Upimaji wa ardhi ya makazi ni muhimu Ili kuepusha majanga

Upimaji wa ardhi ya makazi ni muhimu Ili kuepusha majanga

Lotus 123

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2021
Posts
3,151
Reaction score
5,513
Ni vyema vijiji vipimwe na kufanyiwa tathimini kama ardhi yake inafaa Kwa makazi na shughuli za kibinadamu,Kuna baadhi ya maeneo watu wanaishi kwenye mabonde au karibu na Kingo za mito,Kuna maeneo ambayo kimsingi hayafai Kwa ajili ya makazi lakini mamlaka zipo kimya.Tusingojee mpaka majanga yatokee ndio tuanze kulaumiana.
 
Ni vyema vijiji vipimwe na kufanyiwa tathimini kama ardhi yake inafaa Kwa makazi na shughuli za kibinadamu,Kuna baadhi ya maeneo watu wanaishi kwenye mabonde au karibu na Kingo za mito,Kuna maeneo ambayo kimsingi hayafai Kwa ajili ya makazi lakini mamlaka zipo kimya.Tusingojee mpaka majanga yatokee ndio tuanze kulaumiana.
Alijaribu Mwl. Nyerere na Vijiji vya ujamaa tukamuona hayawani. No Tanzania pekee mpaka ipitisbe sensa ndio ijue watu wake ni wangapi na wako wapi.

Taifa linahitaji sio tu kujua Lina watu wangapi, linapaswa kujua wako wapi, mahitaji yao specific kwa muda wa miaka mitano, kumi na ishirini na tano ni yepi au yatakuwa yepi.

Tunahitaji kujua wamekaaje ndani ya miji au Vijiji vyao, mtawanyiko wa huduma ukoje na utakuwaje kwa baadae. Ikitolea Kijiji kimekuwa sana huduma mpya muhimu zitakwenda wapi ili ziboreshe Mji na sio kuweka pembeni na kuua miji ya asili au chimbuko.

Tunahitaji kujua namna ya kupanga maji yetu, tukianza na maji ya Mvua, ili kuboresha ikolojia ya maeneo ya miji yetu na Hali ya hewa kwa ujumla. Tunahitaji kuboresha miundombinu kama ya maji safi, maji taka, barabara na taka ngumu ili kuchagiza ujenzi wa compact cities. Sio kuatwanyika hovyo tuu mijini ambayo inaathiri gharama za Usimamizi wa miji, na gharama za maisha kwa wakazi wa miji.

Yooote haya ni zao la mipango miji. Mipango miji ni kama Hakimu mahakamani, au refa uwanjani. Japo majina makubwa ni ya mawakili na washitaki kwenye kesi ila kesi ni nzuri tu ikiwa Hakimu ni mzuri. Au wachezaji wa pande mbili, makocha na mashabiki wanaweza kupata sifa kubwa sana ila yote yamewezekana tuu kwasababu Yuko refa au mwamuzi aliyelinda Haki za wote kufurahi.

Kwa kweli kama serikali utaendelea na utaratibu wa kufanya urasimishaji...yaani KUPOKEA maamuzi ya wananchi( uninformed decisions) za kuanzisha miji kiholela na kuzifanyabiuwa formal decisions kuyashinda majanga haya ni ndoto. Na zaidi huko mbeleni tutaona majanga ambayo hatujawahi kamwe kuyaona. Maana haya mazinholela yatakomaa kwenye maeneo hatarishi na Matokeo ya majanga kwenye maeneo hayo baadae yatakuwa ni ya kutisha.

Kwenye hili wananchi lazima wajue matown planner kazi yao ni kuwasaidia kujenga mifumo ya kulinda maslahi yao kwenye matumizi ya Ardhi, na sio kuwapangia ni Cha kufanya. Ila Hilo kutokuwapangia lisifananishwe na kuwapa ruhusu wananchi kuamua tuu kama wanavyotaka, la hasha ila ni kumaanisha kusikiliza matown planner wakiwashauri kwa kuwapa na njia mbadala ya kutumia Ardhi zao kwa namna ambayo sio hatarishi kwao na kwa wengine bila kupoteza uwezo wa kujipatia kipato stahiki.

