Elections 2015 Updates: Mchakato na Matokeo ya kura za maoni ya Ubunge CCM nchini kote

Elections 2015 Updates: Mchakato na Matokeo ya kura za maoni ya Ubunge CCM nchini kote

songea mjini nani kapita
Kapita Leonidas Gama, yule Mkuu wa Mkoa mwenye uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi na kusimamia. Ni pandikizi la mtu kama Cptain John Komba. Pale CCM wamelamba dume
 
msagatiherry huyo Abedi na siasa haijui maana yeye maslahi yapo mbele . ndio aliyoipotosha ccm 2010 kuwa monica mbega anakubalika kumbe ikawa kinyume so kwa taarifa yako safari hii CCM makao makuu wana watu wao kila jimbo hawadanganyike kwa kuwasikilza watu kama abeid ambayo ni mpotoshaji.

Unamaanisha kuwa mgombea ubunge anapangwa Lumumba! Kura za maoni za wanaccm kumbe hazina maana? Lumumba wakifanya hivyo itakuwa shangwe upand wa pili!
 
Last edited by a moderator:
Kapita Leonidas Gama, yule Mkuu wa Mkoa mwenye uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi na kusimamia. Ni pandikizi la mtu kama Cptain John Komba. Pale CCM wamelamba dume

Nimefurahi mno tena mno.Huyo serikali ijayo namwombea asikose nafasi kubwa ya uongozi ana uwezo mkubwa sana tena sana
 
Wewe upo wapi nipo iringa hapa ccm imedorora kbs na mtu waliyekuwa wanamtegemea mama jesca kawa wa tatu magamba wenyewe wanasema bado mchungaji msigwa ni shida jipange na hoja zako

Jamani iringa nina hamu ya kujua mtu alijiita frank kibik alinadiwa kwa udi na uvumba na mkewe anajiita tumaini msowoya kiasi cha kumnadi kupitiliza... kashika nafas ya ngap
 
Nakumbuka mwaka wa 1979 mashujaa wetu walipotoka vitani waliripoti kwa mkubwa wao, walitoa taarifa yao yenye maneno machache kwamba "kazi tuliyotumwa tumeimaliza"

Vijana wetu na wamama tuliowatuma baada ya kukabidhiwa kadi za ccm katika ofisi za chama, waliopewa jukumu la kuhakikisha wanampigia kura mgombea tunayetaka kupanda naye jukwaani. Mungu mkubwa wanachama wetu wa chadema wenye kadi za CCM wamerudi kwa furaha, wametupatia taarifa kuwa "kazi waliyotumwa wamemaliza"

Mh. Lema hana haja ya kufanya kampeni tena Arusha, jukumu alilonalo sasa ni kwenda kuwashukuru wananchi wakati anasubiri kuapishwa.

Huyu Monaban ambaye hapa Arusha anajulikana kuwa mbakaji wa maeneo ya wazi kwa kujimilikisha kwa hila tunampiga asubuhi kabla ya misa ya kwanza...
 
Mikumi Vipi wakuu mbona mmenichinjia Baharini
 
Asitegemee kama ataweza kumtingisha lema aendelee tu kuuza unga wake
 
ccm makundi mwaka huu yatawanyonga Lema hana mpinzani Arusha
 
Kwa hali ilivyo kwa sasa hakuna anaeweza kupambana na UKAWA. Ata ccm sio saizi ya UKAWA.
 
Nasikia huko kwa ngazi ya udiwani ndiyo mmeharibu kabisa, ninavyoona mimi wengi walioshinda kura za maoni hawatapitishwa kugombania majimbo ama kata walizoshinda, watapitishwa wengine hata waliopata ushindi mdogo kabisa.
 
Back
Top Bottom