Uongozi UDOM watetea PhD za Mawaziri, na Wabunge

Uongozi UDOM watetea PhD za Mawaziri, na Wabunge

sabuwanka

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
691
Reaction score
757
Siku mbili baada ya shahada za uzamivu (PhD) za viongozi wa kisiasa hasa Mawaziri na Wabunge kuibua mjadala, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) umezitetea na kueleza namna ya kuondoa shaka juu yake.

Akizungumza na Mwananchi, Makamu Mkuu wa UDOM, Profesa Faustine Bee amesema wenye shaka wanaweza kujiridhisha kwa kutembelea maktaba ya chuo hicho kuona machapisho ya wahitimu wenyewe.

Alisema suala la viongozi wakubwa kuhitimu shahada za uzamivu ni la muhusika mwenyewe anavyojipanga, kupangilia muda wake na majukumu aliyonayo.

“Ni suala la nidhamu ya muda, mtu kupangilia muda wake wa kazi na masomo kwa kuzingatia taratibu na maelekezo ya chuo na wasimamizi. Mimi sioni shida mtu kuhitimu kama anazingatia hayo,” alisema Profesa Bee

Profesa Bee alisema watu wengi wanaosoma shahada ya uzamili na uzamivu wakati wanafanya kazi na wana majukumu mengi, hivyo si sahihi kumhukumu mtu kisa ni mwanasiasa.

Profesa huyo alisema kama mwanafunzi anayesoma anayo nidhamu ya muda, licha ya majukumu yake, lazima atapata wasaa wa kukusanya taarifa.

“Hapa tuna walimu wengi wanasoma uzamivu na wanaendelea na kazi zao za kufundishia wakati nao wanasoma, hivyo suala sio nani, bali vigezo.

Wote hao (mawaziri, wabunge) wamefuata utaratibu wa usimamizi na kuwasilisha mawasilisho ambayo waliyatetea mbele ya jopo la wanataaluma,” alisema Profesa Bee.

Alisema mtu kazi kama si ya kwake, angeshindwa kuitetea, lakini wote walitetea kazi zao vizuri na taarifa na machapisho yao yanapatikana katika chuo hicho na watu wanaweza kuyaona kwa kuwa ni ya umma.

Mjadala huo uliibuliwa juzi na mwanazuoni na mwanasiasa mkongwe, Profesa Mark Mwandosya alipoandika kupitia Twitter: “Nawapongeza wanasiasa mliotunukiwa shahada za uzamivu, udaktari wa falsafa. Nawafahamu mna uwezo mkubwa. Lakini inawezekana kweli ukawa mbunge na waziri, ukapata muda wa utafiti na kuandika tasnifu, hata ya uzamili ni kazi sana. Swali kwa vyuo vikuu, je, vigezo au viwango vimebadilika?” alihoji Profesa Mwandosya.

Mbali ya kuwahi kuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwandosya pia aliwahi kuwa mbunge na waziri katika Serikali za tatu na nne.

Swali hilo limewaalika wanazuoni mbalimbali na mijadala kwenye mitandao ya kijamii, baadhi walimpinga na wengine wakimuunga mkono.
Gazeti la mwananchi la 21/12/2021
 
PhD by Thesis unaweza kuikamilisha hata kwa miaka miwili tu, inategemea commitment msimamizi na mtahiniwa mwenyewe. Pia inategemea research design na scope ya utafiti husika. Unaweza kupata PhD kirahisi ikiwa title na study yako ni ngumu au rahisi kwa kiwango gani

Kwa mtahiniwa wa PhD ni vizuri kuzingatia hayo, study yako ifanye iwe rahisi iwezekanavyo katika upatikanaji wa data na topic iwe straight na simple.

Vv
 
Hizi ni zama za tehama, kwa nini mtu aende mpaka chuoni kupata machapisho ya kazi zao ?

Nini kazi ya UDOM institutional repository ?

Kwa nini kazi za wanafunzi wengine zinawekwa huko lakini hizo za hao wanasiasa haizpatikani mpaka mtu aende mguu kwa mguu ?

IMG_20211222_075825.jpg
 
Hiki chuo cha UDom kinazidi kujengewa image mbaya kadri miaka inavyosonga. Kuna interview fulani ya kazi rafiki angu alishinda, wenzake wote walifyekwa kisa tu wamesoma UDom, yeye kasoma kwingne.
 
