Updates: Misri vs Tanzania [Michuano ya makundi kufuzu AFCON 2017]

Updates: Misri vs Tanzania [Michuano ya makundi kufuzu AFCON 2017]

Nadhani muziki kwa sasa unaleta maana zaidi ya fani zingine zote za michezo Tanzania. Kwingine kote tumeshindwa..
 
Wamejitahidi sana kupunguza mabao, maana Yanga ya mwaka ule walipigwa 6-0. Hongereni Pluijm na muajiri wako Malinzi

Kwani timu iliyocheza ni Yanga au timu ya taifa?

Hata hivyo ni wachezaji watatu tu wa Yanga waliochezeshwa leo Dida, Nadir na Joshua
 
Henry Morris msimu uliopita alikuwa Mtibwa,akitokea Simba ambapo alichezea baada Ya kutoka Kovinger Ya Norway. Na before alikuwa Simba. Aliechezea Prison ni Oswald Morris! Henryhajawi kuchezea Prison

Mkuu acha kuwa mbishi...

Huyo unayemuita wewe Henry Morris unakosea, ni Henry Joseph na ndiye aliyecheza huko Norway baada ya kutoka Simba na pia msimu uliopita alikuwa Mtibwa...

Henry Morris ni mchezaji(mshambuliaji) wa zamani wa Taifa Stars na Prisons ya Mbeya. Wakati yupo Prisons alikuwa anacheza na kaka yake Oswald Morris.

Hii ni ile Prisons ya kina Kasonso iliyobeba ubingwa wa muungano kama kumbukumbu zangu zipo sahihi...

Baadaye Henry alichukuliwa na Yanga na mpira ukaishia hapo...
 
Kana sijaachana na soka mwaka huu stakuja kuacha,shabiki wa liverpool,simba na taifa stars...
 
Watanzania mnaweza kutangaza nia tu...

Uzalendo badae sana...
 
tutajiudhi sana matatizo ya mpira wetu ni mengi, maandalizi ya vijana kuazia kule umitashumta, umiseta, timu b za vilabu vya ligi kuu na timu za kids zao zote ovyo. Tumechagua kuwekeza kwenye siasa kuliko kitu kingine chochote; bunge la katiba, kampeni, mikutano hivi vitu ndo vimetujaa vichwani kwetu. viongozi wa michezo wanaigeuza kama madaraja ya kuingilia kwenye siasa. Usishangae Malinzi nae akachukua fomu za ubunge kama wenzake kina Mkamia, Rage, Madega na wengineo.

Hatujali tena kuandaa wachezaji wachanga kwenye vilabu vyetu , tunahangaika na mafather wanaodanganya umri kina Haruna Moshi, Mgosi na wenzao.

Ligi yetu inayolisha Taifa Stars huko ndiko kina Simba, Yanga, Azam wanakoshindana kununua mechi. Wachezaji wanavimba vichwa kumbe ushindi umeshapatikana kabla ya mechi. Huko mikoani ndio balaa uzalendo ni wa kufa mtu kwenye viwanja vya timu zao.

Tutabadilisha makocha mpaka basi, kuna vingi vya kubadilisha. Hata tukijitoa mashindano ya kimataifa kwa miaka 20 haitasaidia kama matatizo ya mpira wetu hayatapata dawa . Tuanze na Viongozi wa soka.
 
Wamejitahidi sana kupunguza mabao, maana Yanga ya mwaka ule walipigwa 6-0. Hongereni Pluijm na muajiri wako Malinzi
Acha kuongea bila Facts kama unatokea kwenye vijiwe vya bange!
Hivi unajua idadi ya wachezaji wa yanga waliocheza game dhidi ya Misri!!!!!
Hao wachezaji wa simba unaowaona wewe wanajua wamefanya nini kule Rwanda ambako waliitwa kwenda kwenye mashindano ya kuadhimisha mauaji ya kimbali!!! Mbona walipigwa game zote mbili tena wakicheza na timu ambazo hazikutumia wachezaji wao muhimu wa timu za taifa?!
Tuzungumzia timu yote ya taifa bila kutaja wachezaji wa timu fulani. Tutafute chanzo cha timu yetu ya taifa kufanya vibaya katika mashindano mbalimbali.
 
Hebu tuacheni ushabiki pembeni,mi nadhani kuna haja ya kutafuta mwekezaji katika timu yetu ya taifa.Mpira siku hizi ni biashara.Hili ndo halijawahi kufanyika,nina iman waTz watapata burudani safi.
 
Dida, Kapombe, Nadir, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Mkude, Nyoni, Kazimoto, Kiemba, Ulimwengu, Samatta

hapo mafundi walikuwa ni wawili tu mkude na samatta wengine waliobaki ni mapoyoyo watupu. timu ikishakuwa na michezaji mingi ya yanga tayari ni nuksi na laana tosha na kwanini tusipigwe hizo za juma nature tatu bila? halafu angalia jinsi mtangazaji poyoyo mwingine maulid kitenge alivyokuwa akifurahia kuwa eti timu yetu itaibuka na ushindi kwakuwa inacheza katika uwanja usio na mashabiki. sasa jana tumecheza bila hao mashabiki tumepigwa " za juma nature " tatu bila je mashabiki wao wangekuwepo tungepigwa ngapi? ushauri wangu tu mtangazi huyu maulid kitenge ajitahidi kubadilika na ajifunze kuwa analyst na kinachomopnza ni ushabiki wake wa kipuuzi na sasa ameshatuaminisha ni kwanini hata form four " alizungusha ". tena naona kama vile misri jana wametustahi tu pengine kwakuwa tanzania nayo ipo mstari wa mbele katika kutatua mgogoro wao wa kisiasa ila wangeondoa huo ukarimu kwetu nakuambieni jana tungekula wiki (7) au kikosi cha timu nzima(11).
 
Back
Top Bottom