Upelelezi kesi ya Zumaridi haujakamilika, kwanini anashikiliwa?

Upelelezi kesi ya Zumaridi haujakamilika, kwanini anashikiliwa?

Hapa ndipo ulipo ujinga wetu -- FAM

Kwamba Kila tunayemdhania ni mchuma janga na akale na wa kwao.

Kwani mkuu wewe ni mlamba asali?
Mkuu kuna wakati ukiteleza kutaka kuonesha kana kwamba una nguvu kuliko serikali, lazima serikali ikuoneshe kwamba ipo na ina msuli, iwe kwa haki au kwa figisu figisu.
Vinginevyo tutakuwa na nchi isiyotawalika kabisa

Hata Wewe ungekuwa mtawala, huwez kuruhusu tukio la askari kupigwa na Watu eti makerubi lipite kimya kimya.
Kesho na keshokutwa askari watakuwa wakipigwa na kuzuiwa kufanya kazi zao na Watu au makundi mengine. Mwisho wake ni nini? Lazima somo litolewe kwamba ukifika sehemu fulani ni moto utaungua.
 
Watakuwa wameziona ni nyepesi, wao wanatafuta nzito zaidi ambazo hazionekani matokeo yake wanaendelea kumshikilia tu kiuonevu.
Tafsiri kamili ya kuwa wanachofanya ni uonevu uliopitiliza yaani ukiukaji mkubwa wa haki za wengine.
 
Kwenye himaya ya walamba asali uongo uongo ndiyo kwao. Mambo nyeti hufanyiwa siasa.

Alisema Samia watuhumiwa waache kukamatwa bila upelelezi kuwa umekamilika. Hizo kumbe zilikuwa hekaya za abunwasi tu.

Kumesikika Mwanza:

"Wakili wa Serikali Mwandamizi, Hemedi Khalid ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa kuwa upelelezi wa kesi inayomkabili Diana Bundala, maarufu kama ‘Mfalme Zumaridi’ haujakamilika."

Tabora Nako,

""Watu wasikamatwe kabla ya uchunguzi," Waziri Mkuu Majaliwa haimuhusu?"

Uongo uongo tu kwenye mambo nyeti. Huu ni muendelezo ule ue wa kutuona wananchi ni kama mang'ombe tu, kwa kutopigania kuona haki zetu zinalindwa kwa mujibu wa katiba.

Yapi yameheshimiwa? Ni kuacha kupigwa au kuteswa watuhumiwa? Ni polisi traffic kujazana mabarabarani kufukuzia rushwa? Ni takukuru kuwajibika? Ni maoni ya wananchi kuheshimiwa? Nk, nk?

Ama kwa hakika, "watanzania tatizo letu ni ujinga uliopitiliza." -- FAM.
Mi nafikiri Mungu wa Zumaridi alikamatwa kabla ya maelekezo hayo kutolewa. Ukumbuke kuwa Mwanza pia kuna Masheikh na Maustaadh kibao wapo Butimba kwa zaidi ya miaka kumi kisa tu "upelelezi bado haujakamilika". Hivyo unapolaumu kwa miezi sita lia kabisa kwa wale wa zaidi ya miaka kumi.
 
Mkuu kuna wakati ukiteleza kutaka kuonesha kana kwamba una nguvu kuliko serikali, lazima serikali ikuoneshe kwamba ipo na ina msuli, iwe kwa haki au kwa figisu figisu.
Vinginevyo tutakuwa na nchi isiyotawalika kabisa

Hata Wewe ungekuwa mtawala, huwez kuruhusu tukio la askari kupigwa na Watu eti makerubi lipite kimya kimya.
Kesho na keshokutwa askari watakuwa wakipigwa na kuzuiwa kufanya kazi zao na Watu au makundi mengine. Mwisho wake ni nini? Lazima somo litolewe kwamba ukifika sehemu fulani ni moto utaungua.

Utawala ni kwa mujibu wa katiba. Katiba inayoruhusu utawala wenye kukomoa wengine kwa sababu yoyote Ile, hauwezi kuwa na nafasi katika jamii yoyote ya binadamu. Labda kwa jamii ya wanyama wa porini.
 