Chuo kikubwa kama UDOM kukosekana kwa haya machapisho kwenye mtandao ni uzamani sana. Au profesa hajaona umuhimu wa hiki kitu, kwa hiyo mtu aliye mfano nje ya nchi akihitaji kupitia haya machapisho afunge safari mpaka Tanzania?
 
Siku mbili baada ya shahada za uzamivu (PhD) za viongozi wa kisiasa hasa Mawaziri na Wabunge kuibua mjadala, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) umezitetea na kueleza namna ya kuondoa shaka juu yake.

Akizungumza na Mwananchi, Makamu Mkuu wa UDOM, Profesa Faustine Bee amesema wenye shaka wanaweza kujiridhisha kwa kutembelea maktaba ya chuo hicho kuona machapisho ya wahitimu wenyewe.

Alisema suala la viongozi wakubwa kuhitimu shahada za uzamivu ni la muhusika mwenyewe anavyojipanga, kupangilia muda wake na majukumu aliyonayo.

“Ni suala la nidhamu ya muda, mtu kupangilia muda wake wa kazi na masomo kwa kuzingatia taratibu na maelekezo ya chuo na wasimamizi. Mimi sioni shida mtu kuhitimu kama anazingatia hayo,” alisema Profesa Bee

Profesa Bee alisema watu wengi wanaosoma shahada ya uzamili na uzamivu wakati wanafanya kazi na wana majukumu mengi, hivyo si sahihi kumhukumu mtu kisa ni mwanasiasa.

Profesa huyo alisema kama mwanafunzi anayesoma anayo nidhamu ya muda, licha ya majukumu yake, lazima atapata wasaa wa kukusanya taarifa.

“Hapa tuna walimu wengi wanasoma uzamivu na wanaendelea na kazi zao za kufundishia wakati nao wanasoma, hivyo suala sio nani, bali vigezo.

Wote hao (mawaziri, wabunge) wamefuata utaratibu wa usimamizi na kuwasilisha mawasilisho ambayo waliyatetea mbele ya jopo la wanataaluma,” alisema Profesa Bee.

Alisema mtu kazi kama si ya kwake, angeshindwa kuitetea, lakini wote walitetea kazi zao vizuri na taarifa na machapisho yao yanapatikana katika chuo hicho na watu wanaweza kuyaona kwa kuwa ni ya umma.

Mjadala huo uliibuliwa juzi na mwanazuoni na mwanasiasa mkongwe, Profesa Mark Mwandosya alipoandika kupitia Twitter: “Nawapongeza wanasiasa mliotunukiwa shahada za uzamivu, udaktari wa falsafa. Nawafahamu mna uwezo mkubwa. Lakini inawezekana kweli ukawa mbunge na waziri, ukapata muda wa utafiti na kuandika tasnifu, hata ya uzamili ni kazi sana. Swali kwa vyuo vikuu, je, vigezo au viwango vimebadilika?” alihoji Profesa Mwandosya.

Mbali ya kuwahi kuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwandosya pia aliwahi kuwa mbunge na waziri katika Serikali za tatu na nne.

Swali hilo limewaalika wanazuoni mbalimbali na mijadala kwenye mitandao ya kijamii, baadhi walimpinga na wengine wakimuunga mkono.
Gazeti la mwananchi la 21/12/2021
Rushwa imeingia mpaka kwenye taasisi za elimu ya juu, tumekwisha
 
Dah Prof Faustine K Bee anajishusha.
Wahadhiri wengi kusoma kwao ni rahisi maana wanashinda wanafundisha hivyo vitu,na kuna assignment hutoa kwa wanafunzi zinawasaidia hata wao katika masomo yao.

Sasa mwanasiasa akashinde anazurula bungeni kweli,na wao kirahisi tu wanampa PhD!

Sikutegemea haya kwa msomi na kiongozi wetu mkubwa kama prof.K Bee.
 
Hiki chuo cha UDom kinazidi kujengewa image mbaya kadri miaka inavyosonga. Kuna interview fulani ya kazi rafiki angu alishinda, wenzake wote walifyekwa kisa tu wamesoma UDom, yeye kasoma kwingne.
🤔🤔🤔🤔🤔 Noted.
 
