Kama kinachosemwa ni ukweli basi Hazina lazima ndo itakaushwa kabisa.Yaani bado kuna watu wanapiga serikali ya Jon?
Si bora hata hao wanao kwepa hizo kodi maana wametafuta kwa jasho lao. Vipi kuhusu Wanasiasa wanao zitumia hizo kodi kununulia Ma V8?Aisee kwenye vyoo vya uma watu wanapiga sana hawatoi risit na wala sio hapo Busisi tu japo hapo ni kawaida yao, nenda choo cha stendi ya Igombe pale mambo ni yaleyale hawatoi risit na usipouliza ndio kabisa hawakupi, na kwenye maduka nayo siku hizi yapo baadhi yanato risit ambazo zinaonesha kiasi cha pesa ulichotumia kununulia bidhaa ila kiasi cha kodi kilichokatwa hakipo sasa haya mambo nayo wanatakampaka Rais aje aseme.
Yaani unalalamika pesa ya choo kwani shs ngapi mkuu umelipa?Kuna wizi unaendelea siku ya 3 Leo kivuko cha busisi Mwanza. Wananchi wanalipia huduma ya Choo bila receipt wala machine siku ya 3 sasa. Watu wanatoa km sadaka kanisani. Nimejaribu kuuliza kwanini hawatoi receipt wala mashine nimeambiwa ni maelekezo kutoka ofisi ya TEMESA.
Pia, nimemuuliza kijana anaekusanya hizi pesa anithibitishie jinsi gani pesa zote zitafika sehemu husika. Amesema atafikisha kwa sababu anaaminika.
Tunaomba Serikali ichukue hata za haraka kuzua wizi huu.