Rais haoni kuwa hatoshi kwa kusimama majukwaani kupiga hadithi za sungura na fisi kwenye haki zetu? Kwa hakika tunahitaji katiba itakayotusimamia. Siyo hawa ndumila kuwili!
Ni mambo yale yale ya kusema maendeleo hayana chama huku unageuka kusema wasiochagua chama changu wasahau maendeleo.

Hili la kukamata baada ya upelelezi kukamilika ni uongo tu kama uongo mwingine.
 
Mi nafikiri Mungu wa Zumaridi alikamatwa kabla ya maelekezo hayo kutolewa. Ukumbuke kuwa Mwanza pia kuna Masheikh na Maustaadh kibao wapo Butimba kwa zaidi ya miaka kumi kisa tu "upelelezi bado haujakamilika". Hivyo unapolaumu kwa miezi sita lia kabisa kwa wale wa zaidi ya miaka kumi.

Nisome vyema mkuu. Ninaongelea ukiukwaji wote wala si Zumaridi peke yake. Nikitambua zipo kesi nyingi ambazo hata zingine media haijaziangazia kufikia kufahamika.

Tusaidiane kupiga kelele kuyaweka madhila ya wenzetu vikaangoni kufahamika.

Ifahamike bila kuisafisha nyumba hii, Leo wao kesho sisi.

Unyamani hakuna aliye salama.
 
Utawala ni kwa mujibu wa katiba. Katiba inayoruhusu utawala wenye kukomoa wengine kwa sababu yoyote Ile, hauwezi kuwa na nafasi katika jamii yoyote ya binadamu. Labda kwa jamii ya wanyama wa porini.
Kutawala kwa katiba 100% ni theory maana hakuna katiba yenye ufanisi 100%, hilo gap ndio huwa linafidiwa na msuli sasa. Ishi kwa practical hiyo na utakuwa salama
 
Nisome vyema mkuu. Ninaongelea ukiukwaji wote wala si Zumaridi peke yake. Nikitambua zipo kesi nyingi ambazo hata zingine media haijaziangazia kufikia kufahamika.

Tusaidiane kupiga kelele kuyaweka madhila ya wenzetu vikaangoni kufahamika.

Ifahamike bila kuisafisha nyumba hii, Leo wao kesho sisi.

Unyamani hakuna aliye salama.
Nakuunga mkono. Ila tuanze kufuatilia kwanza, Sheria hii inaanzia wapi. Kama inarudi nyuma, basi tupaze sauti waachiwe.
 
Nakuunga mkono. Ila tuanze kufuatilia kwanza, Sheria hii inaanzia wapi. Kama inarudi nyuma, basi tupaze sauti waachiwe.

Ikumbukwe kuwa si sheria bali ni tamko la nia njema toka kwa amiri jeshi mkuu. Tunayataka haya kwa mujibu wa sheria.

Kama matamko yake hayana mashiko ndipo haja ya kuyakazia kwa mujibu wa katiba inapokuja.

Kwamba ni matamko ya nia njema yaliyomo katika tunayoyapambania kwenye katiba mpya, hayawezi kuwabagua wanaoshikiliwa pasipokuwa na ushahidi wa kutosha.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Kutawala kwa katiba 100% ni theory maana hakuna katiba yenye ufanisi 100%, hilo gap ndio huwa linafidiwa na msuli sasa. Ishi kwa practical hiyo na utakuwa salama
Ninakazia, utawala ni kwa mujibu wa katiba. Haipo % wala allowance ya u-shamba wa bibi.
 
Nimeshangazwa sana na hii habari, mtuhumiwa anashikiliwa gerezani zaidi ya miezi 7 lakini kila siku upande wa mashtaka wanadai upelelezi haujakamilika, sasa kwanini walimkamata?

Inavyoonekana, mashtaka wanayomtuhumu nayo yenye uzito ni yale ya kuwafanyia fujo polisi siku waliyoenda kumkamata, kinyume na hapo hakuna mashtaka mengine ya maana waliyonayo, ndio maana kila siku upelelezi bado haujakamilika.

