Update: Mwili wa Mtoto Albino (Asimwe) wakutwa hauna baadhi ya viungo

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mtoto mwenye Ualbino Asimwe Novath aliyekuwa na miaka miwili na miezi sita, mkazi wa Kitongoji cha Mbale Kijiji cha Bulamula kata ya Kamachumu wilaya ya Muleba mkoani Kagera amekutwa amefariki na mwili wake umefungwa kwenye mfuko (Sandarusi) huku ukiwa hauna baadhi ya viungo.

Akizungumzia tukio hilo Katibu Tawala Wilaya ya Muleba Benjamin Mwikasyege amesema kuwa mwili huo umekutwa umetelekezwa kwenye karavati yenye maji ya barabara ya Makongora, Kijiji cha Malele.

Aidha ameongeza kuwa mwili wa marehemu umechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano ili kubaini walio tekeleza tukio hilo.

Asimwe Novath aliibwa nyumbani kwao Mei 30 mwaka huu, baada ya mama yake kukabwa na watu wasio julikana usiku wa saa 2:30 kisha mtoto huyo kuchukuliwa ambapo amekuwa akitafutwa hadi mwili wake ulipopatikana leo Juni 17, 2024, katika Kijiji cha Malele kata Ruhanga wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

asimwe-jpg.3020827
Pia soma:
- Kagera: Kisa cha Mtoto mwenye Ualibino kudaiwa kuibiwa, RPC Makungu asema tayari wameanza uchunguzi

- Kufuta mauaji ya albino, ni kutokomeza kabisa Waganga wapiga ramli
 
Mtoto wa miaka miwili mwenye ualbino Asiimwe Novath ambaye aliyedaiwa kuibiwa nyumbani kwao usiku wa tarehe 30, Mei 2024 akiwa na mama yake katika kijiji cha Bulamula, wilayani Muleba Mkoani Kagera imeripotiwa miwili wake umepatikana leo Juni 17,2023 ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake ikiwamo mikono miwili, Ulimi na Macho.
Screenshot_20240617-200807_1.jpg

Akizungumzia tukio hilo mama mkubwa wa mtoto huyo Vestina Richard, amesema wamepigiwa simu na mwenyekiti wa kijiji jirani na kupewa taarifa kuwa kuna mwili wa mtoto umeokotwa na raia, ndipo walipotuma watu kuthibitisha kama mwili ule ni wa mtoto Asiimwe.

"Mwili umekutwa umechoka vibaya, amekatwa mikono yote miwili, ametolewa macho na amekatwa ulimi." Amesema Vestina.

Akizungumzia tukio hilo Katibu Tawala Wilaya ya Muleba, Benjamin Mwikasyege amesema mwili huo umekutwa umetupwa kwenye karavati yenye maji, barabara ya makongora Kijiji cha Malele.

Ameongeza kuwa mwili umechukuliwa kwa ajili ya hatua za uchunguzi huku akitoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano kubaini waliohusika na tukio hilo.

Itakumbukuwa mtoto huyo mtoto huyo ni zaidi ya siku 15 tokea alipodaiwa kuibiwa huku ikidaiwa kuwa Baba Wa mtoto huyo alishikiliwa na polisi tangu tukio hilo lilipotokea kwa ajili ya uchunguzi.

Soma Kagera: Kisa cha Mtoto mwenye Ualibino kudaiwa kuibiwa, RPC Makungu asema tayari wameanza uchunguzi
 
Mtoto mwenye Ualbino Asimwe Novath aliyekuwa na miaka miwili na miezi sita, mkazi wa Kitongoji cha Mbale Kijiji cha Bulamula kata ya Kamachumu wilaya ya Muleba mkoani Kagera amekutwa amefariki na mwili wake umefungwa kwenye mfuko (Sandarusi) huku ukiwa hauna baadhi ya viungo.

Akizungumzia tukio hilo Katibu Tawala Wilaya ya Muleba Benjamin Mwikasyege amesema kuwa mwili huo umekutwa umetelekezwa kwenye karavati yenye maji ya barabara ya Makongora, Kijiji cha Malele.

Aidha ameongeza kuwa mwili wa marehemu umechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano ili kubaini walio tekeleza tukio hilo.

Asimwe Novath aliibwa nyumbani kwao Mei 30 mwaka huu, baada ya mama yake kukabwa na watu wasio julikana usiku wa saa 2:30 kisha mtoto huyo kuchukuliwa ambapo amekuwa akitafutwa hadi mwili wake ulipopatikana leo Juni 17, 2024, katika Kijiji cha Malele kata Ruhanga wilaya ya Muleba mkoani Kagera.
 
Mtoto wa miaka miwili mwenye ualbino Asiimwe Novath ambaye aliyedaiwa kuibiwa nyumbani kwao usiku wa tarehe 30, Mei 2024 akiwa na mama yake katika kijiji cha Bulamula, wilayani Muleba Mkoani Kagera imeripotiwa miwili wake umepatikana leo Juni 17,2023 ukiwa umeondolewa baadhi ya viungo vyake ikiwamo mikono miwili, Ulimi na Macho.
View attachment 3019577
ilipotokea kwa ajili ya uchunguzi.

Soma Kagera: Kisa cha Mtoto mwenye Ualibino kudaiwa kuibiwa, RPC Makungu asema tayari wameanza uchunguzi
Ukatili,unyama wa ajabu sana huu!
 
TZ ni moja ya nchi yenye high rate of albinism duniani cha ajabu tunawaua hadi leo.

"Tanzania has the highest rate of people with albinism in the world, with estimates ranging from one in 1,400 to one in 1,429 people. This is much higher than other countries, such as the US, where the rate is one in 20,000."
 
Back
Top Bottom