Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Uongo mkubwa zaidi kutokea dunia - The biggest scam in the world

Kwhyo ww unawawmini hao wwwnasayans wako wanaokuandikia vitabu kusoma na kupaste ya mungu uyaamini unasmini ya mzungu akiri fup San na hao wanaokusupport wewe usiamini ss tunaamini endelea kuamini wachawi na wazungu

Uandishi wako tu unaonyesha haya mambo ni zaidi ya upeo wa ufahamu wako mkuu [emoji120]
 
Upo sahihi, mambo ya ufunuo tunajifunza kwenye THIOLOJIA na si SAYANSI. So hilo waachie waliobobea THEOLOGY na si SCIENCE

Ndio tunasema huko kwenye thiolojia mnajazana ujinga
Na ndio the biggest scam ever

Mwanasayansi anatengeneza vitu vinavyosaidia maisha yetu ya kila siku

Wanatheojia wapo busy Mungu gani ndio sahihi na wakweli
 
Science never claims can solve everything

...... NOT IN SCIENCE
Wana JF naomba tufahamu kwamba

Sayansi kimantiki haiungi mkono ukana MUNGU, hoja za wakana MUNGU hazijamea kutoka kwenye sayansi bali katika falsafa (positivism philosophy of knowing approach) na saikolojia , hivyo mkana MUNGU yeyote anayejifanya kutumia hoja za kisayansi kupinga uwepo wa MUNGU ni JUHA nduguye KILAZA, hamna hoja ya kisayansi hata moja inayosadikisha madai yao; sayansi haishughuliki na metafizikia, maadili wala historia, hivyo basi; sayansi haina msingi wa kujenga hoja za kukana kuwepo kwa MUNGU

[emoji4]
 
Science never claims can solve everything

.... NOT IN SCIENCE

Sayansi kiasili imemili kwenye majaribio na hujenga hitimisho kwa kuzingatia matokeo yaliyojikita kwenye makisio na bashiri. Sayansi kama zilivyo fani nyingine haijakingwa na mapungufu, kwa maana hiyo sayansi pekee haitoshi kutufanya tuuelewe ulimwengu katika uhalisia wake na usahihi, kukosekana kwa maarifa yaliyo katika sayansi kunakaribisha kuuchambua, kuujua na kuutazama ulimwengu katika pembe nyingine kama historia, falsafa, thiolojia nakadhalika, wengi katika watu wanaishi na kupumua sayansi na wanaamini katika DIVINITY, na licha tu ya kuamini pia hushukuru kwa kujaaliwa neema mfanowe sayansi kwani kwa kiasi kikubwa mno inawasaidia kukabiliana na changamoto za kimazingira katika ulimwengu wao, ama wengi wetu hatuvikinzanishi viwili hivi (sayansi vs thioloji) na badala yake tunapata faida mara mbili kwani vitabu vitakatifu pia hutudokeza kiasi kuhusu mambo kadhaa wa kadhaa yahusuyo sayansi ikiwemo embryology, relativity, quantum physics na mengineyo

[emoji4]
 
Ndio tunasema huko kwenye thiolojia mnajazana ujinga
Na ndio the biggest scam ever

Sadly you know nothing about theology though you pretend to know, no darkness like ignorance

[emoji4]
 
Wanathiolojia wapo busy Mungu gani ndio sahihi na wakweli
Sawa, maana yake ni

1. Wameafikiana hoja ya msingi zaidi kwao ambayo ni hii: MUNGU yupo, hivyo mengine ni ziada

2. Wanachaji bongo zao kwa majadiliano ambayo huwaongezea maarifa

3. Wao pia ni wanadamu, wana mapokeo, fikra na uelewa tofauti, hivyo hilo ni jambo la kawaida

4. Unaweza kuainisha jambo moja tu ambalo wanadamu wote ulimwenguni wamekubaliana kwa 100% pasina kutofautiana? chagua mfano wowote kwenye tasnia yoyote; sayansi, hisabati nakadhalika, nasubiri kwa hamu, nipo pale

[emoji4]
 