Haya mambo yanaonesha tulivyo na mfumo mbovu wa kimahakama, ajabu hakimu anatakiwa kuwapa upande wa mashtaka angalizo, kesi ikiitwa tena mahakamani upelelezi ukiwa bado haujakamilika mshtakiwa aachiwe huru.
Kwanza ipo wazi

Polisi, Mahakimu na Majaji wa Nchi hii wana kawaida ya ku ba ka na ku la wi ti Sheria zilizotungwa na Bunge (ashakum sio Matusi) kwanini nasema hivyo?

Soma Criminal Act (Sheria ya Makosa ya Jinai) inasemaje au Penal Code (Kanuni ya Adhabu) inasemaje kuhusu mashitaka km haya hapo ndio utagundua nini kinaendelea

Juzi kuna Daktari kabaka na kulawiti mtoto wa miaka 17 ila kaachwa kwa dhamana ya million 5 na wadhamini wawili, sasa kuna nini kwa huyu mama?

Kuna Jambo limefichwa sio bure kuna sababu nyingine sio hio ya kupigana na Polisi akiwa nyumbani kwake sio sababu

Sababu ni kujiona yeye ni Mfalme na kujiona yeye ni MUNGU mwanamke kosa jingine ni kuendesha ibada tofauti au kinyume na taratibu za kidini

Kwa hio hilo kosa kabambikiwa na kumshikiria kwa namna nyingine ni kumpotezea upepo wake na wafuasi wake hakuna MUNGU mwanamke wala Mfalme mwanamke

Anashikiriwa sababu yale aliyokua anayafanya ni Chukizo kwa jamii na inapingana na imani zingine za kidini

Serikali inamlinda isije jamii ikachukua sheria mkononi ndio maana wanamshikiria hadi pale vuguvugu lake litapoisha ndio watamwachia

Anajiitaje yeye MUNGU?
Anajiitaje yeye Mfalme? tena Mfalme mwanamke kinyume na tamaduni zetu

Mtoa mada emu fafanua na hapo
 
Kwanza ipo wazi

Polisi, Mahakimu na Majaji wa Nchi hii wana kawaida ya ku ba ka na ku la wi ti Sheria zilizotungwa na Bunge (ashakum sio Matusi) kwanini nasema hivyo?

Soma Criminal Act (Sheria ya Makosa ya Jinai) inasemaje au Penal Code (Kanuni ya Adhabu) inasemaje kuhusu mashitaka km haya hapo ndio utagundua nini kinaendelea

Juzi kuna Daktari kabaka na kulawiti mtoto wa miaka 17 ila kaachwa kwa dhamana ya million 5 na wadhamini wawili, sasa kuna nini kwa huyu mama?

Kuna Jambo limefichwa sio bure kuna sababu nyingine sio hio ya kupigana na Polisi akiwa nyumbani kwake sio sababu

Sababu ni kujiona yeye ni Mfalme na kujiona yeye ni MUNGU mwanamke kosa jingine ni kuendesha ibada tofauti au kinyume na taratibu za kidini

Kwa hio hilo kosa kabambikiwa na kumshikiria kwa namna nyingine ni kumpotezea upepo wake na wafuasi wake hakuna MUNGU mwanamke wala Mfalme mwanamke

Anashikiriwa sababu yale aliyokua anayafanya ni Chukizo kwa jamii na inapingana na imani zingine za kidini

Serikali inamlinda isije jamii ikachukua sheria mkononi ndio maana wanamshikiria hadi pale vuguvugu lake litapoisha ndio watamwachia

Anajiitaje yeye MUNGU?
Anajiitaje yeye Mfalme? tena Mfalme mwanamke kinyume na tamaduni zetu

Mtoa mada emu fafanua na hapo

Hii hapa inaitwa machozi ya mamba:

"Serikali inamlinda isije jamii ikachukua sheria mkononi ndio maana wanamshikiria hadi pale vuguvugu lake litapoisha ndio watamwachia."

Kwani Zumaridi kawaomba ulinzi wa aina hii unayoiongelea mkuu? Siyo kuwa wanamshikilia kinyume na utashi na dhamira yake?
 
Back
Top Bottom