Upendo wa kweli kwa Wanawake umeondoka haupo tena

Upendo wa kweli kwa Wanawake umeondoka haupo tena

Kumejengeka kizazi lia lia jamani yani vijana wa kiume kidogo tu vilio.....hadi nawaza sijui ni hizi staili mupya mupya za kubebea mimba ndio chanzo!!!!! Ndio maana zamani ilikua ni missionary tu wazee walikua na maana
Hiki kizazi Mungu tu akiokoe, sio bure kuna mahali tunakosea. Vitoto vya kiume vimekuwa nyoro nyoro sana.
 
Sababu familia ya mwanamke inakuwa imelose na familia ya mwanaume inakuwa imegain, occasionally mwanamke atatumia jina la ukoo la mwanaume, na watoto wenu pia watatumia jina la ukoo la mwanaume na si la mwanamke

Ndio maana kwa wazungu ni kawaida kukuta watoto wanatumia majina ya koo zote mbili za wazazi wao, sababu hawana utaratibu wa mahari lakini huku kwetu ni ajabu kufanya hilo, sasa mwanamke akianza kujilipia mahari inakuwaje hapo

Halafu mbona hela za kuhonga wanawake wa kuwaondolea upwiru kabla hamjaoa huwa mnazo, ila mkitaka tu kuoa ghafla hamna hela, ni kinyume na tamaduni za kiafrika mwanamke kujilipia mahari fanya ufanyavyo umlipie mahari mtoto wa watu

1. Siwezi na sijawahi kuhonga na zitakuja kuhonga.

2. Watu wawili wanapoenda kuanzisha familia yao hakuna ukoo au upande wowote unaoloose. Hizo ni imani na mila potofu.

3. Sio lazima mwanamke atumie jina la ukoo wa mwanaume na wala sio lazima watoto watumie majina yenu.

4. Kutoa mahari ni biashara ya kuzalilisha na kumfanya Mwanamke kama bidhaa.

Siwezi kutoa mahari kamwe kwaajili ya kununua mtu ambaye amenipenda na nimempenda mwenyewe. Tumekubaliana kwa hiyari yetu.

Wazazi shughuli yao/yetu inaishia pale mtoto akishaweza kujitegemea. Mambo ya ndoa au mahusiano ya mtoto hayatuhusu/hayawahusu.

Unapoingiza mambo ya ku-gain au ku-loose ndio unaingiza Biashara badala ya upendo. Na hapo ndipo chanzo cha ndoa kuitwa utapeli, wizi na unyonyaji. Kwa sababu ni biashara.

Vijana wote hasa wenye akili za kitibeli ambao kuanzia karne ya 22 watakuwa wengi hawatafanya huo upuuzi na utaonekana ulikuwa ni mila za kishenzi
 
Kwa kweli mi naacha kuchangia harusi, naona ni upuuzi mtupu, bora wachukuane hivyohivyo ili wakishindwana waachane kimyakimya. Haiwezekani watu watu waoane kwa gharama kubwa halafu muda mfupi waachane kizembe kisa mume kaishiwa hana hela na mke kumoana si chaguo lake kisha kuanza harakati za kujitoa kwenye ndoa kwenda kutafuta mwanaume mwingine mwenye hela. Sasa hapo upendo uko wapi?
 
Upendo umepungua ndio ila sio kwa kujilipia mahari...

Acha kukwepa majukumu yako mwanaume...
Japo hunaga zambi ila unajichanganya sana na sisi wasadukayo ,kwa hilo tu nakupenda sana dada yangu[emoji3059][emoji3059][emoji3059]
 
Usisubiri kupendwa utakuwa too disappointed

Kama una hela hakikisha una spend wisely kula chakula Bora Sana lala Sehemu Nzuri Sana wasiliana na watu wako wote muhimu

Binadamu wengi hawajui huwa wanahitaji kitu gani kutoka kwa watu hivyo usijitwike mzigo mkubwa wa kutaka kupewa UPENDO utajiumiza Sana
Neno hili
 
Ukiyumba tu hata kama mlianza vizuri kwisha habari yako mke anakimbia.
mitaani siku hizi kuna wanawake wengi mno waliowakimbia waume zao kisa kuishiwa hela, ramani za hela zimewagomea. Wanazurura hovyo hovyo wakilaghai wanaume hawajaolewa. Bodaboda na waume za watu wenye chenji wanawafaidi sana hawa wanawake kwa hela ndogo za mboga za majani. Ni washenzi wakisikia waume zao ramani na michongo ya hela inasoma vizuri wanajirudisha kwa gia ya rivasi hata kama waume zao tayari wameoa wake wengine. Utawahurumia tu kwa jinsi walivyopaukiana na kukosa wa kuwaoa.
 
