Updates: Misri vs Tanzania [Michuano ya makundi kufuzu AFCON 2017]

Mkude hafanyagi kitu stars

nadir haroub " cannavaro " anafanya nini? acha upoyoyo wako uliotukuka. mkude si unaona hapo anavyohangaika katikati na hapati ushirikiano? au huoni mkuu? kwanza samahani naomba kujua hapo ulipo unauangalia huu mpira au unataka tu kunipotezea muda wangu huku wewe ukiangalia mpira kwa kupitia simulizi tu za watu humu? nadhani utakuwa huna tofauti na wale mashabiki wetu wa kibongo wanaoingia mpirani zikiwa zimebaki dakika 15 mpira kuisha ( fungulia mbwa au ng'ang'a ) sasa subiri waingie zikiwa zimebaki hizo dakika halafu mpira uishe uone watakavyohadithia kwa uwongo na kweli utadhani wametizama mechi full time!
 
Kwa T. Stars hii sina hata tone la matumaini. Wameenda mapumziko kutuvutia kasi, kichapo hakiepukiki.
 
Taifa Stars sijui hawajakula, wakiguswa tu wanapepea watu wanachukua mpira.

ethiopia kuna lishe kweli? wao wenyewe miili yao ni ya " mbu " full kukondeana kwa matatizo ya lishe halafu timu imeweka huko kambi wiki moko unadhani watakuwa na stamina kweli mkuu?
 
Huyu dogo anaevaa jezi namba 9 ana rasta ndio nani? Kanyoosha msuli mmoja matata sana hapa, kidogo walie jamaa, dah timu nzima namjua cannavaro na Henry morris na mbwana samatta, na kapombe

hata mimi huyo henry morris wako simjui je ni mchezaji wa kutoka ulaya au?
 

Shida yako umeingiza usimba na uyanga!! mi siko huko mkuu
 
Nadhani Stars inajitahidi sana. Nimeangalia dakika 30 za mwisho kipindi cha kwanza. Golikipa ni mzuri sana, bila jitihada zake tungekuwa tumepigwa mbili mpaka half time hii. Beki mwenye jezi namba 2-nadhani ni Nyoni huyu, anacheza vizuri sana. Tatizo letu mpira unadunda sana eneo letu. Tujibadilisha ukawa unadunda kwao tunaweza kutoka na ushindi.
 
hata mimi huyo henry morris wako simjui je ni mchezaji wa kutoka ulaya au?

Kamanda hiyo timu ya Taifa yenyewe nashangilia kwa kuwa ni mbongo tu wa asili, sijawahi kuona mechi yyte uwanjani, kwa sababu siishi home ntamjulia wapi? Nasikia tu mtangazaji hapa anataja jina
 
Chanel gani wanaonyesha?

endelea tu mkuu kukodolea macho humu humu jf kwani members wote waliomo humu kwa sasa na wanaochangia ndiyo channel yenyewe hivyo tufuatilie tu na usibanduke hapo ulipo tafadhali.
 
Huyu dogo anaevaa jezi namba 9 ana rasta ndio nani? Kanyoosha msuli mmoja matata sana hapa, kidogo walie jamaa, dah timu nzima namjua cannavaro na Henry morris na mbwana samatta, na kapombe

Kiemba huyo

Nashangaaga kule azam wanambaniaga sana, sijui kwanini wakati anaonekana ana kiwango kizuri tu akiwa regular player
cc Watu8
 
Last edited by a moderator:
Huyu dogo anaevaa jezi namba 9 ana rasta ndio nani? Kanyoosha msuli mmoja matata sana hapa, kidogo walie jamaa, dah timu nzima namjua cannavaro na Henry morris na mbwana samatta, na kapombe

Duh!!

Mkuu Henry Morris ni mchezaji wa zamani sana huyo alikuwa anakipiga Prisons nafikiri akasajiliwa Yanga baadaye...

Ni wale wachezaji wa mwanzo kabisa kuonekana na Prisons ligi kuu...

Sasa hivi atakuwa hachezi tena mpira huyu...
 
ethiopia kuna lishe kweli? wao wenyewe miili yao ni ya " mbu " full kukondeana kwa matatizo ya lishe halafu timu imeweka huko kambi wiki moko unadhani watakuwa na stamina kweli mkuu?

Hii comment yako nimecheka mkuu. Kwahiyo walikwenda kufanya mazoezi ya njaa?
 
Kipindi cha pili kinaanza...
 
Hamasa ya timu yetu ipochini sana utafikiri hakuna kinachoendelea yaani watu matokeo yoyote ya kufungwa wamejiandaa nayo lkn kinyume na hapo huenda watu wakaigeuzia uso, matokeo km vile droo au bahati mbaya ushindi
 
Shida yako umeingiza usimba na uyanga!! mi siko huko mkuu

ahsante, jamaa ameleta ushabiki wa vilabu wakati hii ni stars, mbona kuna thread za simba na yanga humu lakn zimekufa hamna wa kuzifufua, hebu tuongelee kinachoendelea simba na yanga tuweke pembeni kwa muda mfupi huu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…