Ninaliombea taifa hili Leo na kesho yake ikawe yenye heri. Na naliombea kama halitaweza kupata wanasiasa wanaowapenda na kuwatakia mema, angalau lipate wanasiasa wenye kiburi na shauku ya kufanya mambo sawa sawa ikiwemo kupanga miji itakayo shinda majaribu ya muda.
 
Ni vyema vijiji vipimwe na kufanyiwa tathimini kama ardhi yake inafaa Kwa makazi na shughuli za kibinadamu,Kuna baadhi ya maeneo watu wanaishi kwenye mabonde au karibu na Kingo za mito,Kuna maeneo ambayo kimsingi hayafai Kwa ajili ya makazi lakini mamlaka zipo kimya.Tusingojee mpaka majanga yatokee ndio tuanze kulaumiana.
Serikali yetu haipimi ardhi ili kuwakinga wananchi na majanga, bali hufanya hovyo ili kujipatia maokoto.
 
Naona wasomi mnashusha midesa hapa ya maana.

Changamoto ya wasomi ni njaa.

Mkishalamba asali mnaziacha taaluma zenu na kujivika viburi vya fedha.
 
Naona wasomi mnashusha midesa hapa ya maana.

Changamoto ya wasomi ni njaa.

Mkishalamba asali mnaziacha taaluma zenu na kujivika viburi vya fedha.
Ni wasomi wa aina gani unamaanisha?

Maana usikute unamaanisha wasomisiasa
 
Alijaribu Mwl. Nyerere na Vijiji vya ujamaa tukamuona hayawani. No Tanzania pekee mpaka ipitisbe sensa ndio ijue watu wake ni wangapi na wako wapi.

Taifa linahitaji sio tu kujua Lina watu wangapi, linapaswa kujua wako wapi, mahitaji yao specific kwa muda wa miaka mitano, kumi na ishirini na tano ni yepi au yatakuwa yepi.

Tunahitaji kujua wamekaaje ndani ya miji au Vijiji vyao, mtawanyiko wa huduma ukoje na utakuwaje kwa baadae. Ikitolea Kijiji kimekuwa sana huduma mpya muhimu zitakwenda wapi ili ziboreshe Mji na sio kuweka pembeni na kuua miji ya asili au chimbuko.

Tunahitaji kujua namna ya kupanga maji yetu, tukianza na maji ya Mvua, ili kuboresha ikolojia ya maeneo ya miji yetu na Hali ya hewa kwa ujumla. Tunahitaji kuboresha miundombinu kama ya maji safi, maji taka, barabara na taka ngumu ili kuchagiza ujenzi wa compact cities. Sio kuatwanyika hovyo tuu mijini ambayo inaathiri gharama za Usimamizi wa miji, na gharama za maisha kwa wakazi wa miji.

Yooote haya ni zao la mipango miji. Mipango miji ni kama Hakimu mahakamani, au refa uwanjani. Japo majina makubwa ni ya mawakili na washitaki kwenye kesi ila kesi ni nzuri tu ikiwa Hakimu ni mzuri. Au wachezaji wa pande mbili, makocha na mashabiki wanaweza kupata sifa kubwa sana ila yote yamewezekana tuu kwasababu Yuko refa au mwamuzi aliyelinda Haki za wote kufurahi.

Kwa kweli kama serikali utaendelea na utaratibu wa kufanya urasimishaji...yaani KUPOKEA maamuzi ya wananchi( uninformed decisions) za kuanzisha miji kiholela na kuzifanyabiuwa formal decisions kuyashinda majanga haya ni ndoto. Na zaidi huko mbeleni tutaona majanga ambayo hatujawahi kamwe kuyaona. Maana haya mazinholela yatakomaa kwenye maeneo hatarishi na Matokeo ya majanga kwenye maeneo hayo baadae yatakuwa ni ya kutisha.

Kwenye hili wananchi lazima wajue matown planner kazi yao ni kuwasaidia kujenga mifumo ya kulinda maslahi yao kwenye matumizi ya Ardhi, na sio kuwapangia ni Cha kufanya. Ila Hilo kutokuwapangia lisifananishwe na kuwapa ruhusu wananchi kuamua tuu kama wanavyotaka, la hasha ila ni kumaanisha kusikiliza matown planner wakiwashauri kwa kuwapa na njia mbadala ya kutumia Ardhi zao kwa namna ambayo sio hatarishi kwao na kwa wengine bila kupoteza uwezo wa kujipatia kipato stahiki.