Mwanasayansi anatengeneza vitu vinavyosaidia maisha yetu ya kila siku

Wanatheojia wapo busy Mungu gani ndio sahihi na wakweli

1. Sayansi kwa lugha nyepesi inadili na vinavyoonekana, vinavyoshikika, vinavyohisika, vinavyosikika na vinavyopimika

2. Thiolojia kwa lugha nyepesi inashughulika na metafizikia na imani; visivyoonekana, visivyoshikika na visivyopimika

Wanathiolojia kama walivyo wanasayansi nao pia ni wabobezi, licha ya kuwepo mipaka, muingiliano na mkinzano mdogo katika maeneo yao, kwa wakati mmoja yeyote kati yao anaweza kujikita katika tasnia yake na pia kubeba fikra za mrongo wa upande mwingine kwa mfano SIR. ISAAC NEWTON alikuwa mwanasayansi na pia alikuwa mkristo, PROF. GEORGE LEMAITRE mwasisi wa nadharia ya bing bang alikuwa ni mchungaji

Wengi katika wanafalsafa na wanasayansi wakubwa kwa wadogo wanaamini kuwepo kwa DIVINITY (THEISM au DEISM), wapo wachache wasioamini kuwepo kwa MUNGU na kutokuamini kwao hakujajengwa kwenye misingi ya kisayansi, hivyo suala la kuwa mwanasayansi na kuamini au kutokuamini kuwepo kwa MUNGU ni uchaguzi uliyotokana na uchanganuzi na upembuzi wa hoja zilizomdiriki mlengwa
 
Wana JF naomba tufahamu kwamba

Sayansi kimantiki haiungi mkono ukana MUNGU, hoja za wakana MUNGU hazijamea kutoka kwenye sayansi bali katika falsafa (positivism philosophy of knowing approach) na saikolojia , hivyo mkana MUNGU yeyote anayejifanya kutumia hoja za kisayansi kupinga uwepo wa MUNGU ni JUHA nduguye KILAZA, hamna hoja ya kisayansi hata moja inayosadikisha madai yao; sayansi haishughuliki na metafizikia, maadili wala historia, hivyo basi; sayansi haina msingi wa kujenga hoja za kukana kuwepo kwa MUNGU

[emoji4]

Mkuu tunaweza kujadiliana bila personal attack na lugha za maudhi?

Huu sio UGONVI [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Ndio tunasema huko kwenye thiolojia mnajazana ujinga
Na ndio the biggest scam ever

Mwanasayansi anatengeneza vitu vinavyosaidia maisha yetu ya kila siku

Wanatheojia wapo busy Mungu gani ndio sahihi na wakweli

1. Je, unaweza kumtibia mtu mwenye kipindupindu (cholera) kwa maombi ya kiimani?

2. Je, unaweza kumtibia mtu aliyepandisha majini (mapepo) kisayansi?

[emoji4]
 
Mkuu tunaweza kujadiliana bila personal attack na lugha za maudhi?

Juha maana yake ni mjinga, hii ni sifa na si neno katika lugha chafu, ama neno KILAZA limetokana na jina la mchezea ala ya muziki (gitaa) aliyekuwa akiitwa JUMA KILAZA pale alipohitaji kushindanishwa na mwenzake hali ya kuwa uwezo wake ulikuwa mdogo
 
Huu sio UGONVI [emoji120][emoji120][emoji120]

Umeibua makosa ya tahajia kwa mara nyingine na nyingine; ni UGOMVI na si UGONVI, ni SIYO na siyo SIO, napaswa kuomba msamaha kwa kukukosoa kwa namna hiyo? pole, jikaze, nivumilie ndivyo nilivyo
 
Haiwezekani kwasababu imani ni kitu ambacho hakipo


Hakuna mapepo wala majini
Huwezi kutibu kitu ambacho hakipo
Umewahi kuvuta bangi iliyotokana na majani ya mmea wa vanilla?

[emoji4]
 
Yaani "kichaa mmoja" aanze kusema anaongea na Mungu na kumpa muongozo wa binadamu uweje halafu tukubali tu

Ndio tunasema huko kwenye thiolojia mnajazana ujinga

Mkuu tunaweza kujadiliana bila personal attack na lugha za maudhi?

Uandishi wa baadhi ya maneno yako unajitofautishaje na wangu?

Unahitaji marejeo zaidi juu ya uandishi wako uliojaa dhihaka na kebehi tofauti na hizi-quotes? rejea wasilisho lako la mada; post namba 1
 
Back
Top Bottom