U
Hili jambo nimelithibitisha kwa watu wengi walio katika mahusiano hasa yale yakuanza na NDOA kisha ndio waishi pamoja.

Sisemi mahari ni nzuri au mbaya ila Mahari ni kipimo kikubwa sana kilichonifanya nije na huu uzi.

Nimeuliza wanawake zaidi ya 10 swali 1 ambalo ni

Je, Mpenzi wako akikosa mahari akaomba umsaidie kumlipia yani umpe hela aje kukulipia utafanya hivyo?

Kati ya wote waliokataa na kusema hawawezi ni 9/10 na katika hao ni 1/10 tu ndio ameweza kukubali kulipia mwanaume wake mahari.

Ukweli mahari ni jambo la mwanaume lakini hivi kama kweli lengo lenu ni 1,nia yenu ni 1 kuna shida gani mwanamke ukimsaidia mwanaume mahari au kumpa hela akakulipie kama Uwezo huo unao?

Imagine mimi ni kijana nina kauwezo kadogo namuoa mwanamke kama ZARI natakiwa kumlipia Mahari ZARI wakati uwezo kanizidi kila eneo hivi mapenzi hapa yako wapi?

Kwa upande wangu mahari ni sawa lakini wanawake wasioweza wapa waume zao mahari au wasaidia kulipa mahari sioni kama wanaupendo wanaweza badilika na kuwa chochote huko mbeleni.

Ni heri hawa wanawake wa Sogea Tuishi kweli wale wanaupendo lakini hawa wa Nenda kwetu kajitambulishe wanangu tunapigwa...

Sisapoti sogea tuishi ila nasema kwamba wanawake wanaopenda process zifatwe hawana upendo wa kweli kama wale wa sogea tuishi.

Kanitoleee mahari kama kweli unanipenda, siendi sasa. Majini nyie hamna upendo mnatuigizia.

shwaaaaaaa....
Uzi wako umeanza vizuri ila kadiri unavyozidi unatushusha hadhi wanaume... Unamiaka mingapi mkuu...??
 
Usisubiri kupendwa utakuwa too disappointed

Kama una hela hakikisha una spend wisely kula chakula Bora Sana lala Sehemu Nzuri Sana wasiliana na watu wako wote muhimu

Binadamu wengi hawajui huwa wanahitaji kitu gani kutoka kwa watu hivyo usijitwike mzigo mkubwa wa kutaka kupewa UPENDO utajiumiza Sana
Uko sahihi.
Bila kusahau kumpenda Mungu kwa moyo wako wote.
 
1. Siwezi na sijawahi kuhonga na zitakuja kuhonga.

2. Watu wawili wanapoenda kuanzisha familia yao hakuna ukoo au upande wowote unaoloose. Hizo ni imani na mila potofu.

3. Sio lazima mwanamke atumie jina la ukoo wa mwanaume na wala sio lazima watoto watumie majina yenu.

4. Kutoa mahari ni biashara ya kuzalilisha na kumfanya Mwanamke kama bidhaa.

Siwezi kutoa mahari kamwe kwaajili ya kununua mtu ambaye amenipenda na nimempenda mwenyewe. Tumekubaliana kwa hiyari yetu.

Wazazi shughuli yao/yetu inaishia pale mtoto akishaweza kujitegemea. Mambo ya ndoa au mahusiano ya mtoto hayatuhusu/hayawahusu.

Unapoingiza mambo ya ku-gain au ku-loose ndio unaingiza Biashara badala ya upendo. Na hapo ndipo chanzo cha ndoa kuitwa utapeli, wizi na unyonyaji. Kwa sababu ni biashara.

Vijana wote hasa wenye akili za kitibeli ambao kuanzia karne ya 22 watakuwa wengi hawatafanya huo upuuzi na utaonekana ulikuwa ni mila za kishenzi
So Mkuu hujawahi kabisa kutoa hela kwa ajili ya mbususu? Na kwanini? Hapa sijamaanisha wale dada poa.
 
Kwa kweli mi naacha kuchangia harusi, naona ni upuuzi mtupu, bora wachukuane hivyohivyo ili wakishindwana waachane kimyakimya. Haiwezekani watu watu waoane kwa gharama kubwa halafu muda mfupi waachane kizembe kisa mume kaishiwa hana hela na mke kumoana si chaguo lake kisha kuanza harakati za kujitoa kwenye ndoa kwenda kutafuta mwanaume mwingine mwenye hela. Sasa hapo upendo uko wapi?
Alafu we ni Mkristo ujue.
Mahari ndio njia sahihi ambayo Mungu wa Wayahudi wa zamani ambaye ni Mungu wa Wakristo kwa sasa ameidhinisha kwa wanadamu kuhalalisha mahusiano kati ya mke na mume.
 
