Upi mtazamo wako kukithiri kwa mada zinazochochea chuki za kidini jukwaani

Upi mtazamo wako kukithiri kwa mada zinazochochea chuki za kidini jukwaani

Mtoa mada umeandika kitu cha msingi Sana...Kwa kusema kweli hata Mimi ni mfia dini lakini natishwa na kiwango cha kukashfiana,,kudharauliana na husda vilivyoongezeka Sana humu jukwaani baina ya wakristo na waislam...
Sometimes Huwa nawaza Labda kuna mtu au kikundi cha watu wanatuchonganisha...au Sisi wenyewe tumekiwa mahasidi Sana....Kuna vitu watu humu jukwaani wanaandika pasipo woga lakini vinaharibu umoja ukaribu na hata tolerance...,.Tu jiulize sana wafia dini humu na tubadilike wote........Tujue kwamba huu mchicha tunaoupanda tutakuja kufa tuuache ukiwa mbuyu na hakuna wa kuweza kuung'oa,,,,,,Kingine hata kama ni mwenzetu katika dini analeta kashfa tumuangalie kwa makini asijekuwa anatutumia kwa maslahi flani.....Tuwe na hekima ya kufikiria vizuri katika mijadala yetu tumshinde shetani.
Ahsante sana mkuu
 
Nimewaza nikuweke kwenye corner utuambie ni vitabu vya dini Gani vinasema hivyo. Nikapoteza ila nimeshtuka Umeamua kuniuliza. Unanguvu Gani za Kiroho? Au imetokea tu? 🙄🙄
😂 mind reader
 
bro nimeshuhudia mada ambazo mtu analeta swali kama kuchochea tu mjadala hata anapojibiwa unaona kinachofuata ni ubishi na kuanza kum attack mtu personally, binafsi na appreciate pale watu wanapojadiliana kwa hoja makini na kukubaliana hata pale wasipokubaliana.take ur time pitia nyuzi zinazoanza na kuuliza swali la kidin uone mwisho wa siku mjadala ulielekea wap?
ni vema ukafahamu aina ya mijadala ambayo haina hitimisho, ingawa ni muhimu zaidi ikiwa wanaojadiliana wakawa na sense of peace in minds, kitu ambacho hata kama hawajakubaliana lakini wanaishia kua na peace of mind 🐒
 
So tuendelee kuitana makafiri,wavaa kobazi n.k si ndio ? Unavyoona hiyo mijadala ina tija gani ?
Unaujua utani.
Utani inaitwa jina lolote lile na isikasirike.
Hii ndio jamii iliyostarabika katika nyakati za Leo.
Sisi hatukasilika kuitwa Wagalatia au Makafiri.
Tunauchulia kama utani tu basi.
Mimi nina ndugu wa damu Waislamu na sijawahi kuwakebehi.
Kwani wewe ukiitwa Kobazi Kuna shida gani?
Kwani wewe ni Kobazi hadi ukasirike.
Mada za Kidini ni za kutaniana tu, na kama unazichukulia kwa usiriazi basi na ujiondoe tu.
 
Unaujua utani.
Utani inaitwa jina lolote lile na isikasirike.
Hii ndio jamii iliyostarabika katika nyakati za Leo.
Sisi hatukasilika kuitwa Wagalatia au Makafiri.
Tunauchulia kama utani tu basi.
Mimi nina ndugu wa damu Waislamu na sijawahi kuwakebehi.
Kwani wewe ukiitwa Kobazi Kuna shida gani?
Kwani wewe ni Kobazi hadi ukasirike.
Mada za Kidini ni za kutaniana tu, na kama unazichukulia kwa usiriazi basi na ujiondoe tu.
Lakini una uhakika majibishano huwa yanaishia kiutan utan kwa kila mtu maana kipimo cha uvumilivu au kuhimili kejeli na utani hakifanan kwa watu wote
 
Watu wasizibwe midomo na wala hauwez kuwaziba midomo tunahitaji wana jamii forum tuwe mfano mzuri wa kuendesha mijadala isiyohamasisha chuki/ kejeli kwa imani nyingine , kwenye mifano ya machafuko hapo nimetaja Afrika ya kati i hope unafaham historia vzr .
Ungetoa Mifano ya Chuki Unayoipinga Tukaona Kama Mod Wana kazi ya Kufanya Au Laah
 
Hakuna uhuru usio na mipaka.
JF yenyewe wamekuekea code of ethics, wenyewe wanaziita principles. Au hujaona watu wakila ban humu.
Nadhan tatizo linaanzia kwenye nadharia ya jukwaa huru kuna kauli inasema ,"uhuru wako unapoishia ndipo heshima ya mwingine inapoanzia."
 
Back
Top Bottom