Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,984
Kwa wale manofuatilia taarifa za usahihi wa utambulisho wa Denis Urio nadhani mmeona waliosoma sekondari ya Kingori wakikataa kutomfahamu shahidi huyu means awakusoma naye.
Nimetafuta ilipo Kingori Secondary inasomeka ipo wilaya ya Arumeru siyo Hai. Nimetafuta wanafunzi waliomaliza form four 1999 hakuna jina la Denis Urio kwenye hiyo shule.
Lakini pia shahidi anaonekana kutomfahamu hata mwalimu mkuu na hii ndiyo sababu ya Mimi kufanya search kuona huyu mtu anafahamika? Tofauti na majina na mwaka lakini shahidi ameshindwa kujua hata divisheni 4 inaanza na alama ngapi.
Katika mazingira haya unajiuliza huyu mtu kwanini hakufukuzwa kazi wakati wa vyeti feki? Lakini kama taarifa zinazosambaa mitandaoni zinadai Denis Urio ambaye siyo mchaga ni mmeru alihitimu shule 2000 na familia ya Urio ipo karibu na shule kwanini vyombo vya habari visitafute ukweli?
Kwa upande wa mahakama, kwanini wanakubali kupokea mashahidi ambao wanataarifa za majina ya watu wengine? Je, upande wa utetezi kwanini wasiombe Mhe. Jaji wafungue kesi ndani ya kesi ili kuthibitisha mahakamani kwamba shahidi aliyepo mahakamani hayo ni majina yake?
Kwanini upande wa utetezi wasiwekee pingamizi ushahidi wa Denis Kwa kuwa huyu siyo Denis Hadi atakapothibitika kwamba ni Denis.
Kuweka pingamizi kutawafanya utetezi waweze kuwasilisha ushahidi kuthibitisha huyu shahidi anadanganya taarifa zakuzaliwa na taarifa za wazazi wake, maana naamini akihojiwa majina ya wazazi wake yaani baba na mama, wapi walipo, amezaliwa Kijiji Gani na kusomea primary wapi utakuja kubaini huyu ni Denis au si Denis
Nimetafuta ilipo Kingori Secondary inasomeka ipo wilaya ya Arumeru siyo Hai. Nimetafuta wanafunzi waliomaliza form four 1999 hakuna jina la Denis Urio kwenye hiyo shule.
Lakini pia shahidi anaonekana kutomfahamu hata mwalimu mkuu na hii ndiyo sababu ya Mimi kufanya search kuona huyu mtu anafahamika? Tofauti na majina na mwaka lakini shahidi ameshindwa kujua hata divisheni 4 inaanza na alama ngapi.
Katika mazingira haya unajiuliza huyu mtu kwanini hakufukuzwa kazi wakati wa vyeti feki? Lakini kama taarifa zinazosambaa mitandaoni zinadai Denis Urio ambaye siyo mchaga ni mmeru alihitimu shule 2000 na familia ya Urio ipo karibu na shule kwanini vyombo vya habari visitafute ukweli?
Kwa upande wa mahakama, kwanini wanakubali kupokea mashahidi ambao wanataarifa za majina ya watu wengine? Je, upande wa utetezi kwanini wasiombe Mhe. Jaji wafungue kesi ndani ya kesi ili kuthibitisha mahakamani kwamba shahidi aliyepo mahakamani hayo ni majina yake?
Kwanini upande wa utetezi wasiwekee pingamizi ushahidi wa Denis Kwa kuwa huyu siyo Denis Hadi atakapothibitika kwamba ni Denis.
Kuweka pingamizi kutawafanya utetezi waweze kuwasilisha ushahidi kuthibitisha huyu shahidi anadanganya taarifa zakuzaliwa na taarifa za wazazi wake, maana naamini akihojiwa majina ya wazazi wake yaani baba na mama, wapi walipo, amezaliwa Kijiji Gani na kusomea primary wapi utakuja kubaini huyu ni Denis au si Denis