi ipasavyo!

Maana hawa wafanyabiashara wakubwa ndiyo wakwepa kodi wakuu duniani kote huku wakishirikiana na watendaji wasio waaminifu serikalini.

Ningehakikisha nchi inakuwa na sheria kali za kuwabana wala rushwa, wabadhirifu, na wezi wa mali za umma. Yaani ukibainika umeiba, basi suala la kufilisiwa na kufungwa lile ni jambo la kawaida kabisa.

Nitajenga mifumo imara ya kisheria, kiuchumi, kijasusi, kisiasa, nk. ili kuondoa ule utegemezi wa mtu mmoja tu katika nchi. Yaani nitahakikisha kila mwananchi anatimiza wajibu wake.
 
Mazingira na mazuri sana kwa chochote kufanyika humu nchini.....

Ningehamasisha na kusisitiza watu waache uvivu wafanye kazi kwa bidii sana, bila kuchoka wala kukata tamaa hasa kazi za, kilimo, ufugaji na biaashara 🐒
-Kuondosha mazingira ya face to face bargaining, always digital system inaondoa rushwa za kipumbavu, kila kitu kinakuwa kiko katika mfumo maalum, na mambo yote na taratibu zinakuwa fed katika "COUNTRY DIGATAL DATA BASE SYSTEM"
 
Kama ungekuwa na uongozi ngazi za juu, ungekuwa au kuja na mpango au mbinu gani ya kuikuza Tanzania kiuchumi bila kumtwisha mzigo wa kodi au makato mengine mwananchi?

Kumekuwa na mijadala mbalimbali kuhusu mzigo wa kodi au tozo kwa wananchi, huku watu hao wakiwa na hoja ya Tanzania ni nchi iliyobarikiwa rasilimali nyingi sana hiyo zikitumiwa vizuri nchi itakuwa kiuchumi maradufu huku wananchi wakipunguziwa mzigo wa tozo na kodi ambazo zinaonekana kuwaelemea.

Katika kuzingatia hoja hizo ungekuwa wewe una nafasi ya kufanya maamuzi ungefanya jambo gani, mbinu gani au mipango gani ili kutumia rasilimali na fursa zilizopo kuzalisha ili kuongeza pato la Taifa na hivyo Tanzania iweze kupaa kuichumi na wananchi tupate maisha yale ambayo wengi tunayatamani kwa angalau thamani ya fedha yetu iweze kupaa juu.
Nimepitia comments zote na nimeona watu wanataja tu kwamba wangefanya hiki au wangefanya vile bila ya kueleza bayana hayo yote yangefanikiwaje au yatawezaje kuzaa matunda yanayokusudiwa? Je, mmeshawahi kufanya uchunguzi au utafiti kidogo ktk mojawapo ya nchi ambazo zimefanikiwa kuwa na maendeleo makubwa na mazuri kwenye nyanja za uchumi wa nchi?

Ukifanya uchunguzi wa kina kwenye hizo nchi zilizoendelea utagundua kwamba Kitu pekee, cha muhimu kabisa na cha kwanza walichoanza nacho ni Kutengeneza Miongozo Mizuri zaidi ktk nchi juu ya namna watu wote wanavyopaswa kuishi na namna watakavyoenenda kwenye masuala yote yahusuyo maisha yao.

Hapa nazungumzia kuhusu kutunga Katiba nzuri ya nchi, Sheria pamoja na kuwa na Serikali imara kabisa iliyojikita kwenye Mifumo ya Taasisi imara na zilizo madhubuti kabisa. Hii ndio Siri kubwa kabisa ya mafanikio au maendeleo Bora karibia kwenye hizo nchi zote zilizoendelea kiuchumi.
 
1. Ningelibadili mifumo ya ulipaji Kodi, twende digital zaidi
2. Kila wizara ingepata sifa kulingana na juhudi na maarifa ya kazi waifanyayo kulikoni kuwa na chawa wenye kusifia mahala ambapo kazi haitendeki
3. Report bana matumizi ingerudi, manunuzi ya V8 ningeondoa, Prado TXL Zinafaa Sana tu
4. Hata posho cjui n kiinua mgogo Cha wake wenza wa Marais wastaafu ungeondoka tu
5. Kila ataeguswa na report ya CAG, jela na utaifishaji wa Mali zake ingemhusu
Namengine mengi
 