Chuo kikubwa kama UDOM kukosekana kwa haya machapisho kwenye mtandao ni uzamani sana. Au profesa hajaona umuhimu wa hiki kitu, kwa hiyo mtu aliye mfano nje ya nchi akihitaji kupitia haya machapisho afunge safari mpaka Tanzania?
Huyo nae hana sifa ya kuongoza hiyo taasisi. Bora angenyamazatu
 
Hiki chuo cha UDom kinazidi kujengewa image mbaya kadri miaka inavyosonga. Kuna interview fulani ya kazi rafiki angu alishinda, wenzake wote walifyekwa kisa tu wamesoma UDom, yeye kasoma kwingne.
Achaa uwongo wewe mbona mimi niliwashinda waliosoma UDSM wote
 
Siku mbili baada ya shahada za uzamivu (PhD) za viongozi wa kisiasa hasa Mawaziri na Wabunge kuibua mjadala, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) umezitetea na kueleza namna ya kuondoa shaka juu yake.

Akizungumza na Mwananchi, Makamu Mkuu wa UDOM, Profesa Faustine Bee amesema wenye shaka wanaweza kujiridhisha kwa kutembelea maktaba ya chuo hicho kuona machapisho ya wahitimu wenyewe.

Alisema suala la viongozi wakubwa kuhitimu shahada za uzamivu ni la muhusika mwenyewe anavyojipanga, kupangilia muda wake na majukumu aliyonayo.

“Ni suala la nidhamu ya muda, mtu kupangilia muda wake wa kazi na masomo kwa kuzingatia taratibu na maelekezo ya chuo na wasimamizi. Mimi sioni shida mtu kuhitimu kama anazingatia hayo,” alisema Profesa Bee

Profesa Bee alisema watu wengi wanaosoma shahada ya uzamili na uzamivu wakati wanafanya kazi na wana majukumu mengi, hivyo si sahihi kumhukumu mtu kisa ni mwanasiasa.

Profesa huyo alisema kama mwanafunzi anayesoma anayo nidhamu ya muda, licha ya majukumu yake, lazima atapata wasaa wa kukusanya taarifa.

“Hapa tuna walimu wengi wanasoma uzamivu na wanaendelea na kazi zao za kufundishia wakati nao wanasoma, hivyo suala sio nani, bali vigezo.

Wote hao (mawaziri, wabunge) wamefuata utaratibu wa usimamizi na kuwasilisha mawasilisho ambayo waliyatetea mbele ya jopo la wanataaluma,” alisema Profesa Bee.

Alisema mtu kazi kama si ya kwake, angeshindwa kuitetea, lakini wote walitetea kazi zao vizuri na taarifa na machapisho yao yanapatikana katika chuo hicho na watu wanaweza kuyaona kwa kuwa ni ya umma.

Mjadala huo uliibuliwa juzi na mwanazuoni na mwanasiasa mkongwe, Profesa Mark Mwandosya alipoandika kupitia Twitter: “Nawapongeza wanasiasa mliotunukiwa shahada za uzamivu, udaktari wa falsafa. Nawafahamu mna uwezo mkubwa. Lakini inawezekana kweli ukawa mbunge na waziri, ukapata muda wa utafiti na kuandika tasnifu, hata ya uzamili ni kazi sana. Swali kwa vyuo vikuu, je, vigezo au viwango vimebadilika?” alihoji Profesa Mwandosya.

Mbali ya kuwahi kuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwandosya pia aliwahi kuwa mbunge na waziri katika Serikali za tatu na nne.

Swali hilo limewaalika wanazuoni mbalimbali na mijadala kwenye mitandao ya kijamii, baadhi walimpinga na wengine wakimuunga mkono.
Gazeti la mwananchi la 21/12/2021
Professor mwenyewe anaitwa Bee halafu tunatarajia awe serious
 
Asante Mkuu. Hili suala JUMANNE KISHIMBA (Mb) amekuwa akiihoji Serikali.

Aliyesoma kuanzia chekechea hadi anapata Shahada ya Uzamili kwa kukalishwa darasani akifundishwa na Mwalimu ni vigumu sana kukuelewa.
 
Back
Top Bottom