Upelelezi uliofanywa kwa kampuni ya kituruki na uwaguse wawekezaji wote wapya

Upelelezi uliofanywa kwa kampuni ya kituruki na uwaguse wawekezaji wote wapya

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Rais Samia aliongea kwa ukali pale bandarini siku ya tarehe 4 mwezi huu wa Desemba. Sina uhakika kama wasaidizi wake walimtegemea kumsikia akiongea kwa kujiamini kiasi kile. Ni kama vile Rais ameanza kutanua makucha yake. Ule muda wa honeymoon ya miezi ya kutambuana kati yake na wasaidizi wake imeshamalizika.

Akamwaga kila kitu hadharani na kuelezea kwa kirefu namna kampuni ya kituruki ilivyogundulika kuwa ni ya madalali na sio yenye uwezo wa kufanya kazi iliyoajiriwa kuifanya. Mpaka kuja kuigundua kampuni hiyo kuwa haina uwezo tayari mikataba ilishaandikwa na kusainiwa mbele ya watu.

Lipo somo la kufanyiwa kazi kwa upande wa serikali. Isiwe ni suala rahisi tu kujivunia kuleta wawekezaji wapya. Isiwe ni kama sifa hivi kwa viongozi wenye mamlaka ya uwekezaji kutaja namba mpya ya wawekezaji walioweza kupatikana ndani ya kipindi fulani.

Kilichofanyika kwa kampuni ya kituruki na kifanyike kwa makampuni yote yanayotarajia kupewa tenda kubwa kubwa. Tusizuzuke tu na rangi za ngozi zao, tusidanganyike tu na masuti pamoja na vitambi vyao, twende mbali zaidi katika kuhakikisha uhalali wa hiyo mikataba tunayoingia. Sio kila anayekuja kuitikia wito wa ziara za Rais wetu huko nje na ujumbe wake, anayo nia njema kwa taifa letu.

Hawa watu hawatupendi kama tunavyojidanganya kama wanatupenda. Wengine wanatuona kama wajinga ambao wamechelewa kutambua ukubwa wa rasilimali walizonazo. Wengine wana hulka tu za kitapeli wamezoea kukusanya utajiri kwa njia haramu.

Hivyo ni jukumu letu la kwenda taratibu na kwa umakini tunapojiandaa kusaini mikataba na wawekezaji.
 
Bongo unaweza kuwekeza kwa maneno, ila cha msingi ujue lugha vizuri na suti kali kali pia ufikie hape kempisk the kilimanjaro. sasa wakishakupa vibali vyote na leseni ndiyo unakwenda kutafuta hela kwenye mabenki ya nje ama ya ndani uwekeze.

Mwekezaji si hela kama tunavyofikiri tulio wengi, na ndiyo maana Mwalimu alituasa tufanye haya mambo wenyewe na si kuwapa hawa mtu kati.
 
hii nchi inaonekana kuna maeneo tumeweka watoto ( non-matured) tunapigwa kifala sana..

Yaani mtu anakaa kati mnampa tenda ya kujenga meli kadhaa from nowhere yaani mhuni tu, waturuki tu wahuni... Eti Richmond kamati ya Bunge ndio wanakwenda kutafuta ofisi ya Dowans pale Dubai, pale stanbic wale wakwe zake EL eti wakaanzisha kafirm kakutushauri wakapiga hela wakati tumeenda kukopa stanbic....Wakaji wale wahuni wakenya kwenye Korosho na PJ wakatupiga kimyakimya mchana kweupeee...mbona sisi mafala sana, hata kama watu wetu ndio mnaiba kwa kushirikiana nao mtambue mnaiba kijinga sana....na binafsi nikiwa Rais nitafukua mpaka makaburi yenu na kuichoma mifupa moto pamoja na kufilisi vizazi vyenu.....

yaani kuna ujinga unatokea kiasi kwamba ukichukua tu laptop masaa mawili ukaingia kazini unajua kabisa hapa kuna usanii aka upigaji...TUACHENI UFALA, TAIFA LINA WATU MASIKINI KWA SABABU YA UJINGA WENU PUMBAVU NYIE....

Dunia imeshajua, Kule Africa kuna Taifa la watu wapumbavu basi wanakuja tu hapa kila kukicha, waarabu,wahindi na wazungu tunao miaka yote Waturuki wanamiminika kila siku, waegypt nao wamegundua chaka wanaanza kumiminika.... ndugu zetu wakenya weusi wenzetu nao wanatuzidi akili wanaweka kambi hapa kila siku.. TUACHENI UPUMBAVU SASA....
 
Bongo unaweza kuwekeza kwa maneno, ila cha msingi ujue lugha vizuri na suti kali kali pia ufikie hape kempisk the kilimanjaro. sasa wakishakupa vibali vyote na leseni ndiyo unakwenda kutafuta hela kwenye mabenki ya nje ama ya ndani uwekeze.

Mwekezaji si hela kama tunavyofikiri tulio wengi, na ndiyo maana Mwalimu alituasa tufanye haya mambo wenyewe na si kuwapa hawa mtu kati.
Umeongea issue ya maana sana ambayo nafikiri watu wengi hawaijui, kuna Bank nyingi sana zina pesa kibao zinasubiri watu waje wakope wafanye kazi, tatizo wakiangalia wengi ni wababaishaji tuu, naamini ukiwa na solid plan inayoeleweka pesa zitapatikana tuu
 
Back
Top Bottom