Kwa kifupi bila kufafanua,

1: Kupunguza matumizi ya serikali angalau 30%

2: Wabunge mshaara milion 5 kwa mwezi,Gari Toyota RAV4

3: Hakuta kua Na Wakuu wa Mikoa Wala wakuu wa Wilaya

4: Watakao tajwa kwenye ripoti ya CAG mahojiano watafanya wakiwa UKONGA

5: MAFISADI wapiga deal,vishoka,hakuna kuwachekea
Umetoa mchango mzuri lakini Kuna vitu hujavizingatia; katika suala Zima la kiutawala kwa kila eneo la utawala ni lazima kwa mujibu wa Sheria zetu za nchi kila eneo Liwe na mkuu/kiongozi ili uwepo muunganiko wa Moja kwa Moja kutoka nafasi ya chini ya mgawanyiko wa utawala Hadi juu Yani lazima tuwe na kiongozi wa Kitongoji, Kijiji/mtaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa, na nchi. Ukisema utaondoa wakuu wa mikoa na wilaya maana yake utafuta wilaya na mikoa kwenye hesabu ya maeneo ya kiutawala jambo ambalo sio sawa.
Lakini pia mbunge kulipwa milioni 10 au 20 haiwezi kuwa sababu ya kudidimiza uchumi wa mwananchi endapo tu nchi itakuwa na mikakati imara ya kujipatia mapato na kukuza uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi mkubwa hasa kwa kutoa kipaombele kwenye rasilimali ambazo zitazalisha mapato makubwa na kufanya matumizi muhimu kwa awamu kwa kila mwaka wa husika wa mapato na sio kufanya matumizi vuluvulu bila mpango mfano; Serikali inaweza kesema mwaka huu wa fedha 2024/25 vipaumbe ni mishahara, maji, na pengine ujenzi wa baadhi ya barabara kwenye wilaya Fulani. Ukisema huu mwaka nchi nzima tutaangalia kwenye umeme na maji au elimu na afya naamini utafanikiwa lakini ukitaka yote yafanyike huwezi kuyafanya kwa usahihi ila mishahara ni lazima kila mwaka.
Ni kama nyumbani tu, mwaka mwingine utajenga na mwaka mwingine utao huwezi kufanya yote na kama utaona ni muhimu kufanya yote basi utoe vipaumbele kwa mambo muhimu zaidi kama vyanzo vyako vya mapato vinakuruhusu kufanya hivyo bila kumdidimiza mwananchi ingawa huwezi kukwepa kumtumia mwananchi kwaajili ya kuchangia mapato ya taifa kupitia Kodi na TOZO.
Poa mwanangu.
 
Umetoa mchango mzuri lakini Kuna vitu hujavizingatia; katika suala Zima la kiutawala kwa kila eneo la utawala ni lazima kwa mujibu wa Sheria zetu za nchi kila eneo Liwe na mkuu/kiongozi ili uwepo muunganiko wa Moja kwa Moja kutoka nafasi ya chini ya mgawanyiko wa utawala Hadi juu Yani lazima tuwe na kiongozi wa Kitongoji, Kijiji/mtaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa, na nchi. Ukisema utaondoa wakuu wa mikoa na wilaya maana yake utafuta wilaya na mikoa kwenye hesabu ya maeneo ya kiutawala jambo ambalo sio sawa.
Lakini pia mbunge kulipwa milioni 10 au 20 haiwezi kuwa sababu ya kudidimiza uchumi wa mwananchi endapo tu nchi itakuwa na mikakati imara ya kujipatia mapato na kukuza uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa ufanisi mkubwa hasa kwa kutoa kipaombele kwenye rasilimali ambazo zitazalisha mapato makubwa na kufanya matumizi muhimu kwa awamu kwa kila mwaka wa husika wa mapato na sio kufanya matumizi vuluvulu bila mpango mfano; Serikali inaweza kesema mwaka huu wa fedha 2024/25 vipaumbe ni mishahara, maji, na pengine ujenzi wa baadhi ya barabara kwenye wilaya Fulani. Ukisema huu mwaka nchi nzima tutaangalia kwenye umeme na maji au elimu na afya naamini utafanikiwa lakini ukitaka yote yafanyike huwezi kuyafanya kwa usahihi ila mishahara ni lazima kila mwaka.
Ni kama nyumbani tu, mwaka mwingine utajenga na mwaka mwingine utao huwezi kufanya yote na kama utaona ni muhimu kufanya yote basi utoe vipaumbele kwa mambo muhimu zaidi kama vyanzo vyako vya mapato vinakuruhusu kufanya hivyo bila kumdidimiza mwananchi ingawa huwezi kukwepa kumtumia mwananchi kwaajili ya kuchangia mapato ya taifa kupitia Kodi na TOZO.
Poa mwanangu.
Aiseeeeeeee!
Kwa reasoning capacity ya namma hii inaonyesha kwamba Tanzania bado Ina safari ndefu zaidi ya kwenda ili kuanza kuifikia ndoto ya maendeleo ya kweli.
 
