Lord Diplock MR,
Hivi Chadema kwa Mfano ina Mwenyekiti?
Nilikua kila siku nasema Mbowe ni CCM aliyepo Chadema kwa manufaa yake kibiashara.
Nikawa nashambuliwa kwa maneno makali.
Mbowe amekwapua pesa zote za Ruzuku kwa miaka mitano na kufanya mambo ya hovyo na kujikuta akikiingizia Chama hasara kwa makesi ya ajabu ajabu.
Muda wote hapakuwa na kesi yoyote ya kikatiba dhidi ya matukio ya wazi yaliyokuwa yakifanyika.
Mfano Kuna Mkubwa mmoja wa Polisi alijitokeza wazi kufanya siasa kinyume na katiba ya nchi.
Hatukuona Chama chochote kikitumia ruzuku yake kufungua kesi ya kikatiba kwa hilo juu ya huyo kiongozi.
Miaka yote watu wanapita bila kupingwa na hawapigiwi kura lakini hakuna Chama kilichohoji mahakamani uhalali wa Mbunge wa jimbo kuwawakilisha wananchi bila Kupigiwa kura kinyume na katiba matokeo yake ni kukua kwa hilo joka kuu la kupita bila kupingwa?
Sasa imekua ni kubaki kulalamika tuu kama wanafunzi wa form two.
Miaka mitano bila mikutano ya kisiasa tulitegemea Chama kiwe na fedha za kutosha.
Bila pesa nani atawaunga mkono kwenye mapambano dhidi ya udhalimu. Hata wakati wa kudai Uhuru palikua na matajiri waliodhamini mpambano ule kwa kuchanga pesa.
Nani atakua tayari kufungwa au kuuawa au kujeruhiwa na kuiacha familia yake ikiteseka kwa sababu eti Wapinzani wamekosa ubunge ambao wanufaika wa kwanza ni wao na familia zao.
Hamuwezi kunielewa mana mmeshupaza shingo kama CCM walivyoshupaza japo wao wana nguvu ya dola nyuma yao na kiburi kimewajaa huko wapinzani wakijawa na woga na ubinafsi ulioongozwa na Mbowe kwa miaka 5 na sasa matokeo yake ni kukosekana kwa mikakati insyotekelezeka kwa Chadema. ACT wao bado ni wachanga kifedha.
Kwa sasa Kila Mkurugenzi na msimamizi wa Tume anajitafutia namna ya kupiga pesa toka kwa Wagombea wenye pesa wa CCM ili awaengue wapinzani na mgombea wa CCM apite kirahisi sana. Ni Mradi mzuri sana kwa mwaka huu kuliko miaka yote.
Wakurugenzi wanaosimamia haki wapo kwenye sintofahama kama wanamfurahisha Bashiru na Polepole au laa. Wale wanaowaengua wapinzani ni wazi kuwa wanawafurahisha sana na kuonekana kuwa wanakipigania Chama. Baada ya uchaguzi watapandishwa vyeo na kufurahia udhalimu wao huku familia zao zikiishi kwa raha na furaha na maisha bora na wale waliotenda haki watatolewa na kuishi kwa tabu kwa sababu ya kusimamia haki.
Kama hamuwezi kupambana nao basi unganeni nao tu mule bata.
Kama tungekua na viongozi wa Upinzani waadilifu kabisa kama alivyo Tundu Lisu basi wananchi wangeingiwa na roho za kijasiri kwa uwezo wa Mungu wa haki na kila mtu dhalimu asingepewa nafasi hata dakika moja ya kufurahia udhalimu wake kwa namna yoyote.
Mtu anafanya mambo ya kuhatarisha amani ya nchi kwa makusudi kabisa tena kwa rushwa ya fedha na cheo halafu anawaita polisi ili watumie nguvu kuwadhuru wenye haki yao na yeye anarudi nyumbani kwake kwa furaha na Kitita cha Pesa na kupongezwa na familia kuona kumbe kutumikia matakwa ya CCM inalipa sana.
Nani atawatendea haki wapinzani kwa hali hiyo?
Eti mnataka kujitoa kwenye uchaguzi kabla ya kuwatoa waliovuruga uchaguzi kwa tamaa zao za kutaka vyeo na fedha!!
Jambazi hata akiwa rafiki yako hua hafai kuachwa mana siku ya kutenda ujambazi akikukuta kwenye tukio hakuachi ,unakua wa kwanza kuuawa.
Kuwaacha salama madhalimu ni kuzidisha kizazi cha madhalimu. Kama wahuni walipewa 20000 ili washambulie mkutano wa Chadema inakuaje MTU akipewa million 100 dhidi ya dhalimu.
Bora mjitoe tu watu waendelee na shughuli zao.
Mana huu woga wa CCM iliyofanya makubwa hatuelewi unatokana na nini?
Bila shaka ni nia ya dhati ya kuondoa upinzani wa kivyama yaani upinzani usiwepo Bali ubaki ni watu wanajipendekeza kwenye Chama kimoja.
Nchi itarudi utumwani na huenda hata nchi ikatawaliwa kifalme na ukabila ukawa mkubwa sana.