Unyanyasaji wa kibinaadamu hasa kwa wezi siyo mzuri

Unyanyasaji wa kibinaadamu hasa kwa wezi siyo mzuri

Mwizi aliniibia simu yangu asubuhi, jioni akakamatwa kaiba Tv, akapigwa sana, akaletwa hospitali, nikiwa ninamshona majeraha aliyepigwa, na mwananchi mmoja akatoa simu yangu iliyoibwa asubuhi akasema na simu yake hii hapa huyu mwizi.

Jamani iliniuma lakini kwa kuwa ni kazi na wito, nikaendelea kutoa huduma. Na badae nikachukua simu yangu.

Tokea pale yule mwizi alipotoka jela baada ya miaka 3 akaja kuniomba msamaha na sasa hivi ndio mjumbe wa mtaa wetu

Amebadilika kabisa. Hawa watu hubadilika.
 
Tulia siku wakijakukutembelea utaisoma. Hata maandiko matakatifu yamesema mwizi huja kwaajili ya kuvunja na kuua. So its a game of timing. Ukimuwai mwue, akikuwai inamisha apake kilainishi usamehewe kifo
 
Mwizi aliniibia simu yangu asubuhi, jion akakamatwa kaiba Tv, akapigwa sana, akaletwa hospital , nikiwa ninamashona majeraha aliyepigwa, na mwananchi mmoja akatoa simu yangu ilioibiwa asubuhi akasema na simu yake hii hapa huyu mwizi.Jaman iliniuma lakin kwa kuwa ni kazi na wito , nikaendelea kutoa huduma .Na badae nikachukua simu yangu.
Tokea pale yule mwizi alipotoka jela baada ya miaka 3 akaja kuniomba msamaha na sasa hivi ndio mjumbe wa mtaa wetu , amebadilika kabisa.Hawa watu hubadilika.
[emoji122][emoji122]
Hii point ndio ambayo Bwana Mungu wa Majeshi atalala nao mbele wauaji wote wa wezi!

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Huwa wanapelekwa mahakamani na hapo watu wengi hawaendi kutoa ushahidi ndio maana wanaachiwa Futuza unadhani ukienda kutoa ushahidi mahakamani, lazima ale mvua hata miaka 3 na itakuwa fundisho.
Ni Bora tuwahukumu mapema ili tusihangaike
 
Bahati yake huyo Kibaka amekufa bila kuliwa kiboga na watu wenye hasira kali.

Wagalatia 6:7-8
Mshahara wa dhambi ni mauti.
 
Ukimkamata mwizi mfikishe kwenye vyombo vya sheria achukuliwe hatua nasio kuchukua sheria mkononi za kumuua hapo tunatengeneza au tunabomoa!
Hata ulaya na nchi zilizoendelea mwizi lazma wampige pipe(bunduki) yote ni Yale Yale tuu, maana atakufa, sema Kwa mwizi wa bongo mpaka uje ufe utafanyiwa ukatili wa Kila namna ila kiujumla wizi ni mbaya kifo kinakuhusu.
 
Habari za asubuhi wana jamii! Hope mko poa na Xmass ilienda good.

Kuna jambo limenitatiza kidogo kuna kijana amekamatwa akiiba nyumbani kwa jirani hapa, ila cha kushangaza badala ya kumpeleka polisi wakamfungulie mashtaka wameishia kumtesa, kumdhalilisha na kumnyanyasa.

Wamekoroga cement na kumlazimisha ainywe mbaya zaidi wamemfunga kamba mikono na kuimwagia petrol kisha wakaichoma moto, jamani sio uungwana hata kidogo hii ni jamii ya namna gani ya kutesa wezi na vyombo vya sheria vipo? Mbona jamii imekuwa na watu katili kiasi hiki?

Tukataeni unyanyasaji wa aina yoyote ile katika jamii zetu. R.I.P kibaka, walimwengu ni makatili sana.
Wewe subiri siku wanavamia kwako afu wakufire mbele ya mkeo na wanao, afu Kwa zarau wanakunyang'anya na kuchukua kwanguvu na kibabe mali ulotafuta Kwa kujibidiisha na Kwa uchungu. Hakika nakuambia utarudi humu kuja kufuta huu Uzi.
 
Shida sio wezi kuuawa shida wengi wanaouliwa sio wezi wanasingiziwa kuna watu mbumbumbu sana wakifika tu wanaanza kupiga.
 
Ulimwengu Ni mwalimu mzur sn kwa kijana alishindikana mwa wazazi wake
 
Uko sahihi mkuu yaani mtu umemkamata kabisa na uzuri CCTV camera zipo kwanini usimpeleke polisi muende mahakamani mkamalizane? Yaani wamempa mateso sana mengine nimeona hata aibu kuyasema hapa. Ila kama jamii tuna la kujifunza na tukubali kuacha huu ukatili kwa namna moja ama nyingine.
Mtoa mada unaongelea polisi ipi? Mahakamani zipi? Za nchi Hii au ?
 
Huwajui wezi vizuri wewe, siku wakikuzingua Utajua hujui na police hutompeleka
 
Omba ukutane na kibaka kazini.afu akute huna kitu huo unyanyasaji utajua vizuri
 
Bora hao wezi wakwenu wanakuibia alaf wanakuacha wezi wa huku kwetu wanakuibia alaf wanakuua, au wanakufunja miguu kisha wanakutegesha kwenye leli ili treni ikija ikusage ufe, wanyama sanaa hao mkuu
 
Habari za asubuhi wana jamii! Hope mko poa na Xmass ilienda good.

Kuna jambo limenitatiza kidogo kuna kijana amekamatwa akiiba nyumbani kwa jirani hapa, ila cha kushangaza badala ya kumpeleka polisi wakamfungulie mashtaka wameishia kumtesa, kumdhalilisha na kumnyanyasa.

Wamekoroga cement na kumlazimisha ainywe mbaya zaidi wamemfunga kamba mikono na kuimwagia petrol kisha wakaichoma moto, jamani sio uungwana hata kidogo hii ni jamii ya namna gani ya kutesa wezi na vyombo vya sheria vipo? Mbona jamii imekuwa na watu katili kiasi hiki?

Tukataeni unyanyasaji wa aina yoyote ile katika jamii zetu. R.I.P kibaka, walimwengu ni makatili sana.
Wananchi wenye hasira ni marafiki wema wa polisi
 
Habari za asubuhi wana jamii! Hope mko poa na Xmass ilienda good.

Kuna jambo limenitatiza kidogo kuna kijana amekamatwa akiiba nyumbani kwa jirani hapa, ila cha kushangaza badala ya kumpeleka polisi wakamfungulie mashtaka wameishia kumtesa, kumdhalilisha na kumnyanyasa.

Wamekoroga cement na kumlazimisha ainywe mbaya zaidi wamemfunga kamba mikono na kuimwagia petrol kisha wakaichoma moto, jamani sio uungwana hata kidogo hii ni jamii ya namna gani ya kutesa wezi na vyombo vya sheria vipo? Mbona jamii imekuwa na watu katili kiasi hiki?

Tukataeni unyanyasaji wa aina yoyote ile katika jamii zetu. R.I.P kibaka, walimwengu ni makatili sana.
Jamii ina makatili sana na moja wapo ni hao wezi... Imagine umenunua tv unajikusanya ununue na king'amuzi kabla hata hujaiwasha anapita nayo kama ya kwake.
 
Back
Top Bottom