Sasa kama mnafahamu hilo nafikiri badala ya kulaumu wanawake tuanze kulaumu wazazi ambao bado wanaamini tamaduni hizo maana hata wanawake nao ni victims tu wa hizo imani, kuna makabila hadi leo binti akisema anataka akaolewe tu bila mahari kisa kampenda mwanaume ukoo mzima wanashika vichwa, na kifuatacho ni vikao visivyoisha vya kuwasema binti pamoja na wazazi au walezi wake

Naelewa unazungumzia nini.
Wanawake ndio wahanga wakubwa wa hizo mila sema wengi hawajui kwa sababu hawana macho ya kuona Mbele.

Mími silaumu mabinti wala silaumu wazazi. Nitajilaumu mwenyewe ikiwa nitafanya jambo ambalo ninaona kabisa hili ni uongo, unyanyasaji, ukandamizaji wa haki za ninayempenda na anayenipenda.

Siwezi kutoa mahari. Hiyo ni moja.
Pili ninatafuta mwanamke ambaye anamuona na mtazamo kama wangu. Sitaki kumuumiza mtu kisa mtazamo na mila na desturi zao.
Yeye kama anataka kutolewa mahari basi nitamuacha atafute wanaume wenye mitazamo na muono wa aina hiyo.

Nimeshuhudia mamia ya wanaume wanaonyanyasa wake zao kwa kisingizio cha kutolewa Mahari.
Nimeona mamia ya wanawake waliolaghaiwa kutolewa mahari kwa kudanganywa kisha wakaachwa Solemba.

Nimesikia na kuona maelfu ya wanaume wakilalamika kuhusu kutoa mahari wengine ni kubwa wengine ni ndogo. Mara sijui mahari huimalizi yaani mambo ya ajabu sana.

Binti yangu kamwe sitachukua mahari kama ambavyo mimi sikutoa mahari nilipomchukua Mama yake.

Umepata Mwanamke, mmeelewana. Kinachofuata ni kwenda kutambulishana nyumbani kwa Mwanamke na kwa mwanaume. Maswala ya pesa sijui mahari sijui wanipangie sijui niwapangie huo upuuzi haufanyiki.
Ni mambo ya aibu.

Yaani Watu wazima na akili zenu mnakaa mnapanga ati binti yetu mahari iwe ngapi? Kweli!

Huko tunapoenda itafahamika mbivu na mbichi. Mambo yote ya kijinga yatapuuzwa. Ukweli utashinda. Na uongo uongo wa kizamani utajitenga
 
So Mkuu hujawahi kabisa kutoa hela kwa ajili ya mbususu? Na kwanini? Hapa sijamaanisha wale dada poa.

Siwezi kuhonga mimi.
Yaani nitoe pesa nipate ngono au penzi. Hilo sijawahi na sitokuja kufanya.

Siwezi mhonga Mwanamke anayenipenda na ninayempenda.
Yaani nimpe mtu hela ili afanye wajibu wake.

Au unazungumzia kufanya zinaa, kum-cheat mpenzi wangu?
 
Usisubiri kupendwa utakuwa too disappointed

Kama una hela hakikisha una spend wisely kula chakula Bora Sana lala Sehemu Nzuri Sana wasiliana na watu wako wote muhimu

Binadamu wengi hawajui huwa wanahitaji kitu gani kutoka kwa watu hivyo usijitwike mzigo mkubwa wa kutaka kupewa UPENDO utajiumiza Sana

Vizur
Toa sadaka
Wakumbuke wasiojiweza
Mengine ni ziada
Kusanya kibunda kula maisha

Ikiwa utahisi unahitaji kuowa owa
Ukiona hauna hitaji hilo achana nalo
Kula life
 
Siwezi kuhonga mimi.
Yaani nitoe pesa nipate ngono au penzi. Hilo sijawahi na sitokuja kufanya.

Siwezi mhonga Mwanamke anayenipenda na ninayempenda.
Yaani nimpe mtu hela ili afanye wajibu wake.

Au unazungumzia kufanya zinaa, kum-cheat mpenzi wangu?
Nazungumzia kuhonga mkuu. Sio kucheat.
 
Back
Top Bottom