Ninaliombea taifa hili Leo na kesho yake ikawe yenye heri. Na naliombea kama halitaweza kupata wanasiasa wanaowapenda na kuwatakia mema, angalau lipate wanasiasa wenye kiburi na shauku ya kufanya mambo sawa sawa ikiwemo kupanga miji itakayo shinda majaribu ya muda.
Kwa suala zima la Mipangomiji na Upimaji wa Ardhi, Serikali yetu imeshindwa vibaya sana, naweza nikasema kwamba imeshindwa kwa kishindo kwa takribani 98%.
Kuna KIFO cha taaluma ya Mipangomiji nchini Tz.
 
Kwa suala zima la Mipangomiji na Upimaji wa Ardhi, Serikali yetu imeshindwa vibaya sana, naweza nikasema kwamba imeshindwa kwa kishindo kwa takribani 98%.
Kuna KIFO cha taaluma ya Mipangomiji nchini Tz.
Mipango miji kwa sehemu ni zoezi endelevu na lenye mrengo wa kisiasa.

Shida kubwa inakuja wanasiasa wanapoegemea Siasa zaidi na kukosa maono ya baadae huku wananchi wamekosa uvumilivu na subira na hawana dira Matokeo yake tunakwenda kama hayawani.

Chakusikitisha mipango miji si kipaumbele... Maana taaluma nyingi kama Wajenzi, Wasanifu Majengo na wanasiasa kwa Sasa Wana uhuru ambao Matokeo yake ni Kuna mengi yanafanyika ila hakuna continuity na collaboration kuhakikisha tunafikia lengo la kumkomboa Mtanzania.

Town planner kazi yake ni kuharmonize scramble for use of land and other natural resources mijini kwa namna ambayo inaleta tija kwa wote.

Town planner ni mtetezi wa kila mtu anayetumia Ardhi iwe ya mjini au kijijini.. anahakikisha hakuna anayeonewa au kukandamizwa. Na kunakuwa hakuna prejudice kwenye namna raailiyza serikali zinatumika ili kuleta maendeleo endelevu na kuyatafsiri katika maisha ya watu.

Town planner ni rafiki wa wananchi anayeibua mahitaji yao na kuwasaidia kuformulate dira na njia ya kuyafikia au kufungua possibilities za kuitimiza ndoto na kuboresha kesho yao.

Lakini pia ni rafiki wa watawala kuwasaidia kuchuja mawazo sahihi kutoka kwa wananchi na kusaidia kuyatengenezea mipango wakati huo huo wakiwa no tool ya kusaidia watawala kutafsiri sera na mipango yao kwa namna yenye tija kwa wananchi.

Town planner ni Daraja, Msafiri akifika salama na kwa haraka, anayemwagiwa sifa ni Gari, Dereva na Barabara...ila tuu Mvua zinapokuwa kubwa sana na Daraja likaondoka, anayelaumiwa na safari always ni Daraja, na sio barabara.

Kama taifa kwa Sasa aliyeondoa utaratibu wa kuwatumia matown planner kwenye nyadhifa za utendaji wa miji na majiji alikosea pakuwa.. hakuna taaluma selfless kama taaluma ya mipango miji. Hawa wengine wote ni wachuuzi na ndio walioharibu miji.
 
Tatizo la Tanzania ni kuendekeza ujinga na umasikini
 
Tatizo la Tanzania ni kuendekeza ujinga na umasikini
Inawapa ukurugenzi wa uendelezaji miji Mainjinia na Social studies ...hawajui lolote kuhusu kuendeleza miji kwa kuanzia. Ndio maana wanakuwa kama headless chickens kila ngoma wanacheza.. mama akisema kitu wote mbio huko, wakisia madawati wote huko, aakisikia mapato wote huko...maana to be honest hawajui wanafanya nini ofisini zaidi ya kusimamia day to day.

Hapa Chama kilifeli...lazima kiangalie upya suala hili. La si hivyo kutafeli zaidi na pakubwa zaidi
 
Back
Top Bottom