Ningefuta ruzuku Zote Kwa vyama siasa

Punguza bunge liwe dogo Kila mkoa uwe na mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa

Viti maalumu vya wabunge ningefutilia mbali.

Vikao vya bunge ningebipinguza na Siku za kukaa ningepunguza
 
Kuhakikisha tunapata Katiba mpya
 
Aiseeeeeeee!
Kwa reasoning capacity ya namma hii inaonyesha kwamba Tanzania bado Ina safari ndefu zaidi ya kwenda ili kuanza kuifikia ndoto ya maendeleo ya kweli.
Shida watu Huwa wanaamini kwamba mambo ya nchi hasa kwenye suala Zima la utawala kwamba mtu unaweza kujifanyia tu chochote bila kuzingatia kanuni za nchi.
Kila nchi Ina kanuni zake na katika kila mipango ya nchi Ina hatua zake. Nchi nyingi za Afrika Bado zipo kwenye mchakato wa maendeleo kwa hatua Yani kila jambo lipo kwenye mchakato wa hatua kwa hatua. Mfano sisi Tanzania tunaweza kusema tuna rasilimali nyingi ambazo zitakuza uchumi wetu kwa haraka lakini Bado tangu miaka mingi iliyopita hatuna uwezo wa kuziutilize rasilimali zetu kwa kiwango Cha juu mfano tuna madini lakini hatuwezi kuyavuna vizuri kuwa pesa badala yake tunahitaji wawekezaji ambao baadhi Yao malengo Yao ni kutuibia.
Kwahyo tunapojadili ni lazima tujue kwamba Bado tupo kwenye mchakato wa kuendelea kwa hatua. Mfano Bado technology yetu Iko chini na ili tuwe kama wenzetu nchi za ulaya lazima tuwe na technology kubwa kama wao na wao michakato Yao ilifanyika kwa hatua haikufanyika ghafla tu.
Bado tunahitaji nchi yetu isiwe na watu wa uchumi ambao hatazungumza maandishi ya kwenye vitabu vya uchumi bila kuhusisha uhalisia wa nchi husika.

Bado tunapotaka kuzungumza kuhusu mabadiliko ya nchi kiuchumi ni lazima tuzingatie misingi ya nchi kiuchumi, kiutawala na kijamii bila kusahau kwamba mabadiliko yoyote ni lazima yatokane na mabadiliko ya kanuni za nchi.
 
Uwajibikaji tu.

Kila taasisi itafanya kile inasema inafanya. Asiyewajibika anaachishwa kazi tunabakiza wawajibikaji na tunaajiri wapya walioko mtaani. Wasomi wapo wengi tu mbona.

Nikikuta mtaani mambo ya tiba hayaendi vizuri Meneja TMDA atawajibika kuhakikisha muhusika wa eneo hilo amewajibishwa.

Nikikuta bidhaa mbovu mtaani Meneja wa TBS atawajibika kumuwajibisha wachini yake hadi muhusika wa mwisho.

Vivyo hivyo Mazingira
Polisi
Wizara zooote
Kila kitu tulipofeli ni uwajibikaji tu.

Mwizi/mkwepa kodi akikamatwa atawajibikaje kama polisi na mahakama haitawajibika? Lakini atawajibikaje kama mwananchi hatashiriki ulinzi/kodi kwa nafasi yake. Lakini je? Ni nani ataamini kwamba upo uwajibikaji ikiwa tu katiba ina mianya ya kukosekana kwa uwajibikaji?

Yoda alishatuma kipicha hapa ngoja nikitafute;
Screenshot_20240424-074905_X.jpg

Ndivyo inavotakiwa kuwa bhas. Mambo yote yawe kikatiba. Na wote tuwajibike kwa hiyohiyo katiba taratibu na sheria.
 
Back
Top Bottom